Nini kinaendelea kwenye Uchumi wa Tanzania?

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,480
5,506
Kuna watu wenye maoni tofauti kuhusu hali ya kiuchumi ya Tanzania. Kuna wanaofikiri kwamba uchumi wetu kama taifa unayumba na kuna ambao wanasema kwamba uchumi unakua. Katika hali ya kawaida kabisa ni lazima kila anayetoa hoja awe na sababu za msingi na ambazo zitahakikisha kwamba hoja inaeleweka na hatua stahiki zinachukuliwa.

Katika moja ya mapitia yangu nilikutana na hoja ndogo ya usimamizi wa uchumi ambayo inalenga zaidi kuleta fursa za kiuchumi (Unlocking the economy) Kwa kawaida kabisa katika usimamizi wa uchumi kila kauli,maamuzi na matukio yanayotokea katika mfumo wa kisiasa, kijamii na kiuchumi huwa yanaathiri hali ya uchumi katika njia ya faida(gain) au hasara (loss)Kwa hivyo basi tunapoutazama uchumi wa Tanzania ni lazima tuungalie katika namna mbili. Namna ya kwanza ni Macro economic Indicators na Pili ni Micro economic indicators.

Mimi binafsi nikiangalia katika hivyo vyote naona kwamba hali ya uchumi ni nzuri na kama taifa tunaelekea sehemu nzuri.Kufungwa kwa biashara, watu kupoteza au kukosa ajira na biashara kuwa ngumu ni kawaida katika uchumi wa soko ambapo kuna ushindani mkali. Kama biashara imashindwa ushindani basi huwezi kusema ni matatizo ya serikali hapana ila iwapo maamuzi ya serikali ama kisheria au kisera ndo yamefanya biashara hio kuanguka basi unaweza kulaumu serikali na ni lazima kuwa makini katika kutoa lawama hizo kwani kuna uwezkano kabisa kutoa lawana hizo kukawa na madhara zaidi ya kiuchumi.

Pamoja na ukweli huu hapo juu serikali haiwezi kujitoa lawamani kwa yanayotokea katika uchumi kaika kipindi hiki.Tanzania sasa limekuwa taifa la Wamachinga na Wachuuzi. Uchumi wetu umekuwa ni wa madalali, wachuuzi na wauza sura. Hakuna mfumo wa kiuchumi na kisera unaoongoza uelekeo wa taifa. Hii ni hatari.Serikali inapswa kutambua kwamba inapoendelea kuruhusu uchumi wetu kuelekea unakoelekea kuna siku SERIKALI ITAKOSA KODI HALALI YA KUKUSANYA na itaanza kukusanya kodi HARAMU au kodi ya DHULUMA. Kuna siku itafika serikali itshindwa kujiendesha kwa sababu ya ujinga na uzembe wa watendaji katika kushughulikia maswala ya kisera mapema.

Nasema hivi kama mtu ambaye nimeona kabisa hali ilivyo na nikagundua kwamb hali ikiacha kama ilivyo kama taifa tuna hatari kubwa mbele yetu. Swali la kujiuliza ni Je, nini kifanyike?

Kwanza kabisa ni lazimi serikali irekebisha mfumo wa ukusanyaji kodi na maduhuli ili iwe rahisi kulipa.Kisha iondoa ukiritimba katikka kuanzisha na kusimamia biashara.Sioni sababu ya Zoezi la kuanzisha biashara kuwa GUMU. Ukitaka kuanzisha biashara Tanzania unajikuta unatumia muda mwingi na gharama nyingi katika maswala ambayo hayaongezi thamani yoyote katika biashara yako.

Eneo lingine amblo linalohitaji kutazamwa ni eneo la uwekezaji hasa katika miradi ya miundo mbinu.Nasema hivi kwa sababu naona kabisa kama taifa tumewekeza biala mpangoa katika miradi ya miundo mbinu. Ujenzi wa MJi mkuu mpya. Ujenzi wa Miundo mbinu kule Dar es Salaam na katika miko mingine. Swali la kujiuliza je Rasilimali Pesa tulizonazo zinatiosha kuwezesha ujenzi wa miundo mbinu yote hii katika kipindi kifupi? Kama hapana basi ni bora tukaenda hatua kwa hatu huku tukitafuta namba ya kuingiza PESA kwa kuwekeza katika watu wetu na uzalishaji ili tuweze kujenga uchumi shirikishi.

