Nini maana ya kulala chini unapofiwa?

Nini maana ya kulala chini unapofiwa?

Kwa sisi waxaramo unapofiwa kuanzia siku ile ya kwanza ya msiba mtalala chini kwenye mkeka siku tatu hii tunaita kukaliza maiti siku yatatu asubuhi na mapema tunaamka kwa pamoja tunafagia uwanja pamoja na vyumba vyote walivyolala wafiwa takataka zote tunaweka kwenye sufulia tunachanganya na majivu bibi au shangazi atahusika kubeba kichwani tunaongozana wote kwa pamoja aliebeba sefulia akiwa ametangulia mbele hadi makabulini anatupa sefulia pamoja na uchafu wake haraka sana tunageuza na kuludi nyumbani hiii humaanisha maladh yoyote aliyougua marehemu yasijiludie kwa mwanafamilia mwingine.

Kama alikufa kwa ajali je
 
Nakubaliana na waliosema watu hulala chini kwavile vitanda haviwezi kutosha kwa watu wote wanaokuja kwa ajili ya msiba.

Ila sasa hiyo mila ya wazaramo nayo kiboko!
 
Hiyo na mila na utamaduni wa baadhi ya makabila hapa Tanzania, sio kweli kwamba vitanda havitoshi, ila ni alama(symbol) kwamba marehemu yuko chini hivyo na sisi tuonyeshe kwamba tuko pamoja Nate, hata kama ametangulia mbele ya haki, alikuwa siku zote analala kitandani lakini siku zake za mwanzoni kuondoka duniani inabidi tuwe naye kwa kuonesha kwamba pamoja na kwamba umekufa lakini sisi tuko pamoja na wewe, ni mila, no utamaduni na wala sio ushirikina kabisa
 
In sawasawa na baadhi ya makabila wanapokuanza kunywa pombe lazima waimwage chini angalau kidogo, ni mila, ni utamaduni,


Mila zinatofautiana kutokana na makabila na maeneo, mila fulani inaweza isikubaliane na wewe kwasababu sio mila yako, mfano, kurithi make wa kaka yako, kutema mate kila unapoonana na albino, kusali kabla ya kula, so lazima wewe uamini lakini wengine wanaamini kwasababu ni mila zao, na wewe huamini kwasababu sio mila zako.
 
Kwa sababu wahudhuriaji ni wengi vitanda havitoshi. Labda uvipange kama hospitali. Gharama hiyo utaiweza.
 
Nina uhakika humaanishi watu wote msibani hulala chini na kucha vitabda visitumike? Ninachojua ni kuwa kwa vile msibani wanakuja watu wengi na ile sio nyumba ya wageni ni obvious vitabda havitawatosha na hivyo lazima watu walale chini. Nothing special.

Na makochi kutolewa sponchi ili wakalie chaga nini tafsiri yke?
 
Natumai sufuria inakua kuukuu au iliyotoboka na kuwekewa viraka, sio mpya non stick.
 
Kwa sisi waxaramo unapofiwa kuanzia siku ile ya kwanza ya msiba mtalala chini kwenye mkeka siku tatu hii tunaita kukaliza maiti siku yatatu asubuhi na mapema tunaamka kwa pamoja tunafagia uwanja pamoja na vyumba vyote walivyolala wafiwa takataka zote tunaweka kwenye sufulia tunachanganya na majivu bibi au shangazi atahusika kubeba kichwani tunaongozana wote kwa pamoja aliebeba sefulia akiwa ametangulia mbele hadi makabulini anatupa sefulia pamoja na uchafu wake haraka sana tunageuza na kuludi nyumbani hiii humaanisha maladh yoyote aliyougua marehemu yasijiludie kwa mwanafamilia mwingine.

Hapo labda mnachoweza kuzuia kwa njia hiyo ni ugonjwa wa kuku lakini wa binadamu acheni mtamaliza kutupa masufuria tu ndg zangu.
 
Ni kuomboleza zaidi. Kitandani utajisahau utalala kwa raha zote wakati ni wakati wa majonzi. Ukilala chini usiku unakuwa mrefu wa kujigeuzageuza kwa hivi unakuwa wakati mzuri wa kutafakari lililopo mbele yenu
 
Me Mila yangu ni Uislam, tofauti na hapo sina mila ingine,
Mtu akifa, azikwe siku ile ile labda km kafa ucku au jion sana, kumsengenya maiti,





















Unapokufa ndio unapozikiwa,
Kulia ruksa ila kuomboleza haifai kwan unakufuru, mf. "baba/mama umeondoka, nitaishi vipi mimi jamani, nani atanitunza, bora tungeenda wote...."
"mume wangu jaman, umeniacha kwanini, nimeumbuka jaman uwiii, Mungu ungenichukua mimi ukamuacha yeye, watoto hawa watatu nawalea vp mimi maskini...."
Baada ya kuzika majiran warudi makwao wabaki ndugu kujadili mustakabali mzima.
Na mengineyo.
 
Kwa sisi waxaramo unapofiwa kuanzia siku ile ya kwanza ya msiba mtalala chini kwenye mkeka siku tatu hii tunaita kukaliza maiti siku yatatu asubuhi na mapema tunaamka kwa pamoja tunafagia uwanja pamoja na vyumba vyote walivyolala wafiwa takataka zote tunaweka kwenye sufulia tunachanganya na majivu bibi au shangazi atahusika kubeba kichwani tunaongozana wote kwa pamoja aliebeba sefulia akiwa ametangulia mbele hadi makabulini anatupa sefulia pamoja na uchafu wake haraka sana tunageuza na kuludi nyumbani hiii humaanisha maladh yoyote aliyougua marehemu yasijiludie kwa mwanafamilia mwingine.
Vp kama marehemu hakuugua??
 
Haina maana ni kwakuwa nyumba inakuwa na wageni wengi mkilala vitandani hamtoshi
 
Wanamsikindikiza kwa kulala chini km maiti inavolazwa sakafuni
 
Back
Top Bottom