Kama binadamu yeyote, Mwigulu hajakamilika bado,hivyo basi anahitaji msaada utokao kwa Mungu. Mungu hutumia njia hii ya maombi kutujibu mahitaji yetu. Tazama,kila mtu ana haja yake ndani ya moyo wake. Ikiwa ni hivyo,kwamba maombi ni njia ya mahitaji yetu,basi tusipoomba hatuwezi kupokea.
Labda tuangalie mfano mdogo wa kawaida kabisa;
Chukulia una watoto watatu nyumbani mwako,alafu mtoto wako mmoja akawa na uhitaji wa kununuliwa daftari la mazoezi la hesabati. Kisha;mtoto huyo akawa kimya akisubiri umnunulie pasipo yeye kukuomba anachokihitaji kutoka kwako. Swali,je utamnunulia hilo daftari pasipo kukuomba? Utajuaje kama daftari lake limeisha na anahitaji daftari jingine? Ukweli ni kwamba,hutaweza kumnunulia kwa sababu hajakuomba,na inawezekana usijue kama limeisha.
Isaya 1:18