Nini Kinachoendelea IMF na World Bank?

IMF na World Bank ni mapacha wa baba mmoja na huwezi wapomda IMF kuwa ni mabeberu huku ukilala kitanda kimoja na world Bank. Hizo taarifa za takwimu ni muhimu sana kwa ajili ya wawekezaji wa baadae pia na wakopeshaji.

Wakopeshaji watatumia hizo taarifa kwenye kuset riba ya mikopo ambayo Serikali inakopa ,taarifa za ukuaji wa uchumi zikiwa nzuri basi hata riba ya mikopo mipya inakua ndogo.

Pia kuna credit rating agencies kubwa tatu ambazo ni Standard and Poor (S&P), Moody's pamoja na Fitch group ambao wao wanatoa rating ya nchi kiuchumi. Mara ya mwisho (1/4/2019) Moody's wameipa Tanzania credit score ya -B1 kutokana na muonekano hasi wa ukuaji wa uchumi.

Serikali imelia sana kwamba kabla ya kupewa hiyo score na Moody's ilifaa wakae chini wazungumze nk,lakini jamaa wanatumia data sio vikao kwenye kufanya maamuzi yao. Tatizo lililopo sio mabeberu Ila changamoto za ukuaji wa uchumi ambazo zimesababishwa na uongozi dhaifu. Rating ya -B1 Tanzania haijawahi pata toka kipindi cha Nyerere kwa hiyo lazima tuna shida sehemu na tunatakiwa tujirekebishe.
Hivi mkuu huwa unakuwaga jf siku zote? Nondo kama hizi mbwa wa ccm huwa hawanusagi.
 
huwezi kujiendesha wakati hata sindano hutengenezi wala panadol,

kwa watoto wa jana hawa ndio walimtoa nyerere!! nyie endeleen kubishana nao ndio mtajua kushuka kwa thaman ya shilingi.
 
"Umasikini wa akili ni umasikini mbaya sana kuliko umasiki wowote ule" daima masikini wa kila kitu hata ukimwambia we ni masikini, atakuchukia wakati unamwambia ukweli na kuleta visingizio chungu nzima, endeleeni kujifariji mnasingiziwa
 
Unajua jamaa yangu huwa kuna mahala napata taabu sana kujadili maada kama hizi.

Unaweza kuwakwepa IMF na World bank kama toka uhuru unakopa kwao na bado wanakudai na bado unahitaji misaada yao na misaada ya wanachama wao, ukipata maafa kama mafuriko, njaa, milipuko ya magonjwa nk unahitaji misaada toka kwao. Madeni yakikuzidi unaenda kuomba wakusamehe madeni, miradi kibao ya kijamii unahitaji waje wakusaidie, bajeti yako zaidi ya 40% inatoka kwao... Hao IMF na World bank ukumbuke ni moja ya organs za UN na watoa michango mikubwa huko na hela zao ndio tunawaita wadau wetu waendeleo..

Njia pekee ya kuwakwepa IMF na World bank ni kujitegemea kwa kila kitu na kutoomba msaada kwao na kwa wanachama wao au wanaombatana nao. Tukipata Maafa yoyote tujiokoe na kujisaidia wenyewe na resources zetu, madawa either tununue kwa hela zetu au tutengeneze wenyewe.. IMF na World bank sidhani kama watakufuata fuata kama wewe unajitegemea na huwafuati fuati..
Jamaa wamesahau kuwa hata Ile interchange ya ubungo na barabara ya mwendo kazi ni kwa mkopo was world Bank.Wanaccm baada ya kupata mwenyekiti mpya mr.wahapahapa akiri zimewaruka kabisa
 
Back
Top Bottom