Najua kuna mengi ambayo yanaweza kufanywa na serikali, watu binafsi na wananchi kwa ujumla. Tujadili hapa kwa pamoja kila kinachoendelea katika uchumi wa nchi yetu katika misingi ya uZalendo na Maendelea.

Karibuni.
 
Yaani hata hueleweki, wewe kwa akili yako unadhani uchimi unaharibiw na nani? Yaani machinga ametapakaa kila sehemu unategemea nini hapo mzee?
 
Mleta mada hujui hata umeandika nini, sijui umeandikiwa? Soma upya mada yako, halafu uje kivingine.

Yaani unasema uchumi wetu unakwenda vizuri, lakini mwanzo mpaka mwisho umeandika huku unaonyesha mapungufu ya sheria, taratibu, sera na utendaji unaopelekea kuwa na mchumi mbovu tulionao sasa.
 
Any way uko huru kusema unachojisikia even if hauna uhakika na uchunguzi wa kina juu ya kile unachokisema🙄🙄

#jr
 
Samahani Sana umeanza kwakusema uchumi upo vizuri Ila ndani Zaid Una Anza kusema uchumi wetu vile unaelekea pabaya. Mm nikushauri na kukwambia let us be faithfully mbele ya serikali na wakuu Sera za SASA ZA UCHUMI ZA ONE MAN SHOW ZITATULIZA NA KUTUFANYA KUSHUKA KIMAPATO NA MWISHO KURUDIA MATAPISHI TULIOJIFANYA TUNAWAPONDA AKINA MZEE KIKWETI.

UKISHA GUSA SECTA YA FEDHA NAKUIBANA KIASI HAKUNA PAKUPUMULIA BASI UNACHIMBA KABURI REFU LA UCHUMI.
YANI KWAKUWA WEWE NI SERIKALI KUPITIA TRA UNATUNGA SHERIA ZAKIKATILI ZISIZO NA HAKI YAKUSIKILIZWA MAHAKAMANI NA MAHAKAMA NDIO ITOE AMRI KUCHUKUA FEDHA AU MALI YANI KIJANA MMOJA TU TRA ANA ANDIKA AGENCY NOTICE PESA ZAKO ZINAONDOKA HII NI HATARI HAKUNA MUEKEZAJI ATAWEKEZA PESA KTK TAIFA HALINA SHERIA ZAKULINDA MTAJI WAKE.

NDIO MAANA MWANZONI KABISA MOJA YAMAFANIKIO MAKUBWA YA KIKWETE NIKULINDA MITAJI YA WAWEKEZAJI KWAKUWEKA SHERIA NGUMU KUCHUKUA PESA ZA WAWEKEZAJI KWENYE MA BANK. NYIE MKAONA WAO VILAZA 2015 MKABADILI SHERIA YA KODI KWELI? GOD HAVE A MERCY ON US.
 
Mimi binafsi nikiangalia katika hivyo vyote naona kwamba hali ya uchumi ni nzuri na kama taifa tunaelekea sehemu nzuri.Kufungwa kwa biashara, watu kupoteza au kukosa ajira na biashara kuwa ngumu ni kawaida katika uchumi wa soko ambapo kuna ushindani mkali. Kama biashara imashindwa ushindani basi huwezi kusema ni matatizo ya serikali hapana ila iwapo maamuzi ya serikali ama kisheria au kisera ndo yamefanya biashara hio kuanguka basi unaweza kulaumu serikali na ni lazima kuwa makini katika kutoa lawama hizo kwani kuna uwezkano kabisa kutoa lawana hizo kukawa na madhara zaidi ya kiuchumi.
Je, baada ya kufanya oberservation yako ina maana uliona biashara zinafungwa kutokana na ushindani?!

Majuzi tu hapa tumeona taarifa ya bosi wa Tanga Cement akielezea ugumu wa biashara... je, sababu ya ugumu huo ni ushindani?! Fine, wapo watakaosema ni ushindani kutoka Dangote Cement lakini sio tu bosi huyo hakutaja Dangote Cement kama source ya ugumu wa biashara yao bali hata Dangote mwenyewe tunaona uzalishaji umepungua sana kiasi cha kufanya bei ya saruji kupaa!!!

Hapo kwa Dangote pia wapo watakaosema demand for cement ndio chanzo cha kupaa kwa bei licha ya kwamba nimesha-highlight suala la kupungua uzalishaji! Lakini pamoja na suala la kupungua uzalishaji, pia kuna taarifa nyingine inayohusu deni la karibu TZS 6 Billion ambalo Dangote Cement wanadaiwa na NSK Oil & Gas...

Dangote waliingia mkataba na hii kampuni ili iwe supplied with fuel. Ili NSK waweze ku-finance hiyo deal, wakachukua overdraft kwa Standard Chartered Bank!

Dangote kashindwa kulipa kiasi tajwa!

Kushindwa kwa Dangote kukaifanya NSK Oild & Gas ishindwe kuilipa Standard Chartered Bank!

Standard Chartered Bank nao katika kulinda pesa za wateja wake wakalazimika kwenda mahakamani kuishitaki Kampuni ya Mafuta! Kampuni ya Mafuta nayo ikalazimika kwenda mahakaman kuomba Dangote Cement ifilisiwe!!

Huo mfano wa juu ndivyo ulivyo kwa biashara nyingi!! Nani angetarajia Dangote washindwe kulipa 5.8B hadi wanafikishwa mahakamani?! Ukweli ni kwamba, biashara ni ngumu na ugumu huo hautokani na ushindani!!!

Ushindani pekee unaoweza kuiathiri Dangote Cement ni from imported cements, na kama ndivyo bado wa kulaumiwa hapo ni serikali kwa sababu huwezi kuacha viwanda vya ndani vinakufa kutokana na ushindani wa imported products wakati imported products zenyewe badala ya kurahisisha maisha, ndo kwanza zinafanya maisha yawe magumu kwa wajenzi!!

Aidha, kuna habari imesambaa hivi majuzi... ki ukweli nilishindwa kabisa ku-comment chochote manake hadi sasa nashindwa kuamini kama nilichoona mitandaoni ni kweli! Na hii ndo comment yangu ya kwanza kuhusu hilo suala... ni about Ngurdoto Mountain Lodge!

Kama ni kweli, hivi hotel kama Ngurdoto ina feli feli vipi kibiashara kirahisi namna hiyo?! Anyway, nimesikia hapa na pale kuhusu sijui family conflicts and other blah blah!!

Je, kama Ngurdoto ingekuwa kwenye ile peak yake pangekuwepo na hizo family problems au wana-Familia walio mbali kidogo na biashara wanaliona lihoteli likuuuubwa lakini hakuna wanachopata na hivyo kuanza kushikana uchawi?!

Hata kama pangekuwa na hiyo migogoro, serikali inafanya nini kuhakikisha miradi mkakati kama huu haitumbukii shimoni kwa mambo ya kijinga?!

In short, kosa kubwa kabisa alilofanya Magu ni kujikita zaidi kwenye Uchumi wa Kodi! Hajali kuona kampuni yoyote ile inakufa katika kuhakikisha kampuni husika inatoa hadi senti yake ya mwisho na kulipa kodi!!

Wakati anafanya haya anasahau kampuni husika ikishakufa, atapoteza PAYE pamoja na salary and wages itakayozunguka kwenye uchumi na ku-stimulate sekta zingine za kiuchumi, na hivyo kuleta kodi zingine zaidi na zaidi!!!

JPM na serikali yake HAWAJALI multiplier effect ya kiuchumi, no wonder wamewekeza matrilioni kwenye ndege!! Matokeo yake, baada ya kutengeneza mipango maalumu kuhakikisha kampuni zinazodaiwa kodi zilipe kwa awamu ili kuhakikisha zinaendelea kufanya biashara na hatimae ku-enjoy multplier effect, JPM na Serikali yake wao "kodi yetu kwanza", ukifa, it's up to you!!!

Unaachaje hotel yenye vyumba 300 na 7 Presidential Suites inageuka kuwa hostel ya wanafunzi (kama kweli)?! Serikali ya JPM kama ingekuwa inajali kama inavyotaka ionekane, ingeweza hata kununua kiasi cha shares za Ngurdoto na kufanya management contract kuhakikisha hotel inaendelea kufanya kazi huku ikiendelea kukusanya kodi zake!!

Kama nchi za wazetu, hususani US huwa wanafanya sana bailout kwa kampuni zao kwa vigezo walivyoweka wao, hata JPM angeweza kufanya bailout kwa kampuni zinazoelekea kuangamia hata kama kuangamia huko kumetokana na wao kutolipa kodi kwa sababu nchi maskini kama hii inatakiwa kuwa na goal kubwa ya kuhakikisha biashara nyingi zaidi zinaendelea kuzaliwa na zilizopo zinaendelea kukua!
 
Ukitaka kujadili hali yetu kiuchumi kwa sasa tazama mwenendo wa "variables" zinazoainishwa katika kanuni hii:
Y = C + I + G + NE.
La sivyo ni porojo tu mkuu.

Ignorance is the hell itself,

Mtu anaacha kuzungumzia uwezo wa watu kufanya matumizi ulivyodorora kwa maana ya households Consuption capability and its mutiplier effect on their existing and prospected investment decisions,

Mtu anashindwa hata kugusia jinsi big investors plus charitable institutions zinavyokuwq treated and its own mpact on business continuity ie. Going concern,

Mtu hasemi basi jinsi ambavyo government inaspend within the government institutions badala ya kuhusisha private sector the likes of SUMA JKT & TBA construction projects wanazopewa this a very little or no private sector delegation ili ku stimulate public spending

Kwangu mimi hizo variable tatu tu zinaonyesha jinsi uchumi usivyosimamiwa with integrity aidha kuna kikundi kinataka kuhodhi uchumi na kuturejesha kwenye controlled economy au watu hawafahamu wanachofanya

Kwenye uchumi uliostaarabika huwezi kukuta excessive government intervation kama hapa, kazi ya serikali ni ku design na ku supervise economic policies siyo kufanya direct control.

Hata monita darasani huwa hakuzibi mdomo ila anaandika majina
 
Katika awamu zote, awamu hii tunalishwa matango pori sana kwenye muenendo wa hali ya uchumi nchini...




Cc: mahondaw
 
Ignorance is the hell itself,

Mtu anaacha kuzungumzia uwezo wa watu kufanya matumizi ulivyodorora kwa maana ya households Consuption capability and its mutiplier effect on their existing and prospected investment decisions,

Mtu anashindwa hata kugusia jinsi big investors plus charitable institutions zinavyokuwq treated and its own mpact on business continuity ie. Going concern,

Mtu hasemi basi jinsi ambavyo government inaspend within the government institutions badala ya kuhusisha private sector the likes of SUMA JKT & TBA construction projects wanazopewa this a very little or no private sector delegation ili ku stimulate public spending

Kwangu mimi hizo variable tatu tu zinaonyesha jinsi uchumi usivyosimamiwa with integrity aidha kuna kikundi kinataka kuhodhi uchumi na kuturejesha kwenye controlled economy au watu hawafahamu wanachofanya

Kwenye uchumi uliostaarabika huwezi kukuta excessive government intervation kama hapa, kazi ya serikali ni ku design na ku supervise economic policies siyo kufanya direct control.

Hata monita darasani huwa hakuzibi mdomo ila anaandika majina
True
 
Je, baada ya kufanya oberservation yako ina maana uliona biashara zinafungwa kutokana na ushindani?!

Majuzi tu hapa tumeona taarifa ya bosi wa Tanga Cement akielezea ugumu wa biashara... je, sababu ya ugumu huo ni ushindani?! Fine, wapo watakaosema ni ushindani kutoka Dangote Cement lakini sio tu bosi huyo hakutaja Dangote Cement kama source ya ugumu wa biashara yao bali hata Dangote mwenyewe tunaona uzalishaji umepungua sana kiasi cha kufanya bei ya saruji kupaa!!!

Hapo kwa Dangote pia wapo watakaosema demand for cement ndio chanzo cha kupaa kwa bei licha ya kwamba nimesha-highlight suala la kupungua uzalishaji! Lakini pamoja na suala la kupungua uzalishaji, pia kuna taarifa nyingine inayohusu deni la karibu TZS 6 Billion ambalo Dangote Cement wanadaiwa na NSK Oil & Gas...

Dangote waliingia mkataba na hii kampuni ili iwe supplied with fuel. Ili NSK waweze ku-finance hiyo deal, wakachukua overdraft kwa Standard Chartered Bank!

Dangote kashindwa kulipa kiasi tajwa!

Kushindwa kwa Dangote kukaifanya NSK Oild & Gas ishindwe kuilipa Standard Chartered Bank!

Standard Chartered Bank nao katika kulinda pesa za wateja wake wakalazimika kwenda mahakamani kuishitaki Kampuni ya Mafuta! Kampuni ya Mafuta nayo ikalazimika kwenda mahakaman kuomba Dangote Cement ifilisiwe!!

Huo mfano wa juu ndivyo ulivyo kwa biashara nyingi!! Nani angetarajia Dangote washindwe kulipa 5.8B hadi wanafikishwa mahakamani?! Ukweli ni kwamba, biashara ni ngumu na ugumu huo hautokani na ushindani!!!

Ushindani pekee unaoweza kuiathiri Dangote Cement ni from imported cements, na kama ndivyo bado wa kulaumiwa hapo ni serikali kwa sababu huwezi kuacha viwanda vya ndani vinakufa kutokana na ushindani wa imported products wakati imported products zenyewe badala ya kurahisisha maisha, ndo kwanza zinafanya maisha yawe magumu kwa wajenzi!!

Aidha, kuna habari imesambaa hivi majuzi... ki ukweli nilishindwa kabisa ku-comment chochote manake hadi sasa nashindwa kuamini kama nilichoona mitandaoni ni kweli! Na hii ndo comment yangu ya kwanza kuhusu hilo suala... ni about Ngurdoto Mountain Lodge!

Kama ni kweli, hivi hotel kama Ngurdoto ina feli feli vipi kibiashara kirahisi namna hiyo?! Anyway, nimesikia hapa na pale kuhusu sijui family conflicts and other blah blah!!

Je, kama Ngurdoto ingekuwa kwenye ile peak yake pangekuwepo na hizo family problems au wana-Familia walio mbali kidogo na biashara wanaliona lihoteli likuuuubwa lakini hakuna wanachopata na hivyo kuanza kushikana uchawi?!

Hata kama pangekuwa na hiyo migogoro, serikali inafanya nini kuhakikisha miradi mkakati kama huu haitumbukii shimoni kwa mambo ya kijinga?!

In short, kosa kubwa kabisa alilofanya Magu ni kujikita zaidi kwenye Uchumi wa Kodi! Hajali kuona kampuni yoyote ile inakufa katika kuhakikisha kampuni husika inatoa hadi senti yake ya mwisho na kulipa kodi!!

Wakati anafanya haya anasahau kampuni husika ikishakufa, atapoteza PAYE pamoja na salary and wages itakayozunguka kwenye uchumi na ku-stimulate sekta zingine za kiuchumi, na hivyo kuleta kodi zingine zaidi na zaidi!!!

JPM na serikali yake HAWAJALI multiplier effect ya kiuchumi, no wonder wamewekeza matrilioni kwenye ndege!! Matokeo yake, baada ya kutengeneza mipango maalumu kuhakikisha kampuni zinazodaiwa kodi zilipe kwa awamu ili kuhakikisha zinaendelea kufanya biashara na hatimae ku-enjoy multplier effect, JPM na Serikali yake wao "kodi yetu kwanza", ukifa, it's up to you!!!

Unaachaje hotel yenye vyumba 300 na 7 Presidential Suites inageuka kuwa hostel ya wanafunzi (kama kweli)?! Serikali ya JPM kama ingekuwa inajali kama inavyotaka ionekane, ingeweza hata kununua kiasi cha shares za Ngurdoto na kufanya management contract kuhakikisha hotel inaendelea kufanya kazi huku ikiendelea kukusanya kodi zake!!

Kama nchi za wazetu, hususani US huwa wanafanya sana bailout kwa kampuni zao kwa vigezo walivyoweka wao, hata JPM angeweza kufanya bailout kwa kampuni zinazoelekea kuangamia hata kama kuangamia huko kumetokana na wao kutolipa kodi kwa sababu nchi maskini kama hii inatakiwa kuwa na goal kubwa ya kuhakikisha biashara nyingi zaidi zinaendelea kuzaliwa na zilizopo zinaendelea kukua!
Nondo tupu.
 
Back
Top Bottom