Nini hatma ya CHADEMA endapo watashindwa uchaguzi?

Nini hatma ya CHADEMA endapo watashindwa uchaguzi?

CHADEMA AIJAANZA KUSHINDWA LEO AU JANA TANGU VIANZISHWE VYAMA VINGI NAZANI SWALI LINGEKUWA YULE ALIYE ZOEA USHINDI AKIJASHIDWA ITAKUAJE?:bange:

Vipi ufuasi mkubwa namna kama hii umanza lini ?
 
Baada ya uchaguzi Chadema inabidi izaliwe upya,utakuwa ni wakati muafaka kwa uongozu mpya.

Tindu Lissu na Mnyika watapaswa wapewe mamlaka ya kuongoza chama.
 
Baada ya uchaguzi Chadema inabidi izaliwe upya,utakuwa ni wakati muafaka kwa uongozu mpya.

Tindu Lissu na Mnyika watapaswa wapewe mamlaka ya kuongoza chama.

Kwani huu uongozi uliopo una nini?
 
Kwani mara zote wameshiriki uchaguzi walikua na momentum kama ya mwaka huu? Ukipata jibu njoo.Hilo swali lako la ccm mshalijibu kuwa wakishindwa watakua wapinzani kila mtu anajua.mbona roho inakuuma nikiongelea hatma ya cdm endapo watashindwa?

Ndio CHADEMA mara zote huwa wana momentum kama hii ya mwaka huu. Kwani umewauliza wakakwambia kuwa chaguzi za nyuma hawakuwa na momentum? Hakuna chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi mkuu kwa ajili tu ya kushiriki bila kuwa na lengo la kushinda ili washike dola. Kila chama lengo lake ni hilo. Lakini ktk ushindani wowote kunakuwa na kushinda au kushindwa. Kwa hiyo, mimi sioni tatizo lolote kwa CHADEMA kama wakishindwa eti itakuaje. Jibu ni itakuwa kama ambavyo huwa wanakuwa wakishindwa km huko nyuma. Lakini tofauti inaweza kuwa ni kuingiza Wabunge wengi sn wa upinzani bungeni. Na hali hiyo itakuwa ni faida kubwa sana kwa demokrasia. Mtu anayedhani eti CHADEMA wakishindwa Urais watapoteza hata viti vya Ubunge atakuwa haoni uhalisia. Huku site tuliko mwamko wa wananchi ni mkubwa sana.
 
Ndio CHADEMA mara zote huwa wana momentum kama hii ya mwaka huu. Kwani umewauliza wakakwambia kuwa chaguzi za nyuma hawakuwa na momentum? Hakuna chama cha siasa kinachoshiriki uchaguzi mkuu kwa ajili tu ya kushiriki bila kuwa na lengo la kushinda ili washike dola. Kila chama lengo lake ni hilo. Lakini ktk ushindani wowote kunakuwa na kushinda au kushindwa. Kwa hiyo, mimi sioni tatizo lolote kwa CHADEMA kama wakishindwa eti itakuaje. Jibu ni itakuwa kama ambavyo huwa wanakuwa wakishindwa km huko nyuma. Lakini tofauti inaweza kuwa ni kuingiza Wabunge wengi sn wa upinzani bungeni. Na hali hiyo itakuwa ni faida kubwa sana kwa demokrasia. Mtu anayedhani eti CHADEMA wakishindwa Urais watapoteza hata viti vya Ubunge atakuwa haoni uhalisia. Huku site tuliko mwamko wa wananchi ni mkubwa sana.

Hiyo sentensi yako ya kwanza ni uongo!au mkuu momentum umeitafsiri vp?mimi nilimaanisha ''nguvu'' au huo mwamko wa huko ''site".kwahyo mwamko wa wananchi juu ya kuiondoa ccm mwaka 2005 na leo ni sawa?

Hata Hashim Rungwe na MacMillian Lyimo lengo lao ni kushika dola?

This time around na hyo kick ya lowassa wakishindwa ndo wanakufa hvo.Na nguvu ya upinzani bungeni itaendelea kwa ccm tu sababu ukawa sio chama tuseme kitakua kina wengi kuliko ccm.
 
