Nini lengo la VTS na kwanini isiwe speed governor?

Nini lengo la VTS na kwanini isiwe speed governor?

Habari wana jamvi!

Moja kwa moja nijikite kwenye mada.

Mosi, kumekuwa na heko kwa serikali kutokana na hizi Vehicle Tracking System (VTS) bila kujali utendaji kazi wake na namna unavyoweza kudhibiti mwendo.

Kazi yake ni kumtaarifu dereva anapopitiliza speed zaidi ya 85km/hr lakini sio kupunguza mwendo kama wengi wanavyodhani ndio maana vinapiga kelele.

Hii utaiona kwenye baadhi ya magari na madereva wanaokimbia bila kuzingatia hicho king'ora, mpaka abiria unasikia kukerwa sana na hizo kelele za mfululizo bila kukoma.

Hali ingekuwa tofauti kama wangetumia speed governor maana yenyewe inadhibiti mwendo kwenye speed iliyochaguliwa. Na hapa ingesaidia wahisani wote bila kujali ni nani kwa manufaa ya wote!

Pili, gharama; jamani kiuhalisia bila kumumunya maneno gharama ni kubwa sana na bado kila mwezi wanalipia token. Hivi kweli hizi gharama serikali haizioni? Au nao wako na mgao au ndiyo biashara ya serikali kupitia mgongo wa VTS, au ni kukandamiza wamiliki wa magari hasa mabasi bila kuwa na mbadala wa uchaguzi wa gharama!

Serikali na wahisani kwa ujumla fikirieni hili kwa maslahi ya kumnufaisha kila mmoja. Kwa hili ni wapi mmiliki anafaidika? Nafuu yake iko wapi?

Mbaya zaidi mfumo wake wa kukuwajibisha wahalifu wa speed, hauko intact dereva anafanya kosa leo anakuja letewa faini baada ya miezi mitatu. Kama ni maafa tayari yameshatokea na mhalifu ameshatokomea.

Unakuta hata dereva alishaacha kazi au alifukuzwa kutokana na mambo mengine hapo ndipo mzigo unaenda kwa mmiliki kama ulivyo. (Hapa lengo ni kumuonya dereva au mmiliki?).

Badala yake mfumo wa speed governor ni rafiki kwa umma na watumiaji wengine wa barabara.
Hili ni swala la dereva na mfumo wa gari hawezi kwenda zaidi maana gari imepangiwa speed yake na haiwezi kwenda zaidi ya hapo.

Kwa ucheche niishie hapa.

Karibuni.


HAHAHAAAAAAA
LEO MIDA HII NASAFIR KUTOKA DAR KWENDA MWANZA NIMEKAA SITI YA MBELE NAONA JAMAA/DEREVA ILE CABLE YA SPEED-METER INAYOONYESHA SPIDI YA GARI IMEFETULIWA ( YANI IKOKWENYE ZERO) HAKUNA KING'ORA WALA NINI NIKICHUNGULIA NJE BASI INATEMBEA SO MCHEZO. NIMEMUULIZA KONDA KANIAMBIA WAMEIDISCONECT ILI DEREVA AWE HURU KUKANYAGA ACCELERATOR.
YANI. SERIKALI INAJITAHIDI HUKU NAO WANABUNI MBINU MPYA ZA .KUTEMBEA KWA KASI
 
HAHAHAAAAAAA
LEO MIDA HII NASAFIR KUTOKA DAR KWENDA MWANZA NIMEKAA SITI YA MBELE NAONA JAMAA/DEREVA ILE CABLE YA SPEED-METER INAYOONYESHA SPIDI YA GARI IMEFETULIWA ( YANI IKOKWENYE ZERO) HAKUNA KING'ORA WALA NINI NIKICHUNGULIA NJE BASI INATEMBEA SO MCHEZO. NIMEMUULIZA KONDA KANIAMBIA WAMEIDISCONECT ILI DEREVA AWE HURU KUKANYAGA ACCELERATOR.
YANI. SERIKALI INAJITAHIDI HUKU NAO WANABUNI MBINU MPYA ZA .KUTEMBEA KWA KASI
Mwisho wa reli ni mwanzo wa bandari, mwisho wao ni mwanzo wa wengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee baba unataka kuniambia nikipanda abood kutokea ubungo saa kumi na mbili alfajiri nitafika msamvu saa sita kamili mchana? Ilhali nikipanda bm nitafika saa tatu na nusu asubuhi msamvu??
basi za Abood madereva wengi wako aged, wa zamani, wanaendesha kistaarabu kwa spidi ya kobe mno, nimepanda several times ndani ya wiki 3 mfululizo mengi yalikua yanachukua masaa 6,

madereva wa BM karibia wote ni vijana, hawarembi wakiwa road, uwe na roho ngumu na uwe tayari kwa kukisikia kile ki beep alarm kikipiga mda wote, ng'wi ng'wi ng'wi ng'wi
 
basi za Abood madereva wengi wako aged, wa zamani, wanaendesha kistaarabu kwa spidi ya kobe mno, nimepanda several times ndani ya wiki 3 mfululizo mengi yalikua yanachukua masaa 6,

madereva wa BM karibia wote ni vijana, hawarembi wakiwa road, uwe na roho ngumu na uwe tayari kwa kukisikia kile ki beep alarm kikipiga mda wote, ng'wi ng'wi ng'wi ng'wi
Kumbe Dar Morogoro masaa sita siku hizi aisee[emoji848][emoji848]

Pongezi ziende kwa awamu ya 5 kufanikisha hili na kupunguza ajali.

79966689_484325809107216_998533648112156672_n.jpeg
 
Ila kimetupunguzia ligi barabarani..hasa za mabasi!
 
Ila kimetupunguzia ligi barabarani..hasa za mabasi!
Wangetumia njia rafiki kwa wote sio hiyo kandamizi.

Kama kweli ni kupunguza ligi wawashauri wamili wanunue popote hizo VTS.

Halafu kwa nini 30,000 kila mwezi?

Kwa nini iwe 650,500? Kwa kila gari?

Bei kapanga mwenyewe
Na matumizi kapanga mwenyewe!




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ligi bado zipo kama kawa kama dawa[emoji41]

Angalia hizo picha zote kwa umakini kisha unambie kama hamna ligi hapo
FB_IMG_1567634410856.jpeg
79921562_2811632795537078_1221556881588224000_n.jpeg
FB_IMG_1569590601263.jpeg
FB_IMG_1569590536836.jpeg
FB_IMG_1565926444630.jpeg
FB_IMG_1558773898117.jpeg
FB_IMG_1558088644649.jpeg
FB_IMG_1559652446026.jpeg
FB_IMG_1558088150858.jpeg
FB_IMG_1558773928722.jpeg
 
Asante mkuu na wenye VTS wanaona nazo VTS zinajiona!

Nani anajali kati ya uhuni huu na uhalisia wa mambo[emoji1745][emoji1745] wao ni heri mkono umenona.

Hapo wanachekelea[emoji1787][emoji1787][emoji1787] na kusema wajinga ndio waliwao!!! Na kweli wanawala kisawa sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom