Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Mojawapo ya sababu ambazo zilitolewa kuhalalisha posho za wabunge ni kuwa wanahiatji kutoa misaada kwenye majimbo yao. Na miaka nenda rudi tumeona wabunge na wale wanaotaka kugombea ubunge wakitoa misaada mbalimbali kwenye majimbo yao. Jambo hili limezoeleka sana kiasi kwamba ni kawaida sasa. Najiuliza hata hivyo misaada hiyo kweli ni ya lazima?
Jimbo hupata fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo
Jimbo linakuwa kwenye Wilaya au hata wilaya zaidi ya moda zinazotengewa fedha katika wizara na idara mbalimbali
Jimbo hilo hilo huweza kuwa na manispaa au halmashauri ya manispaa hata zaidi ya moja inayotengewa fedha na kukusanya fedha
Jimbo hilo hilo hupata fedha kutokana na utekelezaji wa kazi za wizara/idara fulani za serikali
Kwa ufupi, hakuna jimbo ambalo linakosa pesa kabisa kwa kipimo chochote hasa zinazohusiana na shughuli za maendeleo.
Najiuliza hata hivyo itakuwaje kama:
a. Wabunge mara baada ya kuchaguliwa watapigwa marufuku kutoa msaada wowote jimboni kwao unaozidi sema shilingi laki moja kwa mwaka?
b. Watu ambao wanataka kugombea ubunge kwenye jimbo fulani wawe hawajatoa misaada yenye thamani ya zaidi ya shilingi laki tano katika miaka mitatu inayotangulia uchaguzi?
c. Waziri yeyote haruhusiwi kutoa msaada wowote wa fedha au wenye thamani isiyozaidi shilingi laki tano katika jimbo lake.
Ninachojiuliza kama kwenye sheria ya maadili ya viongozi ikipigwa marufuku kwa viongozi kutoa misaada ya namna hiyo itakuwa na matokeo gani? Kama wananchi wanakatazwa kutoa misaada au kuwalipa viongozi wao na kuwapatia zawadi za aina mbalimbali kwanini viongozi nao wasikatazwe? Fikiria kiongozi mwenye fedha nyingi sana anavyoweza kutoa misaada mbalimbali kutoka mfukoni mwake bila kujaribu kulobby au kusababisha serikali ilete huduma au wananchi wenyewe wajipatie vitu fulanifulani kwa kukunganisha nguvu zao n.k
Ni wazo baya au zuri?
Jimbo hupata fedha kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo
Jimbo linakuwa kwenye Wilaya au hata wilaya zaidi ya moda zinazotengewa fedha katika wizara na idara mbalimbali
Jimbo hilo hilo huweza kuwa na manispaa au halmashauri ya manispaa hata zaidi ya moja inayotengewa fedha na kukusanya fedha
Jimbo hilo hilo hupata fedha kutokana na utekelezaji wa kazi za wizara/idara fulani za serikali
Kwa ufupi, hakuna jimbo ambalo linakosa pesa kabisa kwa kipimo chochote hasa zinazohusiana na shughuli za maendeleo.
Najiuliza hata hivyo itakuwaje kama:
a. Wabunge mara baada ya kuchaguliwa watapigwa marufuku kutoa msaada wowote jimboni kwao unaozidi sema shilingi laki moja kwa mwaka?
b. Watu ambao wanataka kugombea ubunge kwenye jimbo fulani wawe hawajatoa misaada yenye thamani ya zaidi ya shilingi laki tano katika miaka mitatu inayotangulia uchaguzi?
c. Waziri yeyote haruhusiwi kutoa msaada wowote wa fedha au wenye thamani isiyozaidi shilingi laki tano katika jimbo lake.
Ninachojiuliza kama kwenye sheria ya maadili ya viongozi ikipigwa marufuku kwa viongozi kutoa misaada ya namna hiyo itakuwa na matokeo gani? Kama wananchi wanakatazwa kutoa misaada au kuwalipa viongozi wao na kuwapatia zawadi za aina mbalimbali kwanini viongozi nao wasikatazwe? Fikiria kiongozi mwenye fedha nyingi sana anavyoweza kutoa misaada mbalimbali kutoka mfukoni mwake bila kujaribu kulobby au kusababisha serikali ilete huduma au wananchi wenyewe wajipatie vitu fulanifulani kwa kukunganisha nguvu zao n.k
Ni wazo baya au zuri?