Hivi mkuu huwa unakuwaga jf siku zote? Nondo kama hizi mbwa wa ccm huwa hawanusagi.IMF na World Bank ni mapacha wa baba mmoja na huwezi wapomda IMF kuwa ni mabeberu huku ukilala kitanda kimoja na world Bank. Hizo taarifa za takwimu ni muhimu sana kwa ajili ya wawekezaji wa baadae pia na wakopeshaji.
Wakopeshaji watatumia hizo taarifa kwenye kuset riba ya mikopo ambayo Serikali inakopa ,taarifa za ukuaji wa uchumi zikiwa nzuri basi hata riba ya mikopo mipya inakua ndogo.
Pia kuna credit rating agencies kubwa tatu ambazo ni Standard and Poor (S&P), Moody's pamoja na Fitch group ambao wao wanatoa rating ya nchi kiuchumi. Mara ya mwisho (1/4/2019) Moody's wameipa Tanzania credit score ya -B1 kutokana na muonekano hasi wa ukuaji wa uchumi.
Serikali imelia sana kwamba kabla ya kupewa hiyo score na Moody's ilifaa wakae chini wazungumze nk,lakini jamaa wanatumia data sio vikao kwenye kufanya maamuzi yao. Tatizo lililopo sio mabeberu Ila changamoto za ukuaji wa uchumi ambazo zimesababishwa na uongozi dhaifu. Rating ya -B1 Tanzania haijawahi pata toka kipindi cha Nyerere kwa hiyo lazima tuna shida sehemu na tunatakiwa tujirekebishe.