Nini kifanyike ili kuiokoa CHADEMA?

Bw. Tindo, Vp shughuli za maendeleo zilizofanyika ambazo ni utekelezaji wa ilani ya CCM. Nazo ni fake? Rais huyu kwa kipindi cha miaka 5 amesimamia tu chuki dhidi ya CDM hakufanya lolote? Nahisi labda wewe ndo utakua na chuki dhidi yake na Serikali anayoiongoza.
 

Haipaswi kuwa ni uamuzi wa CCM Lissu kurejea na kupambana au la.

Hilo linapaswa kuwa ni moja katika hadidu za rejea za mwungano.

Inawezekana kuweka maazimio ya vyama vinavyo matter kumrejesha Lissu salama na kupambana. Hii ni whether CCM wanataka au hawataki.

Mbona Mali wanaelekea kusalimu amri.

Saa ya ukombozi ni sasa nasema rev. Mtikila (rip).
 
CHADEMA wakijifanya wabishi kila chama kitasimamisha mgombea wake na CCM itacheza hii game vizuri kwa kuwapa ACT viti vingi vya ubunge na CHADEMA itapewa viti 3 mpaka 5. Baada ya hapo ACT kinakuwa chama kikuu cha upinzani. Baada ya hapo CCM itaiundia ACT mizengwe ili kizoofike na kukipa ngivu chama kingine.

Wanyinga ndiyo wali wao πŸ˜‚ πŸ˜‚πŸ˜‚
 


Wakati utaamua! Tuvute subira.
 
Ahsante kwa kutushilikisha katika njozi zako bila kukuomba.
 
ACT ni Chama kilichojipanga.angalau kinaweza pata hata wabunge kumi.kuliko nyinyi ufipa na chama chenu mtaambulia wabunge watatu tu.
Wenye mbwa wanajua nguvu ya CDM, wenye mbwa walijiapiza kuwa CDM haitakuwepo kufikia leo..wewe endelea kuota!
 
Chama imara ubebwa na sera na sio polisi, maendeleo yeyeto Kama hayabadilishi maisha ya watu huwezi yaita maendeleo,hizo ni propaganda
 

Kwanza ujue shughuli zote za maendeleo hazifanyiki kwa hisani bali ni wajibu. Hata weupe wa Afrika kusini walisimamia maendeleo tena makubwa kuliko ya hapa kwetu, lakini waliendesha chuki kubwa sana ndani ya nchi hiyo. Usitake kujificha kwenye maendeleo yoyote maana maendeleo sio hisani ni wajibu. Ndio maana nasema, serikali hii inashurutisha ionekane demokrasia ni kikwazo cha maendeleo, jambo ambalo sio kweli.
 
Mie i think wacheni kife naturally..wanasiasa wengine wa emerge na vyama vingine vya upinzani viwe strengthern...
 
Ccm haijawahi kuimarika kiasi hiki tangu chama kimoja! Hizo zako ni ndoto za alinacha!
 
Hivi unatumi Nini kufikiri? Akili zingine zinakatisha tamaa kabisa hata kuzitekeleza! Eti siyo hisani...kina membe walipokuwa madarakani walishindwaje kuyafanya aliyoweza Magufuli? Mijitu mwingine inachosha mmfyuuuuu!
 
Weka nakala ya utafiti wenu
haaaa,,,we jamaa umenifurahisha sana.eti"weka nakala ya utafiti wenu".
yani unataka niweke ili ujue ni wabunge wepi wa upinzani watajitoa dk za majerui kabla ya tarehe ya uchaguzi?
 
haaaa,,,we jamaa umenifurahisha sana.eti"weka nakala ya utafiti wenu".
yani unataka niweke ili ujue ni wabunge wepi wa upinzani watajitoa dk za majerui kabla ya tarehe ya uchaguzi?
Kumbe hauna kitu, pole kwa kutegemea policcm na ghiliba. Mwaka huu kichwa kitakuuma bure. Mmechokwa.
 
Hivi unatumi Nini kufikiri? Akili zingine zinakatisha tamaa kabisa hata kuzitekeleza! Eti siyo hisani...kina membe walipokuwa madarakani walishindwaje kuyafanya aliyoweza Magufuli? Mijitu mwingine inachosha mmfyuuuuu!

Narudia tena, kutekeleza miradi ya maendeleo ni wajibu wa serikali yoyote maana ndio inayokusanya kodi. Hata serikali ya mkoloni ilitekeleza miradi ya maendeleo. Kina Membe walitekeleza yao, na pale walipochemsha tuliwapa ukweli wao. Magufuli kafanya muujiza gani mpaka apate uhalali wa kutumia madaraka yake kunajisi uchaguzi, au kuua vyama vingine vya siasa asivyovipenda?
 
Ahsante sana. Umeiweka vizuri safi kabisa. Itabidi niwe naku quote ili kuwasaidia waimba mapambio.
 
Naunga mkono hoja πŸ‘ŠπŸ½πŸ‘ŠπŸ½πŸ‘ŠπŸ½. Isomwe na Zitto kama kusimamisha mgombea mmoja wa upinzani kwenye Urais basi ni Lissu na siyo Membe.

 
Kumbe hauna kitu, pole kwa kutegemea policcm na ghiliba. Mwaka huu kichwa kitakuuma bure. Mmechokwa.
Sawa ila nyinyi komaeni kwenye mitandao.
sisi tunazama kwenye kina cha mkondo wa nungwi mpaka chini kabisa ya bahari ambapo nyinyi hata kwa dawa hamuwezi fika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…