Nini maana ya hekima na ninawezaje kuipata?

Sitatoa maana yake, ila
Hekima yakupa uwezo wa kuwafanya watu waliokuzunguka/ wanaokusikiliza kuweza kubaini nini cha kufanya na kuacha, ili watu/ jamii izidi kustawi na ushirikiano uwe na manufaa na kupunguza chuki ikiwezekana kuitokomeza kabisa.

Hekima hustawisha misingi bora ya kijamii. Hekima hutumika kusululisha matatizo na kuwaasa wanajamii.
Ukiwa na hekima vita ndogondogo unazimaliza bila kuingia uwanjani.
 
Hekima upatikana kwa mlolongo ufuatao; kwanza katika maisha ya kila siku watu hujifunza kwa makosa (mistakes) yao wao wenyewe au kwa makosa ya wengine, hili uzaa uzoefu (experience) na mwisho experience uzaa hekima (wisdom). Kiufupi huo ndio mlolongo wake na wengi wanaokuja kuwa na hekima hujifunza mengi toka makosa ya wengine kuliko makosa yao wenyewe. Hayo yote upatikana baada ya muda mrefu kidogo wa kuishi hapa duniani na si kitu cha ghafla au cha kupata darasani.
 
Fanya Reasoning kabla hujaamua chochote hii ujenga kiwango cha juu cha busara matokeo yake uzaliwa Hekima ndani yake.
Hapa Pia lazima ujue kipi kinaanza kati ya BUSARA na HEKIMA pamoja na utegemeano wake,sababu unaweza ku reason kitu ambacho ni kinyume na reality na ukajikuta katika jambo lililo kinyume na hekima.Kiuhalisia muhusika ameleta mada pana mnoo 😅😅😅
 
Hekima au Hikmah ni mtu kuweza kutoa maamuzi ya haki bila kuegemea upande wowote
Kujua mambo mengi na kuyapambanua vizuri
Mtu mwenye hekima anaweza kutatua tatizo baina ya watu bila kukosea
Knowledge of the reality of things
Hekima ni mtu kuwa WISE na wisdom kama ntaeleweka
Jitahidi kusoma vitabu ambavyo vinaendana na career yako, pia kureason kabla ya kufanya maamuzi ni muhimu sana!
 
Habari wana JF,

Mimi ni mgeni hapa jamvini, nomba niende moja kwa moja kwenye mada kama hapo juu inavyosema.

Ninaomba kujua hekima maana yake nini na ninawezaje kuipata.

Karibuni wakuu.
Labda nikujibu mkuu kwa uelewa wangu.
HEKIMA ni neno dogo sana kimatamshi, lakini ndani yake limebeba ujumbe mpana katika maisha ya mwanadamu.

Hekima pia, ni uwezo wa kutambua Jambo/ mambo yanayofaa na yasiyofaa.

Mtoto mdogo anapozaliwa, anajifunza kutamka/kuongea kabla hajafundishwa shule. Anakuwa na uwezo wakupambanua mambo mfano kwa jambo baya utamuona akilia kumaanisha ni dalili ya hatari ( Jambo lisilo faa kwake).

Kwa maana nyepesi hapo nikwamba HEKIMA mtu anazaliwa nayo.

Asilimia kubwa ya watu walioishi miaka mingi, hujawa na hekima kutokana na mapito yakimaisha walio yapitia.

Mtu alie jawa na hekima, aendeshwi katika maisha badala yake hekima inamuongoza katika kila hatua anayoiwaza kuichukua.

Ukijawa na hekima, utatenda mambo baada ya kufikiri na ndio maana utaona mtu mwenye kushikilia jambo moja alilokusudia kulifanya! Ndiye mwenye nafasi kubwa yakufanikiwa kuliko yule mwenye kuunga unga mambo.

Itaendelea maana hekima ni somo pana
 
Jitahidi kusoma vitabu ambavyo vinaendana na career yako, pia kureason kabla ya kufanya maamuzi ni muhimu sana!

Kusoma vitabu ni knowledge na hekima ni mtu kuwa wise nafikiri ni vitu viwili tofauti ambavyo kidogo vina uiano ila kuwa na Hekima ni mtu mzima sio wote ndio maana kama kuna tatizo kubwa kuna mtu au mzee watamuendea na yeye ndio ana uwezo wa kutatua mambo kutokana na uwezo wake wa kuchambua mambo na kutoa uamuzi sahihi
Hili sio lazima mtu awe na degree ila wapo wazee mpaka vijijini ambao ni very wise na ndio wanategemewa na jamii inayowazunguka kwa kutatua matatizo yao mengi
Kwa mimi ndio ninavyoelewa maana ya hekima
Niongezee mengine mkuu
 
Hekima uwezo unazaliwa nao,Ili uwe na Hekima timilifu lazima ;
i utafakari (fikiri kabla ya kutenda /kunena)
ii Experience

iii Upambanue (Jema/Baya/kwanini)

 
jambo la kwanza make sure unakuwa positive katika kunena na kutenda kwako"..jitahidi kusoma falsafa ...anza kuwa fuatilia watu kama kina aristole..da vince.dalai lamar etc
 
Kwa Wakristo maandiko yanasema "hekima ya masikini haisikilizwi". Tafuta hela utakuwa na hekima na kila utakalosema ili mradi unahela litasikilizwa na kutendewa kazi. Hii ndiyo Hekima haswaa! Nyingine ni kupoteza muda
 
Habari wana JF,

Mimi ni mgeni hapa jamvini, nomba niende moja kwa moja kwenye mada kama hapo juu inavyosema.

Ninaomba kujua hekima maana yake nini na ninawezaje kuipata.

Karibuni wakuu.

Hekima ni uwezo wa
kuteua malengo ya kudumu na kutengua malengo ya mpito,
kutofautisha kati ya
mbinu na malengo, kuchagua mbinu zinazoweza kuleta ufanisi wa malengo yaliyoteuliwa na kubagua mbinu baki, kuchuja
mbinu na malengo mema dhidi ya
mbinu na malengo mabaya, na hatimaye kichukua hatua.
 
Back
Top Bottom