Hili swali waoga hawawezi jibu, kama uonavyo watu wametoka nje ya mada na kuligeuza swali au kuishia kutukana.
ITAKUWA NDO MWISHO WA CHADEMA YA MBOWE, na itawachukua angalau miaka 20 kuja kuwa angalau chama cha kawaida, kushindwa kwa CHADEMA itakuwa ndio BIRTH ya ACT.
Ilipofika CHADEMA sasa hivi, ni DO or DIE. Na pia endapo CHADEMA (ukawa) watashinda, itakuwa ni term moja maana watafanya vibaya sana. Muhula wa pili watakufa kifo kibaya na ndio chadema itazikwa kabisa.

Nyongeza tu: Sisiemu ikishindwa, yategemeana na safu yao wataipanga vipi, wapige msasa wote wenye madoa, kwa kufanya hivi watarudi haraka kwenye ramani sababu ya poor perfomance ya ukawa madarakani. Niwe mkweli, kwa mtazamo wangu, naona ACT waki-gain momentum kila siku na watatumia makosa ya wapinzani wao, 2020 au 2025 kitakuwa cha kikubwa sana.
 
Hiyo sentensi yako ya kwanza ni uongo!au mkuu momentum umeitafsiri vp?mimi nilimaanisha ''nguvu'' au huo mwamko wa huko ''site".kwahyo mwamko wa wananchi juu ya kuiondoa ccm mwaka 2005 na leo ni sawa?

Hata Hashim Rungwe na MacMillian Lyimo lengo lao ni kushika dola?

This time around na hyo kick ya lowassa wakishindwa ndo wanakufa hvo.Na nguvu ya upinzani bungeni itaendelea kwa ccm tu sababu ukawa sio chama tuseme kitakua kina wengi kuliko ccm.

Najua ulimanisha hivyo, lakini ninachokisema hiyo nguvu au mwamko upo kila uchaguzi. Kama ni tofauti imetokana na kutofautiana kwa nyakati na majira, na sio sababu ya Lowassa. Sasa hivi wananchi wengi wamechoka hicho chama chenu cha CCM ambacho kinaonekana sasa kimechoka. Watu wengi wanataka mabadiliko, basi. Kwa hiyo, kuhusisha nguvu au mwamko uliopo mwaka huu na Lowassa pekee ni upotoshaji mkuu. Kuna watu wengi tu ukiongea nao mitaani wanasema kabisa kuwa mwaka huu hata wakiweka jiwe wako tayari kulipigia kura lakini sio CCM. Hata ungegombea wewe kupitia CHADEMA / UKAWA, watu wangekupa kura

Pili, hiyo dhana ya wakishindwa ndio wanakufa haina ukweli wowote, ni dua la kuku halimpati mwewe. Pamoja na kwamba UKAWA sio chama cha siasa, lakini ni mmoja unaoundwa na vyama vya siasa. Sasa km wabunge wataongezeka na kuwa wengi bungeni, wewe unadhani hawatakuwa ni wabunge wa vyama hivyo vya siasa kwa sababu tu UKAWA sio chama? Mimi naamini CHADEMA, CUF watakuwa na wabunge wengi tu wa kutosha. Kadhalika, hata NCCR itapata Wabunge. Wote hao wataunda kambi ikiwa watashindwa uchaguzi kama unavyotaka wewe
 
Swali la msingi Kuulizwa ni nini hatima ya CCM kama itashindwa? Maana ndio chama kilicho madarakani kwa sasa na chenye athari kubwa kama kitaukosa uraisi.
Kwa vyovyote vile Chadema hata ikiukosa urais uwezekano wa kuongeza idadi ya Wabunge ni mkubwa hivyo kuimarika zaidi na kuwa na nguvu kubwa bungeni.
Hayo mengine ni mawazo yako yasiyo na uhalisia
Unatakiwa ujibu swali la mleta uzi, sio kumuelekeza alitakiwa aulize vipi, ungeanzisha uzi wako kuhusu unavyotaka swali liwe na tungekuja kutiririka.
Mtazamo wangu na nafikiri ndo itakavyokuwa labda uamue tu kubisha ni kwamba, LABDA UKAWA wanaweza kuwa na wabunge wengi bungeni KULIKO awali, ila CHADEMA kama chama haiwezi kuwa na wabunge wengi bungeni.
 
