Nini maana ya kulala chini unapofiwa?

Nini maana ya kulala chini unapofiwa?

Kwa sisi waxaramo unapofiwa kuanzia siku ile ya kwanza ya msiba mtalala chini kwenye mkeka siku tatu hii tunaita kukaliza maiti siku yatatu asubuhi na mapema tunaamka kwa pamoja tunafagia uwanja pamoja na vyumba vyote walivyolala wafiwa takataka zote tunaweka kwenye sufulia tunachanganya na majivu bibi au shangazi atahusika kubeba kichwani tunaongozana wote kwa pamoja aliebeba sefulia akiwa ametangulia mbele hadi makabulini anatupa sefulia pamoja na uchafu wake haraka sana tunageuza na kuludi nyumbani hiii humaanisha maladh yoyote aliyougua marehemu yasijiludie kwa mwanafamilia mwingine.

Nyie watani tunafahamu huwa ni uvivu tu wa kutandika kitanda pia mnapenda kulala chini misibani kwani chini mnalala wengi ili Mchonge hadi asubuhi.
 
Hahahaaa kwi teh kuchonga kweli tunachonga ila kwa uvivu wa kutandika vitanda apana
 
Msibani mkusanyiko wa watu ni mkubwa nafasi kubwa inahitajika vyumbani na nje ila watu wakutosha waenee vyumbani na nje kwa iyo kulala kitandani ni sawa kuwa na dawati moja darasani wakae watatu wakati wengine wakae chini!!!
 
Sisi kwa mila zetu tukifiwa hatuogi wiki nzima, u can imagine the smell now...
 
Sisi kwa mila zetu tukifiwa hatuogi wiki nzima, u can imagine the smell now...

Wacha utani, ujue tunajadili kufiwa humu! Dada hiyo mila kwa wote au watoto tu?
 
Nafikiri pamoja na mazingira pia ni ishara ya kuomboleza

Kwenye vitabu vya dini tunaoneshwa zamani kipindi cha maombolezo walikuwa wanavaa magunia na kunyoa nywele pia

Dini gani hizo..maana kwenye Uislam hakuna kitu kama hicho.
 
Kwa sisi waxaramo unapofiwa kuanzia siku ile ya kwanza ya msiba mtalala chini kwenye mkeka siku tatu hii tunaita kukaliza maiti siku yatatu asubuhi na mapema tunaamka kwa pamoja tunafagia uwanja pamoja na vyumba vyote walivyolala wafiwa takataka zote tunaweka kwenye sufulia tunachanganya na majivu bibi au shangazi atahusika kubeba kichwani tunaongozana wote kwa pamoja aliebeba sefulia akiwa ametangulia mbele hadi makabulini anatupa sefulia pamoja na uchafu wake haraka sana tunageuza na kuludi nyumbani hiii humaanisha maladh yoyote aliyougua marehemu yasijiludie kwa mwanafamilia mwingine.

Huu sasa ni ushirikina
 
Sio utani ni kweli, ni kwa watu wote lakini hiyo mila Siku hizi haitekelezwi ila ilikuwepo

Daaah, nawaza kwa sauti hapa, mtu asieoga 1 week anavokuwa! Daah, km unaenda ofisini hapo....!
 
Daaah, nawaza kwa sauti hapa, mtu asieoga 1 week anavokuwa! Daah, km unaenda ofisini hapo....!
Mama yangu aliniambia hizi habari, na wao walikuwa wanatoroka kwenda kuoga mtoni, lakini hairuhusiwi kuoga mpk mtakapovunja matanga.
 
Mama yangu aliniambia hizi habari, na wao walikuwa wanatoroka kwenda kuoga mtoni, lakini hairuhusiwi kuoga mpk mtakapovunja matanga.

Inawezekana! Nchi kuna mila nyingi sana za kushangaza! Sisi kwetu ilikuwepo ile ya kila anaekufa, lazima wazee waende kwa MTAALAMU kuulizia chanzo CHA kifo husika! Lkn baadae watu waliacha baada ya wanamapinduzi kushika hatamu za ukoo!
 
Habari wana JF.

Naomba kuuliza, hivi nini maana haswa ya wafiwa kulala chini kipindi cha msiba? Hii ni kwa baadhi ya makabila.

Mara zote kwenye msiba kunakuwa na mkusanyiko wa watu wengi ambao huwa wanakuja kuwafariji wafiwa
Nyumba husika ktk msiba huwa inapokea watu wengi kuliko uwezo wake, hapo ndipo linapokuja suala la kulala chini na ikibidi nje
Ni mazingira tu yanayo tulazimisha
 
Nina uhakika humaanishi watu wote msibani hulala chini na kucha vitabda visitumike? Ninachojua ni kuwa kwa vile msibani wanakuja watu wengi na ile sio nyumba ya wageni ni obvious vitabda havitawatosha na hivyo lazima watu walale chini. Nothing special.

Umemaliza mkuu hakuna zaidi ya hapo.
 
Huu sasa ni ushirikina
mila nyingi za kibantu zinafanana, mimi nimetoka arusha na tunafanya hivyo ila baada ya kufagia uchafu tunauweka chini ya mgomba na baadae ndizi ikikomaa tunatengeneza pombe
 
Back
Top Bottom