Nini kifanyike kupunguza ajali za barabarani?

Nini kifanyike kupunguza ajali za barabarani?

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Wakuu

=====

Ajali zimekuwa nyingi Kila siku tunaamka na ajali tunakwama wapy?


Je, ajali za barabarani nchini Tanzania zinaendelea kutokea kwa sababu hatujui nini cha kufanya, au kwa sababu tunachukulia usalama barabarani kama jambo la kawaida?
1753682811703.png


Kwa nini madereva wanaorudia makosa hatari kama mwendokasi na ulevi barabarani wanaendelea kuruhusiwa kuendesha? Miundombinu yetu iko salama kweli kwa watumiaji wote – akiwemo mtembea kwa miguu na waendesha bodaboda? Je, elimu ya usalama barabarani inawafikia walio wengi, au tunazungumza zaidi kuliko kuchukua hatua? Na sisi kama raia, tunafanya sehemu yetu kutoa taarifa au kukemea pale tunapoona hatari? Kama kweli tunathamini maisha, ni wakati wa kila mmoja wetu kuwajibika.
 
Ajali nyingi husababishwa na mwendokasi ila raia pia hawajui matumizi sahihi ya barabara

Barabarani itawekwa alama ya wapita kwa miguu ila Raia hawakatizi hapo au zitakuwepo walkways lkn bado utakuta mtu anafanya jogging barabara kuu
 
Wakuu

=====

Ajali zimekuwa nyingi Kila siku tunaamka na ajali tunakwama wapy?
Kama dereva amebainika ana kosa, anyang'anywe leseni, afungwe si chini ya miaka 5 kisha kunyongwa kama aliua. Hii ndiyo adhabu pekee itakayomaliza hili janga.
 
Sababu ni nyingi inategemea kama ni za kimazingira, kibinadamu au kimekanika.

-Mazingira, serikali iboreshe miundombinu na ione namna ya kurekebisha zile sehemu ukorofi.

-Kibinadamu, dereva na askari wa usalama barabarani, hapa kuna uzembe, rushwa, ulevi.

-Makanika, magari mabovu. Serikali iondoe au ipunguze kodi kwenye magari mapya na iongeze kwenye magari yaliyotumika ili watu sasa wanunue mapya na waweze kutumia kwa muda mrefu, tofauti na sasa mtu ananunua gari kwa 65m used afanyie biashara hadi ije hela yake irudi na faida juu ni miaka mingi wakati huo uchakavu wa gari umeongezeka ila ikiwa mpya atleast bado itakuwa katika kwenye ubora hata baada ya matumizi ya muda mrefu kidogo. Vilevile ukaguzi wa mara kwa mara wa hivi vyombo japo suala la rushwa ni kubwa na wenye mamlaka walisha liruhusu.
 
Wakuu

=====

Ajali zimekuwa nyingi Kila siku tunaamka na ajali tunakwama wapy?
Nimewahi kuandika hapa JF namna ya kuondoa kabisa si kupunguza,kuondoa kabisa ajali za barabarani,lakini kwakuwa hapa huwa tunaandika tu kujifurahisha huwa hayachukuliwi na kufanyiwa kazi !

1.KUTOKUWA NA NJIA RASMI YA WAENDA KWA MIGUU


Hili ni tatizo kubwa mno ambalo serikali inayooongozwa na mazumbukuku hawaoni,ni kama nchi inajiendea tu pasipo Kuwa na uongozi wa watu wenye akili timamu !

Njia au barabara nyingi hapa nchini hazina sehemu za waenda Kwa miguu,hivyo waenda Kwa miguu hulazimika kutumia njia za vyombo vya moto humo humo !,Angalia Miji mikubwa yote mikubwa (Dar,Mwanza,Mbeya na Arusha) yaani ni vituko !

Mfano mzuri ,angalia hiyo barabara ya kutoka hapo Kimara hadi Kibaha,imejengwa kana kwamba watu wote Wana magari,hakuna njia pembezoni mwa hiyo barabara ya watembea Kwa miguu,Endapo mtu akitaka Kutembea kutoka Kimara hadi temboni itamlazimu kupita pembeni !,yaani ni vituko !

Mind u,watu wanaogongwa humu ni wengi mno,vile hawatangazwi sehemu yeyote !


2.UFINYU WA BARABARA


Hili ni tatizo kubwa mno ambalo linafichwa Kwa kichaka Cha madereva kutokufuata alama za Barabarani !,ndiyo maana nasema hii nchi inaongozwa na mazumbukuku !

Mara nyingi nchi hii ajali nyingi mara zote hutokea Morogoro na Mbeya,hiyo mikoa ndiyo kitovu Cha ajali hapa Tanzania,ingawaje mikoa mingine pia ajali hutokea lakini si nyingi kama zinazotokea hiyo mikoa miwili !

Sababu kubwa ni malori,unakuta Lori likifeli inakuwa tatizo !

