Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Ni zaidi ya miaka minne sasa, mambo ndani ya klabu ya Simba yanaonekana kuwaendea kombo. Timu ambayo ilijenga heshima Afrika Mashariki na kutisha kwenye mashindano ya CAF, kila siku inaonekana kuzidi kupoteana.
Pamoja na changamoto za kiufundi na usajili, kuna jambo jingine linaloonekana wazi kwa macho ya mashabiki, migogoro kati ya mashabiki,na baadhi ya viongozi wa sasa, na viongozi wastaafu.
Uhalisia wa hali hiyo ulijidhihirisha baada ya sare ya mabao 2-2 dhidi ya Esperance Sportive de Tunis, iliyosababisha kuondolewa kwa Simba katika hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika. Baada ya mchezo huo, mwenyekiti wa klabu, Murtaza Mangungu, alishambuliwa na kunusurika kipigo kutoka kwa mashabiki wenye hasira kali.
Kila msimu mashabiki wanaambiwa, “tunaijenga timu.” Lakini ujenzi huu unaanza lini na unaisha lini? Wachezaji wanakuja na kuondoka bila mwendelezo, makocha wanabadilishwa kabla hata hawajatekeleza falsafa zao, na uongozi unaonekana kama unazima moto badala ya kujenga msingi imara.
Kinachokosekana kinaonekana si pesa, bali ni mwelekeo, utulivu, na dira ya wazi kwani tangu mambo ya transformation yazungumzwe hali bado iko kwenye mkwamo.
Ishu nyingine ni kuongezwa kwa mkataba wa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Simba SC, Zubeda Sakuru, ambapo baada ya mkataba wake wa awali wa miezi sita kumalizika, aliongezewa mkataba wa miaka miwili na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi, Mo Dewji, bila kuishirikisha Bodi ya Wakurugenzi kama inavyotakiwa kisheria, kwa kuwa uteuzi wa CEO hupaswa kupitishwa na Bodi.
Hali hiyo imeibua maswali miongoni mwa baadhi ya wajumbe wa Bodi kuhusu vigezo vilivyotumika katika kumuongezea mkataba huo kwa siri na iwapo aliyetia saini aliridhika kwa misingi gani kwamba anafaa kuendelea na nafasi hiyo, huku wengine wakieleza wazi kuwa hawaridhishwi na utendaji wa CEO wa sasa na wanaona hafai kuendelea kuwa Mtendaji Mkuu wa Simba SC.
Kuna taarifa pia Muwekezaji wa Simba SC, Mo Dewji, ametuma makubaliano ya kukopeshana (loan agreement) kwa CEO wa klabu hiyo, Bi Zubeda Sakuru, ili yasainiwe na kupelekwa kwa mkaguzi kisha kuthibitishwa na Bodi, hatua ambayo ingeifanya Simba Sports Club iwe na deni kwa mwekezaji wake, lakini hadi sasa makubaliano hayo bado hayajasainiwa baada ya kuchelewa kutokana na changamoto za kiafya za CEO na safari ya matibabu nje ya nchi, huku ikielezwa kuwa licha ya kurejea, bado hajasaini kwa sababu ya hofu kuwa kusaini kutaiingiza klabu kwenye madeni.
Nimesoma “TAARIFA KWA UMMA” zote 2 za Klabu ya Simba ambazo moja ilitoka kwa Uongozi wa Simba SC na nyingine kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi, Crescentius Magori, lakini hakuna hata moja iliyojaribu kujibu hoja zilizowasilishwa na wanachama wao.
Yametamkwa mambo mazito kumhusu Rais wa heshima na mwekezaji wa klabu, ndugu Mohammed Gulam-Abbas Dewji, ambayo binafsi nadhani yalifaa kujibiwa kwa hoja na si kwa vitisho. Badala ya kuona majibu ya kina yanayofafanua ukweli wa tuhuma hizo, kilichoonekana ni msisitizo wa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wanaotoa maoni yao.
Kusema watu watapelekwa Polisi kwa kutoa maoni yao ni kujaribu kuzuia uhuru wa kutoa maoni ambao upo kikatiba. Kama kweli watu hawa hawasemi ukweli wowote, kwa nini Bodi haijajibu kwa kukanusha uongo na kuleta ukweli wazi? Kwa nini wanaoshambuliwa ni watoa hoja badala ya hoja zenyewe? Maswali kuhusu kuzimwa kwa simu wakati wa usajili wa dirisha dogo, changamoto za mishahara, na madai ya kukopa fedha kwa ajili ya safari za timu ni mambo mazito yanayohitaji majibu ya wazi, si vitisho.
Hali hiyo imeibua maswali miongoni mwa baadhi ya wajumbe wa Bodi kuhusu vigezo vilivyotumika katika kumuongezea mkataba huo kwa siri na iwapo aliyetia saini aliridhika kwa misingi gani kwamba anafaa kuendelea na nafasi hiyo, huku wengine wakieleza wazi kuwa hawaridhishwi na utendaji wa CEO wa sasa na wanaona hafai kuendelea kuwa Mtendaji Mkuu wa Simba SC.
Yametamkwa mambo mazito kumhusu Rais wa heshima na mwekezaji wa klabu, ndugu Mohammed Gulam-Abbas Dewji, ambayo binafsi nadhani yalifaa kujibiwa kwa hoja na si kwa vitisho. Badala ya kuona majibu ya kina yanayofafanua ukweli wa tuhuma hizo, kilichoonekana ni msisitizo wa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wanaotoa maoni yao.
