Nini lengo la VTS na kwanini isiwe speed governor?

Nini lengo la VTS na kwanini isiwe speed governor?

DJkus

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2018
Posts
354
Reaction score
470
Habari wana jamvi!

Moja kwa moja nijikite kwenye mada.

Mosi, kumekuwa na heko kwa serikali kutokana na hizi Vehicle Tracking System (VTS) bila kujali utendaji kazi wake na namna unavyoweza kudhibiti mwendo.

Kazi yake ni kumtaarifu dereva anapopitiliza speed zaidi ya 85km/hr lakini sio kupunguza mwendo kama wengi wanavyodhani ndio maana vinapiga kelele.

Hii utaiona kwenye baadhi ya magari na madereva wanaokimbia bila kuzingatia hicho king'ora, mpaka abiria unasikia kukerwa sana na hizo kelele za mfululizo bila kukoma.

Hali ingekuwa tofauti kama wangetumia speed governor maana yenyewe inadhibiti mwendo kwenye speed iliyochaguliwa. Na hapa ingesaidia wahisani wote bila kujali ni nani kwa manufaa ya wote!

Pili, gharama; jamani kiuhalisia bila kumumunya maneno gharama ni kubwa sana na bado kila mwezi wanalipia token. Hivi kweli hizi gharama serikali haizioni? Au nao wako na mgao au ndiyo biashara ya serikali kupitia mgongo wa VTS, au ni kukandamiza wamiliki wa magari hasa mabasi bila kuwa na mbadala wa uchaguzi wa gharama!

Serikali na wahisani kwa ujumla fikirieni hili kwa maslahi ya kumnufaisha kila mmoja. Kwa hili ni wapi mmiliki anafaidika? Nafuu yake iko wapi?

Mbaya zaidi mfumo wake wa kukuwajibisha wahalifu wa speed, hauko intact dereva anafanya kosa leo anakuja letewa faini baada ya miezi mitatu. Kama ni maafa tayari yameshatokea na mhalifu ameshatokomea.

Unakuta hata dereva alishaacha kazi au alifukuzwa kutokana na mambo mengine hapo ndipo mzigo unaenda kwa mmiliki kama ulivyo. (Hapa lengo ni kumuonya dereva au mmiliki?).

Badala yake mfumo wa speed governor ni rafiki kwa umma na watumiaji wengine wa barabara.
Hili ni swala la dereva na mfumo wa gari hawezi kwenda zaidi maana gari imepangiwa speed yake na haiwezi kwenda zaidi ya hapo.

Kwa ucheche niishie hapa.

Karibuni.
 
Ni mbinu za kula pesa, kuna vifaa vimefungwa Ubena na Bwawani njia ya Dar Morogoro, havijulikani vinapima nini, japo wanasema vinadhibiti matumizi mabaya ya barabara lakini siku hizi mabasi yanapita na speed 100
 
Ni mbinu za kula pesa, kuna vifaa vimefungwa Ubena na Bwawani njia ya Dar Morogoro, havijulikani vinapima nini, japo wanasema vinadhibiti matumizi mabaya ya barabara lakini siku hizi mabasi yanapita na speed 100
Mambo yapo kwa speed governor ndio baba lao!! Yaani wanaiba hela za watu bila kujali wala aibu na serikali inazidi kulibariki
 
Kwa mtazamo wangu, hii naiona ni biashara kama biashara yeyote.
Sababu kubwa ya mimi kuita biashara in pale wanapo subiria chuma ivuke kiwango kinacho kubalika ili wapate faini.
Jamaa hawana maana hata kidogo hawa. Zaidi sana ni wachumia tumbo kwa kisingizio cha udhibiti mwendo
 
Bado Serikali inatumia makosa ya barabarani kama kitega uchumi. Safety rules hazifanyi kazi namna hiyo tu. Kuna kuonya, mbona hili la kuonya halifanyiki?
 
Ni mbinu za kula pesa, kuna vifaa vimefungwa Ubena na Bwawani njia ya Dar Morogoro, havijulikani vinapima nini, japo wanasema vinadhibiti matumizi mabaya ya barabara lakini siku hizi mabasi yanapita na speed 100
wanadai ni camera
 
Bado Serikali inatumia makosa ya barabarani kama kitega uchumi. Safety rules hazifanyi kazi namna hiyo tu. Kuna kuonya, mbona hili la kuonya halifanyiki?
Wameshika pabaya!! Wako mchawi Karaba na mnyama wake anayezuia maji yasitiririke kwenye kijiji cha akina kirikuu!!
 
Zinaoza tu na jua
Wanawakamua watu kwa manufaa ya genge fulani huku wananchi tumeachwa tuhangaike na hata tunachikihangaikia wanatupokonya bila kujali nguvu iliyotumika!!
 
VTS imesaidia sana kudhibiti mwenda na ajali zitokanazo na mwendokasi.

Ila ile alarm wameweka inakera sana. angalau wangeweka beep tone .

Ila pia nakumbuka kuhusu SPEED GOVERNOR wamiliki wa magari walisema zinachosha engine.

Tatu, niseme tu hiki ni kitega uchumi tu, mini-TRA
 
VTS imesaidia sana kudhibiti mwenda na ajali zitokanazo na mwendokasi.

Ila ile alarm wameweka inakera sana. angalau wangeweka beep tone .

Ila pia nakumbuka kuhusu SPEED GOVERNOR wamiliki wa magari walisema zinachosha engine.

Tatu, niseme tu hiki ni kitega uchumi tu, mini-TRA
Mkuu hii ni over TRA, 650,500 kwa kila bus + 30,000 kila mwezi!!! Kweli huu sio uonevu??
 
Habari za Muda huu Mkuu,

Ulijaribu kufikiria ni vipi endapo yakatokea mazingira ambayo yanamhitaji dereva kukimbia speed zaidi ya iliyowekwa kwenye SG? Labda tuchukulie watu wenye nia ovu wanalikimbiza Basi lililofungwa kifaa hiko au labda kukawa kwa bahati mbaya mama mjamzito ambaye anahitaji msaada wa haraka na ni eneo ambalo wapo ni mbali na Huduma za afya au labfa hata Mgonjwa akawa anahitaji msaada wa haraka.
 
Back
Top Bottom