PEA
Member
- Dec 31, 2010
- 77
- 33
Kinachofanywa na Hazina iliyopo chini ya Wizara ya Fedha kinatisha! Kuanzia mwezi uliopita imejitokeza tabia ya kuwaondoa watu kwenye orodha ya Malipo (Payroll) kwa Makusudi au bahati mbaya haijulikani. Wao wanasema mfumo wa computer unasumbua. Mwezi huu hali imekuwa mbaya zaidi. Kuna taarifa kuwa watu wengi wamekosakana kwenye orodha ya malipo yaani payroll kwa kisingizio hicho hicho. Taarifa kutoka huko Mbeya zinasema Wafanyakazi waliopokea mishahara yao wengine wamekuta kuna upungufu wa kati ya shilingi 30 elfu hadi laki moja na nusu bila taarifa yoyote.
Aidha hata payroll zenyewe inasemekana zimevurugwa vurugwa kiasi kwamba katika halmsahuri unakuta Mwalimu ambye kimsingi anastahili kuwa kwenye payroll ya idara ya Elimu anaonekana kwenye payroll ya Utawala. Majina mengine pia hayamo yakihisiwa kuwekwa kwenye halmshauri zingine (Vote na sub vote tofauti) na wengine kuwa kwenye idara zingine za sekalini.
Kana kwamba haitoshi, jioni hii nilikuwa naangalia kipindi maalum Star Tv kuhusu changamoto za Ualimu Mtazamaji kutoka Dodoma amezungumzia tatizo la makosa kwenye payroll yaliyojitokeza kwa mwezi huu na uliopita ikifanana na kile kilichotokea sehemu nyinginezo.
Je, ni dalili za kuchoka kwa serikali? Je, makato haya yatarudishwa vipi wakati inadaiwa kukitokea tatizo kama hili salary slip hazipelekwi kwa wahusika ili waweze kujua sababu za makato?
Sijuiiiiiiiiiiiiii!
Aidha hata payroll zenyewe inasemekana zimevurugwa vurugwa kiasi kwamba katika halmsahuri unakuta Mwalimu ambye kimsingi anastahili kuwa kwenye payroll ya idara ya Elimu anaonekana kwenye payroll ya Utawala. Majina mengine pia hayamo yakihisiwa kuwekwa kwenye halmshauri zingine (Vote na sub vote tofauti) na wengine kuwa kwenye idara zingine za sekalini.
Kana kwamba haitoshi, jioni hii nilikuwa naangalia kipindi maalum Star Tv kuhusu changamoto za Ualimu Mtazamaji kutoka Dodoma amezungumzia tatizo la makosa kwenye payroll yaliyojitokeza kwa mwezi huu na uliopita ikifanana na kile kilichotokea sehemu nyinginezo.
Je, ni dalili za kuchoka kwa serikali? Je, makato haya yatarudishwa vipi wakati inadaiwa kukitokea tatizo kama hili salary slip hazipelekwi kwa wahusika ili waweze kujua sababu za makato?
Sijuiiiiiiiiiiiiii!