Tungekuwa na serikali inayooongozwa na Viongozi wenye akili timamu,tungekuwa na barabara ya njia nane kuanzia Dar hadi Tunduma,halafu malori yangekuwa na njia yake spesho yasiingiliane na magari madogo na magari ya abiria,hiyo njia inaingiza mapato makubwa mno serikalini lakini hadi Leo barabara zimebaki za muundo wa kikoloni,Ile service road levy inayokusanywa kwenye mafuta nadhani hii ndiyo ingekuwa kazi yake,lakini badala yake inachukuliwa Tsh 1 Bilioni wanaenda kupewa Taifa Stars !,Kwa maana hiyo viongozi Vichwa maji tulionao hawaoni kama Kuna umuhimu wa upanuzi wa barabara!


3.UWEPO WA SHERIA MBOVU KUHUSU BIMA

Ni mara ngapi umeona au kusikia,watu waliokufa au waliopata ulemavu wamepewa malipo ya kujikimu kwasababu ya ajali iliyosababishwa na ubovu wa gari au uzembe wa dereva?

Yaani hii nchi ya Kijinga,ajali ikitokea ambayo unakuta imeua makumi ya watu,atakayekuwa na umuhimu serikalini ni dereva aliyesababisha ajali na kukimbia,lakini waliokufa watanunuliwa majeneza na serikali yako na Kwa mbwembwe wataitisha vyombo vya habari kumulika namna serikali inavyojali "MAITI" kuliko walio hai !,Mtu aliyebaki na ulemavu Kwa ajali hiyo itakula kwake na ulemavu uliosababishwa Kwa Ubovu wa gari au uzembe wa dereva hauna fidia yeyote !

Serikali yako inayooongozwa na mazumbukuku yenyewe inaangalia masilahi yake kupitia Kodi ya Bima ila haingalii Mwananchi wake atakapopata ajali itakuwaje !

Utakaponunua chombo Cha moto Huwezi endesha bila Bima,bima mara nyingi huwa zinamlinda mwenyewe chombo tu ila mwananchi aliyegongwa na aliyevunjika na kufa kwasababu ya ajali huwa ni kama haisemi chochote,na hata kama inasema chochote Haina nguvu Kwa muhanga na process huwa Zina uzumbukuku wa kiwango Cha juu !,ndiyo maana wamiliki na madereva wao wanakuwa na nyodo barabarani!

Angalia nchi zilizoendelea uone namna Bima zilivyo na nguvu Kwa muhanga wa ajali,yaani dereva atakuwa makini kiasi kwamba ataogopa hata kugonga nzi !

Hao watoto wa shule waliogongwa hapo Mbeya,wamezikwa tayari !,mtu yeyote atakayeniletea ushahidi ya kwamba familia zao zimelipwa Kwa Sheria yetu ya Bima,basi huyo mtu binafsi nitampatia laki 5 !

Hakuna kitakachofanyika, Business as usual !,Pata ajali serikali ya kizumbukuku ikuzike Kwa mbwembwe maisha yanaendelea,huku msababisha ajali yeye anaenda kulipwa na makampuni ya Bima na kupewa chombo kipyaaaaaaaaaaa!


4.RUN AWAY TRUCK RAMP

Hizi huwa ni barabara ambazo huwekwa pembezoni mwa barabara ambazo mara nyingi huwa Zina mitelemko mikali Ili kuepusha ajali kwenye magari ambayo yanafeli breki !

Tungekuwa na serikali ambayo inaongozwa na watu wenye akili timamu,kila barabara mpya zote zinapojengwa,maneno yote ambayo inasemekana ni hatarishi,yangekuwa yanajengwa hizi barabara,Kwa mfano pale Iwambi,Mbeya,Kila mwaka inaua watu,lakini kwasababu tuna viongozi wenye Vichwa vigumu kama vya Kamongo,Wala hata hawajali !



maxresdefault.jpg


5.SHERIA ISIMSHUGHULIKIE DEREVA PEKE YAKE,HADI MMILIKI WA CHOMBO ASHUGHILIKIWE


Wamiliki wote wa vyombo vya moto huwa hawaguswi pale ambapo dereva anafanya uzembe na kusababisha ajali !

Tungekuwa na serikali yenye watu wenye akili timamu,ilipaswa itunge Sheria ya kwamba,dereva atakayesababisha ajali atafutia leseni yake,sawa,na baada ya hapo atafikishwa mahakamani,sawa !

Lakini Chombo Cha mmiliki kilichosababisha ajali kitatozwa faini,kama hicho chombo kimesababisha vifo (kuanzia mtu mmoja na kuendelea ) adhabu yake ni kuanzia faini ya Milioni 100 hadi 500 (na hizi faini zitapelekwa moja Kwa moja Kwa familia za wahanga) hii ni nje ya fidia ya Bima,na baada ya hapo miili ya watu waliokufa itagharamikiwa na tajiri anayemiliki chombo husika !

Hii ni Kwa Ma-bus peke yake,huko kwenye magari binafsi,Bajaji na Bodaboda pia Sheria itatamka !


Haya yakifanyika Kwa uaminifu,nakwambia ajali siyo kupungua,zitaisha kabisa
 
Aina gani za ajali barabarani zilizozidi? tuanzie hapo.
 
Mleta hoja weka takwimu watu wachambue sio kutuwekea kabodaboda kamoja tuu ndio ajali zimezidi. Tafuta taarifa MOI na mahospitalini kwingineko na Polisi ili ulete hoja kamili japo unahoja muhimu sana
 
Wakati wa Magufuli ajali zilipungua Kwa asilimia 90% wajifunze yeye aliwezaje
 
Viongozi wenye majukumu haya ndio wazembe, wapo wanakula mishahara tu na kuongezewa nyota tu na vyeo.

Hakuna wa kuwalaumu bali wao tu.

Mbona Magu aliwafanya wanyooke kwa kuwaambia hataki kusikia polisi ananyang’anywa bunduki?
Na akatoa amri majambazi walazwe?

Leo Rais akiamua anaweza kupunguza ajali kwa % kubwa sana.

Wizara ni lazima ipambane na kuhakikisha madereva wanajua sheria za barabarani ipasavyo
Hakuna kutoa leseni mpaka mtu amepasi theory na practical kwa pamoja,

Bei za leseni lazima ziwe juu sana ili kupunguza madereva uchwara

Kama alieleta uzi kuwa anataka ajifunze siku moja na jumatatu aingie kariakoo.

Huo sio utani wapo wengi wa hivyo na wanasababisha watu wengine kufa kwa upumbavu wao.

Msako wa kuuliza license uwepo kila wakati ( mbona watu wanalipa kuwepo barabarani?)

Hela sio issue kwa serikali lazima barabara zote ziwe na alama za kutosha nchi nzima

Hata kwenye kona lazima kuwe na alama
Wanapokosea ni kutokujali uwepo wa alama za kutosha

Hata kama zilikuwepo na zimevunjwa ni wajibu wao kurudishia kila leo, kwani ndio kazi ya wanaosimamia barabara wawe wa taasisi yeyote ile

Ajali mnaweza kuzipunguza sana kama Rushwa itapingwa vikali

Unakuta Lorry matairi yameisha kabisa mpaka unaona zile waya zipo nje
Halafu anatoa 5,000 anaambiwa nenda
Halafu akiuwa watu, utasikia gari lilikosa breki likapata ajali

Hii ndio kauli yao kwenye ajali nyingi

Na nyie wenye magari makubwa kama hamuwezi kuhudumia magari yenu basi mbadili biashara
 
Sheria zifuatwe na tuache kubebana kisa siasa

Leo hii unakutana na boda imebeba abiria wanne boda anayumba tu barabaran iv kwel unaruhusuje boda ibebe abiria wanne.

Leo hii unakutana na bodaboda imebeba mbao za kenchi, ubao wenyewe tu ni mrefu nusu ya barabara afu boda kaubeba tena kibaya zaidi kabeba mbao zaid ya 5

Wamiliki wa mabasi wanaendesha mabasi yao hovyo sabu wanajua kuna kiongozi wa serikal nyuma yao ata wakisababisha ajari hawato wajibika ipasavyo

Lakin pia nlikua naombe serikal ibadirishe sheria zake leo hii ukipata ajari kwenye basi uwe na uwezo wa kufungua kesi na kuwashitaki wamiliki wa mabus

Km sheria ikiwepo na hawa watu wakifunguriwa kesi wakaripa mabilioni ya pesa heshima itakuepo

Lakin yote kwa yote ni sheria za barabarani ziongezwe makari na km zina makari basi zifuatwe na tuache kubebana kisa tunajuana
 
Wakuu

=====

Ajali zimekuwa nyingi Kila siku tunaamka na ajali tunakwama wapy?


Je, ajali za barabarani nchini Tanzania zinaendelea kutokea kwa sababu hatujui nini cha kufanya, au kwa sababu tunachukulia usalama barabarani kama jambo la kawaida?
View attachment 3421320

Kwa nini madereva wanaorudia makosa hatari kama mwendokasi na ulevi barabarani wanaendelea kuruhusiwa kuendesha? Miundombinu yetu iko salama kweli kwa watumiaji wote – akiwemo mtembea kwa miguu na waendesha bodaboda? Je, elimu ya usalama barabarani inawafikia walio wengi, au tunazungumza zaidi kuliko kuchukua hatua? Na sisi kama raia, tunafanya sehemu yetu kutoa taarifa au kukemea pale tunapoona hatari? Kama kweli tunathamini maisha, ni wakati wa kila mmoja wetu kuwajibika.
SMART-GIN zipigwe marufuku!!!
 
Back
Top Bottom