Nini kimeisibu Wizara ya Fedha? Malipo ya Dowans? Maadhimisho ya miaka 50 au ndio mdororo wa uchumi?

PEA

Member
Dec 31, 2010
77
33
Kinachofanywa na Hazina iliyopo chini ya Wizara ya Fedha kinatisha! Kuanzia mwezi uliopita imejitokeza tabia ya kuwaondoa watu kwenye orodha ya Malipo (Payroll) kwa Makusudi au bahati mbaya haijulikani. Wao wanasema mfumo wa computer unasumbua. Mwezi huu hali imekuwa mbaya zaidi. Kuna taarifa kuwa watu wengi wamekosakana kwenye orodha ya malipo yaani payroll kwa kisingizio hicho hicho. Taarifa kutoka huko Mbeya zinasema Wafanyakazi waliopokea mishahara yao wengine wamekuta kuna upungufu wa kati ya shilingi 30 elfu hadi laki moja na nusu bila taarifa yoyote.
Aidha hata payroll zenyewe inasemekana zimevurugwa vurugwa kiasi kwamba katika halmsahuri unakuta Mwalimu ambye kimsingi anastahili kuwa kwenye payroll ya idara ya Elimu anaonekana kwenye payroll ya Utawala. Majina mengine pia hayamo yakihisiwa kuwekwa kwenye halmshauri zingine (Vote na sub vote tofauti) na wengine kuwa kwenye idara zingine za sekalini.

Kana kwamba haitoshi, jioni hii nilikuwa naangalia kipindi maalum Star Tv kuhusu changamoto za Ualimu Mtazamaji kutoka Dodoma amezungumzia tatizo la makosa kwenye payroll yaliyojitokeza kwa mwezi huu na uliopita ikifanana na kile kilichotokea sehemu nyinginezo.

Je, ni dalili za kuchoka kwa serikali? Je, makato haya yatarudishwa vipi wakati inadaiwa kukitokea tatizo kama hili salary slip hazipelekwi kwa wahusika ili waweze kujua sababu za makato?


Sijuiiiiiiiiiiiiii!
 
serikali ya kishikaji, hawana pesa ya kutosha kuwalipa watu wote wanajaribu kuvuruga ili wasingizie tatizo la computer. Mwaka huu watanyosha tu maelezo maana kila wanapodanganya baadaye mambo ndo yanazidi kuwa maBaya zaidi.
 
Kinachofanywa na Hazina iliyopo chini ya Wizara ya Fedha kinatisha! Kuanzia mwezi uliopita imejitokeza tabia ya kuwaondoa watu kwenye orodha ya Malipo (Payroll) kwa Makusudi au bahati mbaya haijulikani. Wao wanasema mfumo wa computer unasumbua. Mwezi huu hali imekuwa mbaya zaidi. Kuna taarifa kuwa watu wengi wamekosakana kwenye orodha ya malipo yaani payroll kwa kisingizio hicho hicho. Taarifa kutoka huko Mbeya zinasema Wafanyakazi waliopokea mishahara yao wengine wamekuta kuna upungufu wa kati ya shilingi 30 elfu hadi laki moja na nusu bila taarifa yoyote.
Aidha hata payroll zenyewe inasemekana zimevurugwa vurugwa kiasi kwamba katika halmsahuri unakuta Mwalimu ambye kimsingi anastahili kuwa kwenye payroll ya idara ya Elimu anaonekana kwenye payroll ya Utawala. Majina mengine pia hayamo yakihisiwa kuwekwa kwenye halmshauri zingine (Vote na sub vote tofauti) na wengine kuwa kwenye idara zingine za sekalini.

Kana kwamba haitoshi, jioni hii nilikuwa naangalia kipindi maalum Star Tv kuhusu changamoto za Ualimu Mtazamaji kutoka Dodoma amezungumzia tatizo la makosa kwenye payroll yaliyojitokeza kwa mwezi huu na uliopita ikifanana na kile kilichotokea sehemu nyinginezo.

Je, ni dalili za kuchoka kwa serikali? Je, makato haya yatarudishwa vipi wakati inadaiwa kukitokea tatizo kama hili salary slip hazipelekwi kwa wahusika ili waweze kujua sababu za makato?


Sijuiiiiiiiiiiiiii!

GARBAGE IN GARBAGE OUT (GIGO) !

ujue hiyo!wizara ina walakini.

 
Sasa hizo pesa za maandalizi ambazo siyo chini mil 160 zinatumika ktk maazimisho na kweli kuna umuhimu iwapo sherehe ilifanyika musoma ya miaka 50 ya mchonga inatosha. Hizo pesa tumie kulipa madeni ya wazee wa east africa na waalimu period.

N kuacha ku victimize staff wazuri na kuwapeleka ITA dogo dr y kayandabila, dogo world bank, imf au un utapata kazi.
 
Ilo nalo tatizo kubwa saana kwani siye Halmashauri yetu akuna kitu til dis tym! Mmmm thats Tz we need!
 
mke wangu yupo bongo ni mtumishi wa idara ya serikali hadi leo hajapokea salary na mwezi uliopita salary yake ilitoka tarehe 36,
 
serikali iliyolaaniwa huishi kilaana laana tu from top to the bottom
 
Back
Top Bottom