Nini kifanyike kuinusuru bei ya Kahawa mkoani Kagera?

Tutor B

JF-Expert Member
Jun 11, 2011
9,025
6,554
Naamini hamjambo waungwana

Mkoa wa kagera unategemea zao la kahawa kibiashara. Inashangaza kuona zao hilo linashuka bei wakati nchi jirani - Uganda bei iko juu. Mkoa una wawakilishi wa wananchi ambao wamekaa kimya wakati wapiga kura wao wananyanyasika kwa kuuza kilo moja ya kahawa kwa Tshs. 1,000/=

Kama ni mwana-Kagera na kama unaguswa na hii hali - tafadhali jitokeze ili tuweze kunusuru uchumi wa mkoa wetu - nashukuru Mkuu wa nchi ameishaliona hilo.

Nini kifanyike kunusuru bei ya zao la kahawa?

Nionavyo mimi: Badala ya kuuza kahawa kama ilivyo .. tuiongezee ubora kwa kuisindika huko huko ili tuuze kahawa inayoenda kutumika.

Kila kata iwe na kinu chake kwa ajili ya kukoboa kahawa ili yale maganda yaendelee kubaki kwenye kata husika na kuboresha ardhi (mbolea)

Nawasilisha!
 
Haya yote hayana maana kama kahawa inaruhusiwi kuvuna border. Watu wanaopeleka Uganda wanapata fedha nyingi.

Syndicate ya wanunua kahawa inashawishi zuio la kuuza nje ili iwanyonye wakulima
 
Naamini hamjambo waungwana ...
Mkoa wa kagera unategemea zao la kahawa kibiashara. Inashangaza kuona zao hilo linashuka bei wakati nchi jirani - Uganda bei iko juu. Mkoa una wawakilishi wa wananchi ambao wamekaa kimya wakati wapiga kura wao wananyanyasika kwa kuuza kilo moja ya kahawa kwa Tshs. 1,000/=
Kama ni mwana-Kagera na kama unaguswa na hii hali - tafadhali jitokeze ili tuweze kunusuru uchumi wa mkoa wetu - nashukuru Mkuu wa nchi ameishaliona hilo.

Nini kifanyike kunusuru bei ya zao la kahawa?

Nionavyo mimi: Badala ya kuuza kahawa kama ilivyo .. tuiongezee ubora kwa kuisindika huko huko ili tuuze kahawa inayoenda kutumika.

Kila kata iwe na kinu chake kwa ajili ya kukoboa kahawa ili yale maganda yaendelee kubaki kwenye kata husika na kuboresha ardhi (mbolea)

Nawasilisha!
mda mwingine watu mnakurupuka tu kushout for nothing,unasema kila kata iwe na kinu kwa ajili ya kukoboa,sjui kama unakaa kager a wewe,unaelewa nini kuhusu KCU? umeshuhudia lini kahawa inasafirishwa isiyokobolewa?
 
mda mwingine watu mnakurupuka tu kushout for nothing,unasema kila kata iwe na kinu kwa ajili ya kukoboa,sjui kama unakaa kager a wewe,unaelewa nini kuhusu KCU? umeshuhudia lini kahawa inasafirishwa isiyokobolewa?
Mimi ni mwana-Kagera, nimezaliwa Kagera, nimekulia Kagera - Primary nimesomea kijijini, Sekondary nimesomea Kahororo Secondary ... kwa hiyo maisha yangu asilimia kubwa nimekuwa mtu wa Kagera.

Nashanga povu la kunisema kuwa nimekurupuka limetoka wapi? Uliona wapi pumba za kahawa zinamrudia mkulima ili aendelee kuboresha ardhi ya shamba lake.

KCU kama unaielewa vizuri tujuze!
 
Hivi waganda huuza wapi kahawa zao?
Soko la dunia ni moja ... iweje ya Kagera iuzwe 1000 ya mganda iuzwe 5000/=? Hayo ndo maswali ya kujiuliza ili kutafutiwa majibu. Alafu mtu from no where anakuja kuitetea KCU;
 
Mimi ni mwana-Kagera, nimezaliwa Kagera, nimekulia Kagera - Primary nimesomea kijijini, Sekondary nimesomea Kahororo Secondary ... kwa hiyo maisha yangu asilimia kubwa nimekuwa mtu wa Kagera.

Nashanga povu la kunisema kuwa nimekurupuka limetoka wapi? Uliona wapi pumba za kahawa zinamrudia mkulima ili aendelee kuboresha ardhi ya shamba lake.
Basi kama umekulia kagera na hujui kama kahawa inakobolewa na wakulima wamepewa uhuru wakuchukua pumba itakuwa ni tatizo lako binafisi,tena umesomea ukanda wa green belt nako hko wanalima kahawa (kahororo) kuna mitaa kama kyaya,rwazi,makongo,bushwa KAWAULIZE WAKULIMA WA MITAA HIYO WATAKUAMBIA
 
karibia wengi wenu mnakurupuka kwenye suala la kahawa,mazira yanayowakuta watu wa kagera yanawakuta wakulima wa kahawa tz nzima,serikali ilikurupuka kuja na mpango wa kuzuia makampuni binafsi kununua na kuchakata kahawa mbivu na kuelekeza vyama vya ushirika kufanya kazi ya kukusanya na kupeleleka mnadani,lakini pm hakuangalia mazingira ya kilimo cha kahawa yalivyo na hayafanani na korosho,pili maeneo mengi hakuna vyama vya ushirika,vilivyopo hali ni mbaya.
havina uwezo hata wa kukusanya tani moja kwa sababu ya mtaji na nyenzo.hali ni mbaya mno mkoan songwe n.k
 
Naamini hamjambo waungwana

Mkoa wa kagera unategemea zao la kahawa kibiashara. Inashangaza kuona zao hilo linashuka bei wakati nchi jirani - Uganda bei iko juu. Mkoa una wawakilishi wa wananchi ambao wamekaa kimya wakati wapiga kura wao wananyanyasika kwa kuuza kilo moja ya kahawa kwa Tshs. 1,000/=

Kama ni mwana-Kagera na kama unaguswa na hii hali - tafadhali jitokeze ili tuweze kunusuru uchumi wa mkoa wetu - nashukuru Mkuu wa nchi ameishaliona hilo.

Nini kifanyike kunusuru bei ya zao la kahawa?

Nionavyo mimi: Badala ya kuuza kahawa kama ilivyo .. tuiongezee ubora kwa kuisindika huko huko ili tuuze kahawa inayoenda kutumika.

Kila kata iwe na kinu chake kwa ajili ya kukoboa kahawa ili yale maganda yaendelee kubaki kwenye kata husika na kuboresha ardhi (mbolea)

Nawasilisha!
Kata nyingi za Kagera hususani W Bukoba kuna Mashine za kukoboa kahawa
Na Kata nyingi zinauza kahawa iliyo koborewa kwa KCU
Mimi nafikiri kuna matatizo mengi ikiwemo
1.K.C.U Kucheleweshewa fedha za malipo kwa wakulima kwenye vyama vya msingi(AMCOS)
2. kuna uzalishaji Mdogo kwa sababu wakulima hawafuati kanuni za Kilimo kama vile kutotumia mbolea , madawa hivyo kupelekea ubora hafifu wa kahawa na hufanya vyama na KCU kutumia hella hella inayopatikana kwa ajiri ya kujiendesha? Hivyo kupelekea wakulima kukatwa tozo nyingi na kuwapunguzia being nzuri
3. KCU kutofanya majukumu yao kwa ufanisi kama vile kutafuta soko zuri la kahawa ya kagera etc
 
Kwa mfano mahitaji ni tani 2 wewe ukizalisha tani 4 ukiuza kwa bei ndogo utailaumu serikali? Je ukilima kahawa zenye ubora mdogo ukauza bei ndogo utailaumu serikali.Nadhani tuache kujifananisha na Uganda maana wametuzidi sana japokuwa thamani ya hela yao ni ndogo kuliko yetu,
 
Tatizo Ni Maagizo Ya PM kuzuia sekta binafsi kununua kahawa moja kwa moja kwa mkulima na kuagza vyama vya ushirika ndivyo vinunue.
 
Naamini hamjambo waungwana

Mkoa wa kagera unategemea zao la kahawa kibiashara. Inashangaza kuona zao hilo linashuka bei wakati nchi jirani - Uganda bei iko juu. Mkoa una wawakilishi wa wananchi ambao wamekaa kimya wakati wapiga kura wao wananyanyasika kwa kuuza kilo moja ya kahawa kwa Tshs. 1,000/=

Kama ni mwana-Kagera na kama unaguswa na hii hali - tafadhali jitokeze ili tuweze kunusuru uchumi wa mkoa wetu - nashukuru Mkuu wa nchi ameishaliona hilo.

Nini kifanyike kunusuru bei ya zao la kahawa?

Nionavyo mimi: Badala ya kuuza kahawa kama ilivyo .. tuiongezee ubora kwa kuisindika huko huko ili tuuze kahawa inayoenda kutumika.

Kila kata iwe na kinu chake kwa ajili ya kukoboa kahawa ili yale maganda yaendelee kubaki kwenye kata husika na kuboresha ardhi (mbolea)

Nawasilisha!
Kahawa inavushwa boda inaenda Uganda,wao waganda wanaiuza wapi mpaka wanapata bei nzuri?kwa nini na sisi tusipereke huko kuuza?
Tatizo hapa kwetu,kuna majizi mengi,unakuta bei kwenye soko la dunia ni nzuri tu,tatizo kuna makato mengi kwenye kila kilo ya kahawa,mpaka imfikie mkulima,anaambulia buku tu,
Tangu nasoma kipindi hicho miaka ya 1995,tatizo lilikuwepo,unaenda kuuza kwenye vyama vya ushirika(society),unaacha mzigo,unaondoka na maneno tu,pesa mpaka msimu ujao,ni utaperi mtupu,
Mimi siamini kama hili linafanyika kwa bahati mbaya,huu ni wizi wa kitaasisi unaoratibiwa na serikali,ili kudumaza maendeleo ya Kagera,na kunufaisha wachache,kuna conspiracy kubwa sana,hii kitu,ni kama ile iliyochangia kuuwa kiwanda cha General Tyre kule Arusha,
Lazima kuna foreign agents wanahusika hapa,
 
Soko la dunia ni moja ... iweje ya Kagera iuzwe 1000 ya mganda iuzwe 5000/=? Hayo ndo maswali ya kujiuliza ili kutafutiwa majibu. Alafu mtu from no where anakuja kuitetea KCU;
KCU ni majizi tu,tangu 1995,nikiwa chalii mdogo tu,natumwa kwenda kupereka kahawa "society", unafika,unapima,unaambiwa ni kilo kadhaa,unaandikiwa kwenye kikaratasi,hela unambiwa,subiri mpaka msimu hujao,bibi wa kijijini anatunzaje hicho kikaratasi mpaka msimu hujao?
Wakati ukizifusha boda,unapata pesa yako chapu chapu,maisha yanakwenda,wabunge wetu wametuangusha sana,inaelekea na wao wananufahika na mfumo huu nyonyaji,
 
KCU ni majizi tu,tangu 1995,nikiwa chalii mdogo tu,natumwa kwenda kupereka kahawa "society", unafika,unapima,unaambiwa ni kilo kadhaa,unaandikiwa kwenye kikaratasi,hela unambiwa,subiri mpaka msimu hujao,bibi wa kijijini anatunzaje hicho kikaratasi mpaka msimu hujao?
Wakati ukizifusha boda,unapata pesa yako chapu chapu,maisha yanakwenda,wabunge wetu wametuangusha sana,inaelekea na wao wananufahika na mfumo huu nyonyaji,
Juan uko sawa kabisa ..
Nini kifanyike:
a) Tuanze kampeini ya kung'oa mibuni yote ili huyo mnyonyaji akose kabisa?
b) Tutafute masomo kwa ajili ya Kahawa ya Kagera kama alivyofanya mtu fulani aliyetafuta soko la Kahawa ya Moshi?
Nionavyo mimi ... ndani ya jamii ya wana-Kagera wapo wasaliti ambao wananufaika na mfumo-nyonyaji wa KCU.
 
Kahawa inavushwa boda inaenda Uganda,wao waganda wanaiuza wapi mpaka wanapata bei nzuri?kwa nini na sisi tusipereke huko kuuza?
Tatizo hapa kwetu,kuna majizi mengi,unakuta bei kwenye soko la dunia ni nzuri tu,tatizo kuna makato mengi kwenye kila kilo ya kahawa,mpaka imfikie mkulima,anaambulia buku tu,
Tangu nasoma kipindi hicho miaka ya 1995,tatizo lilikuwepo,unaenda kuuza kwenye vyama vya ushirika(society),unaacha mzigo,unaondoka na maneno tu,pesa mpaka msimu ujao,ni utaperi mtupu,
Mimi siamini kama hili linafanyika kwa bahati mbaya,huu ni wizi wa kitaasisi unaoratibiwa na serikali,ili kudumaza maendeleo ya Kagera,na kunufaisha wachache,kuna conspiracy kubwa sana,hii kitu,ni kama ile iliyochangia kuuwa kiwanda cha General Tyre kule Arusha,
Lazima kuna foreign agents wanahusika hapa,
Hapo kwenye red ... si kweli hapa kuna wakoloni wa ndani ndo wanatuletea matatizo - hakuna foreign yeyote!
 
Tatizo Ni Maagizo Ya PM kuzuia sekta binafsi kununua kahawa moja kwa moja kwa mkulima na kuagza vyama vya ushirika ndivyo vinunue.
Nyuma ya maagizo hayo kuna faida gani? Nani anashinikiza maagizo hayo yanayowanyanyasa wazazi wetu huko vijijini?
 
Kwa mfano mahitaji ni tani 2 wewe ukizalisha tani 4 ukiuza kwa bei ndogo utailaumu serikali? Je ukilima kahawa zenye ubora mdogo ukauza bei ndogo utailaumu serikali.Nadhani tuache kujifananisha na Uganda maana wametuzidi sana japokuwa thamani ya hela yao ni ndogo kuliko yetu,
Nashindwa kukuelewa mkuu .. waganda wananunua ya kwetu (kwa njia wanazozijua wao) alafu wanaenda kuuza kwao kwa bei nzuri.
Hapo uelewe kuwa kahawa yetu sio mbovu kiasi hicho .. ndo hiyo inayovushwa na kupelekwa huko. Majuzi mzigo ulikamatwa ukipelekwa jirani...
 
kwa yeyote anayeweza kunipa faida za kuuza mazao kwenye vyama vya ushirika maana mim naona n usumbufu mtu
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom