Nini hatma ya Lowassa akikosa urais 2015?

Nini hatma ya Lowassa akikosa urais 2015?

Alfu Lela Ulela

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2010
Posts
1,255
Reaction score
77
Nimeziona juhudi za Lowasa ktk kuutafuta Urais wa jamhuri ya Tanzania kwa hali na mali kabla hata hajapata kashfa ya Richmond iliyomwondoa ofisini.

Aliposhinda Kikwete mwaka 2005 kila mtu alijua Lowasa atakuwa PM. na hakuna aliyeshangaa Lowasa kuwa PM wa nchi hii maana walijua anaandaliwa kuwa Rais mwaka 2015.

Lakini hata alipotupwa nje ya serikali kwa kashfa ya ufisadi bado hajapoteza matumaini ya kuongoza nchi hii. anafanya harakati za kujisafisha na kufanya publicity kila kukicha. anatoa misaada ya fedha, anakubali kila mwaliko, anafanya shughuli za kijamii ili tu kujipatia credit ya urais 2015.

Amefika mbali zaidi kwa kutumia media kujisafisha na kujipigia debe kwa gharama kubwa. (pitia gazeti la Rai leo).

SWALI:JE LOWASA ATAFANYAJE AKIUKOSA URAIS ANAOUOTA KILA SIKU? EITHER KWA KUKATALIWA NDANI YA CHAMA CHAKE ASIPITISHWE AU KWA KUKATALIWA NA WATANZANIA. JE ATAJIUA? ATATUBU NA KUMRUDIA MUNGU? ATAKIMBIA NCHI? ATASTAAFU SIASA? AU ATAFANYAJE?!!!!!!!!!!!!
 
Atakaa kama raia wengine na kumheshimu aliyechaguliwa.
 
kwani umeona jina lake kwenye karatasi ya kupigia kura?
wewe andaa list ya vitu unavyotaka chama na mgombea wake wawenavyo.....alafu uchague kutokana na msimamo wako...
alafu utaona jinsi maisha yatavyo boreshwa.....
 
Tatizo ni kwamba mtu akipatwa na obsession kama aliyonayo EL sasa, anaishia kuwa kipofu. Otherwise engemtembelea Mitt Romney ili asikie kutoka kwenye mdomo wa farasi!
 
Tutamtia mbaroni na kumburuza kortini kwa kufisidi nchi na kusababisha giza la Tanesco.
 
EL sio mchafu sana kama watu wanavyofikiria ingawa mimi simkubali...kitakacho msafisha mwisho wa siku ni kusema ukweli mengi tutayasikia tusubiri tu 2015
 
EL sio mchafu sana kama watu wanavyofikiria ingawa mimi simkubali...kitakacho msafisha mwisho wa siku ni kusema ukweli mengi tutayasikia tusubiri tu 2015

Justice delayed is justice denied. Kama kuna ukweli wowote anaotaka kuusema, ameshindwa nini kufanya hivyo hadi maelfu ya watanzania wamepoteza kutoka a ufisadi wa serikali ambayo ameendelea kuitunzia siri hadi sasa?

Na wenzake wakimgeuzia kibao kuwa ni political card atajibu nini?

EL hana kitu cha kumwokoa zaidi ya pesa zake na ndiyo maana kilio chake hakitakuwa tofauti na cha Mitt Romney!
 
Justice delayed is justice denied. Kama kuna ukweli wowote anaotaka kuusema, ameshindwa nini kufanya hivyo hadi maelfu ya watanzania wamepoteza kutoka a ufisadi wa serikali ambayo ameendelea kuitunzia siri hadi sasa?

Na wenzake wakimgeuzia kibao kuwa ni political card atajibu nini?

EL hana kitu cha kumwokoa zaidi ya pesa zake na ndiyo maana kilio chake hakitakuwa tofauti na cha Mitt Romney!

Great thought..!!!
 
Ataenda kuwa mfugaji kama mwenzake sumaye
 
EL sio mchafu sana kama watu wanavyofikiria ingawa mimi simkubali...kitakacho msafisha mwisho wa siku ni kusema ukweli mengi tutayasikia tusubiri tu 2015
Kama hasemi sasa, anasubiri uchaguzi ufike, ndipo aseme, afadhali akae tu kimya.... utakuwa unafiki kama wengi waliosema wanafahamu a, b, c... alafu hawasemi hata A tu
 
hajasema anagombea jaman mbona mnawahisha mambo, na akitaka kugombea c kuna taratibu, anachokifanya sasa ni kuwa karibu na jamii na kusikiliza changamoto zao then anazifanyia kazi zile zilizopo ndani ya uwezo, msubiri tu muda ukifika atatupa majibu yeye mwenyewe, mnajadili msichokijua.
 
Kama atagombea na kushindwa,fursa bado zipo nyingi sana.

Kwanini hatujiulizi tokea alipojiuzu mpaka sasa nini hatma yake?
 
wanajamvi tujadili hili suala,kwa mwndo anaokwenda nao lowassa ni waz hakuna mwanachama yeyete ndn ya ccm anaeweza kufuata alipo pita,amewaacha mbali sna wapinzan wake,sasa kuna tetes kuwa jina lake litakatwa mapema ili kuhakikisha hagombei nafas ya urais kwa tiketi ya ccm,sasa embu tujadili endapo ccm iitamkta jina lake nn kitatokea?????je ndo mwisho wa ccm au mzee wa mammvi atakubali yaishe????naomba ttujadili hili kwa mustakabli wa nchi yetu,ushabiki usio kuwa na maana tuuweke pemben
 
Back
Top Bottom