Najua ulimanisha hivyo, lakini ninachokisema hiyo nguvu au mwamko upo kila uchaguzi. Kama ni tofauti imetokana na kutofautiana kwa nyakati na majira, na sio sababu ya Lowassa. Sasa hivi wananchi wengi wamechoka hicho chama chenu cha CCM ambacho kinaonekana sasa kimechoka. Watu wengi wanataka mabadiliko, basi. Kwa hiyo, kuhusisha nguvu au mwamko uliopo mwaka huu na Lowassa pekee ni upotoshaji mkuu. Kuna watu wengi tu ukiongea nao mitaani wanasema kabisa kuwa mwaka huu hata wakiweka jiwe wako tayari kulipigia kura lakini sio CCM. Hata ungegombea wewe kupitia CHADEMA / UKAWA, watu wangekupa kura

Pili, hiyo dhana ya wakishindwa ndio wanakufa haina ukweli wowote, ni dua la kuku halimpati mwewe. Pamoja na kwamba UKAWA sio chama cha siasa, lakini ni mmoja unaoundwa na vyama vya siasa. Sasa km wabunge wataongezeka na kuwa wengi bungeni, wewe unadhani hawatakuwa ni wabunge wa vyama hivyo vya siasa kwa sababu tu UKAWA sio chama? Mimi naamini CHADEMA, CUF watakuwa na wabunge wengi tu wa kutosha. Kadhalika, hata NCCR itapata Wabunge. Wote hao wataunda kambi ikiwa watashindwa uchaguzi kama unavyotaka wewe

Mimi nimesema ni mwana au mshabiki wa ccm?kwahyo mtu akikupa mawazo ambayo hutaki kuyasikia ingawa yanaweza kua na ukweli basi tayari ni ccm?

Ndo mana nikasema huo mwako wa mabadiliko kwa gharama yeyote ya hata kupigia kura jiwe ukaleta matokea ambayo sio,unadhani hali itakuaje kwa hao wananchi? Ndio hapo watajikatia tamaa na kina lowassa kurudi kwao wazazi wao na mwisho wa cdm yako(ingawa hujasema lakini umeonyesha ushabiki wa kupindukia)

Kwahyo UKAWA watashinda majimbo yote waliosimamisha wagombea kwa mantiki hiyo?
 
Habari!

Nini itakua hatma ya CHADEMA endapo matokeo ya uchaguzi yataonysha kuwa wameshindwa?Mimi naona huo ndio utakua mwisho wake kitabakia kama TLP ya Mrema.

Hawa makada wote wa CCM waliokuja na lowassa pamoja na lowasaa mwenyewe watarudi CCM wakiiacha cdm mchangani.Nasema hivi sababu wana CCM asilimia kubwa wameingia kimaslahi na maslahi yao yakishindwa kupatikana watarudi kwa mama na baba yao CCM.

Na hata wanachadema wengine asilia walimkubali Lowassa shingo upande sababu waliaminishwa atashinda kwahyo kushindwa kwake kutakua pigo kwao na kuwakatisha tamaa na CHADEMA.Na wananchi waliotaka kuitoa CCM kwa gharama yoyote nao watakata tamaa.CHADEMA imefikia katika kipindi muhimu sana katika historia yake,yani it either win or die!

Na kuna kitu kinaniambia kuwa Kama Magufuli akashinda uchaguzi ndio itakuwa mwisho wa upinzani Tanzania (instincts zangu zinaniambia hivo,ila logically impossible na intuitions nazo sio za kupuuza)
watabaki na waendesha bodaboda na walevi wa viroba..na wale baadhi trap niggas hapo ndio itakua certified kuwa upinzani ni genge la wahuni
 
Mimi nimesema ni mwana au mshabiki wa ccm?kwahyo mtu akikupa mawazo ambayo hutaki kuyasikia ingawa yanaweza kua na ukweli basi tayari ni ccm?

Ndo mana nikasema huo mwako wa mabadiliko kwa gharama yeyote ya hata kupigia kura jiwe ukaleta matokea ambayo sio,unadhani hali itakuaje kwa hao wananchi? Ndio hapo watajikatia tamaa na kina lowassa kurudi kwao wazazi wao na mwisho wa cdm yako(ingawa hujasema lakini umeonyesha ushabiki wa kupindukia)

Kwahyo UKAWA watashinda majimbo yote waliosimamisha wagombea kwa mantiki hiyo?

Mimi sio CHADEMA, lakini ninaunga mkono changes. Sio lazima niwe mwana CHADEMA ndio niunge mkono mabadiliko. Mimi sina chama chochote cha siasa. Ila chama chochote kinachoonesha nguvu ya kuitoa CCM madarakani nitakiunga mkono. Hata Shetani akija leo hii kuwa atasaidia kuifurusha CCM madarakani mimi niko tyr kumuunga mkono. Ndicho ninachofanya mkuu. Km CHADEMA itakufa ikishindwa uchaguzi mkuu ujao, basi ngoja tusubiri tutaona kwa macho yetu. Mimi sio mtabiri; wakati utasema. Let's wait, haina haja ya kuwa wapiga ramli wakati wino upo.

Maana kuna watu wanaona mabadiliko ni kwa ajili ya CHADEMA au wanasiasa tu; kitu ambacho sio kweli. Mabadiliko ni yetu sisi wananchi, hata kama hatuna vyama. Vyama vya siasa wanatuongoza tu kwa sbb wao wana political platform. Kwa hiyo, hasara ya kutopatikana kwa mabadiliko iko kwa wananchi wenyewe, na sio vyama km unavyodhani.
 
Hili swali waoga hawawezi jibu, kama uonavyo watu wametoka nje ya mada na kuligeuza swali au kuishia kutukana.
ITAKUWA NDO MWISHO WA CHADEMA YA MBOWE, na itawachukua angalau miaka 20 kuja kuwa angalau chama cha kawaida, kushindwa kwa CHADEMA itakuwa ndio BIRTH ya ACT.
Ilipofika CHADEMA sasa hivi, ni DO or DIE. Na pia endapo CHADEMA (ukawa) watashinda, itakuwa ni term moja maana watafanya vibaya sana. Muhula wa pili watakufa kifo kibaya na ndio chadema itazikwa kabisa.

Nyongeza tu: Sisiemu ikishindwa, yategemeana na safu yao wataipanga vipi, wapige msasa wote wenye madoa, kwa kufanya hivi watarudi haraka kwenye ramani sababu ya poor perfomance ya ukawa madarakani. Niwe mkweli, kwa mtazamo wangu, naona ACT waki-gain momentum kila siku na watatumia makosa ya wapinzani wao, 2020 au 2025 kitakuwa cha kikubwa sana.

Naona unaelewa kua ilipofikia cdm ni either win or die!(ni kipofu tu wa fikra hawezi kuona hili).Ila nataka kutofautiana na wewe kua cdm wakishinda watavurunda.na sifikiri kua kama ccm wakishindwa itawachukua round moja kurudi.

Ilo la ACT nalo napingana na wewe sababu ni chama cha mtu mmoja na chama cha kigoma tu.
 
nini hatma ya ccm na hizi tafiti zao zinapingwa kila kona na makundi hayo hayo waliotajwa kwenye tafiti zao kuwa wako pamoja ,uchaguzi utakapofanyika ibainike kura zao hazitoshi na wameshindwa itakuwaje ,wamejipanga kukabidhi kijiti bila purukushani
 
Je kitakuwa wapinzani wa kweli kama chadema? Au ndio kama udp..

Tena watakua wapinzani wa ukweli sana sababu watakua wanatamani warudi madarakani na hapo ndo hii nchi itaendelea.
 
Baada ya uchaguzi Chadema inabidi izaliwe upya,utakuwa ni wakati muafaka kwa uongozu mpya.

Tindu Lissu na Mnyika watapaswa wapewe mamlaka ya kuongoza chama.
Mnyika apewe uongozi, sio Tundu Lissu, Tundu Lissu ameonesha udhaifu wa hali ya juu kwa msomi kama yeye. Anakurupuka na anatoa majibu ya saluni za wanawake kwa maswali mazito. Amekula matapishi yake, ameonesha hana msimamo hata kwa body language. Mnyika ameonesha ukomavu fulani, body language ya Mnyika na Mdee speaks volumes. Mnyika wenye akili tumeona na tunajua kabisa kuwa hakubaliani na kinachoendelea na kilichotokea cha kuwapokea makapi na kuiweka kapuni chadema asili, ila kafanya yake kama mgombea ubunge, kanadiwa na Lowassa na kasema chagua Lowassa. HATUJAMUONA yule Mnyika machachari wa bungeni akiwa anamnadi Lowasa, (akili za kuambiwa changanya na zako hapa).
 
Kwani huu uongozi uliopo una nini?

Mbowe kabet kwa Lowassa this time,isipowork inabidi awajibike kwa uamuzi huo ambao umeibadili Chadema kuwa chama tofauti,badala ya kuwa kinara wa mapambano ya ufisadi Chadema imewakumbatia sasa mafisadi.

Ni ngumu kwa Mbowe kama mwenyekiti kuongoza tena Chama kitakachokemea ufisadi, ndio maana ni vyema kuja na timu mpya,Tindu Lissu na Mnyika wangefaa kuongoza timu hiyo.
 
Naona unaelewa kua ilipofikia cdm ni either win or die!(ni kipofu tu wa fikra hawezi kuona hili).Ila nataka kutofautiana na wewe kua cdm wakishinda watavurunda.na sifikiri kua kama ccm wakishindwa itawachukua round moja kurudi.

Ilo la ACT nalo napingana na wewe sababu ni chama cha mtu mmoja na chama cha kigoma tu.
Sitegemei watu wote watakuwa sisiemu endapo itashinda, kuna watu watakuwa wakikinzana na sera za sisiemu na watatafuta jukwaa (chama cha siasa) kuwatetea. Wachache watabaki chadema ya lowassa, ila kama lowassa akishindwa, baada ya mwaka ANASTAAFU siasa, Sioni vyama vilivyopo ktk ukawa kama vitapona endapo chadema (ukawa) watashindwa, hivyo tutabaki na chama kimoja cha upinzani chenye nembo (Zitto) ambacho hakikiwa sehemu ya ukawa.
Kwangu mimi hili suala la chama cha mtu nafikiri ni propaganda tu.
 
Mimi sio CHADEMA, lakini ninaunga mkono changes. Sio lazima niwe mwana CHADEMA ndio niunge mkono mabadiliko. Mimi sina chama chochote cha siasa. Ila chama chochote kinachoonesha nguvu ya kuitoa CCM madarakani nitakiunga mkono. Hata Shetani akija leo hii kuwa atasaidia kuifurusha CCM madarakani mimi niko tyr kumuunga mkono. Ndicho ninachofanya mkuu. Km CHADEMA itakufa ikishindwa uchaguzi mkuu ujao, basi ngoja tusubiri tutaona kwa macho yetu. Mimi sio mtabiri; wakati utasema. Let's wait, haina haja ya kuwa wapiga ramli wakati wino upo.

Maana kuna watu wanaona mabadiliko ni kwa ajili ya CHADEMA au wanasiasa tu; kitu ambacho sio kweli. Mabadiliko ni yetu sisi wananchi, hata kama hatuna vyama. Vyama vya siasa wanatuongoza tu kwa sbb wao wana political platform. Kwa hiyo, hasara ya kutopatikana kwa mabadiliko iko kwa wananchi wenyewe, na sio vyama km unavyodhani.

Yani kama ungekua umeongea kwanzia mwanzo kama ulivoandika hiyo para ya kwanza kusingetokea malumbano yoyote sababu ndio thread yangu inaongelea hvo.Na usifikiri mimi sitaki mabadiliko ni ngali sio mwanachama wa chama chochote yani kama wewe tu mkuu Kaptula la Marx

Ila kitu kingine,usitegemee siasa kwa 100% ikuletee madadiliko katika maisha yako.baadhi ya watu wanaona mabadiliko ni kwa wanasiasa na wanachadema tu sababu washawaona hao wenye political platform (ccm) wanafanya nini kwahyo wakiwapa wengine platform watafanya hivyo hivyo tu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom