Nini hatma ya CHADEMA endapo watashindwa uchaguzi?

Nini hatma ya CHADEMA endapo watashindwa uchaguzi?

bukoba boy

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2015
Posts
5,376
Reaction score
3,976
Habari!

Nini itakua hatma ya CHADEMA endapo matokeo ya uchaguzi yataonysha kuwa wameshindwa?Mimi naona huo ndio utakua mwisho wake kitabakia kama TLP ya Mrema.

Hawa makada wote wa CCM waliokuja na lowassa pamoja na lowasaa mwenyewe watarudi CCM wakiiacha cdm mchangani.Nasema hivi sababu wana CCM asilimia kubwa wameingia kimaslahi na maslahi yao yakishindwa kupatikana watarudi kwa mama na baba yao CCM.

Na hata wanachadema wengine asilia walimkubali Lowassa shingo upande sababu waliaminishwa atashinda kwahyo kushindwa kwake kutakua pigo kwao na kuwakatisha tamaa na CHADEMA.Na wananchi waliotaka kuitoa CCM kwa gharama yoyote nao watakata tamaa.CHADEMA imefikia katika kipindi muhimu sana katika historia yake,yani it either win or die!

Na kuna kitu kinaniambia kuwa Kama Magufuli akashinda uchaguzi ndio itakuwa mwisho wa upinzani Tanzania (instincts zangu zinaniambia hivo,ila logically impossible na intuitions nazo sio za kupuuza)
 
Swali la msingi Kuulizwa ni nini hatima ya CCM kama itashindwa? Maana ndio chama kilicho madarakani kwa sasa na chenye athari kubwa kama kitaukosa uraisi.
Kwa vyovyote vile Chadema hata ikiukosa urais uwezekano wa kuongeza idadi ya Wabunge ni mkubwa hivyo kuimarika zaidi na kuwa na nguvu kubwa bungeni.
Hayo mengine ni mawazo yako yasiyo na uhalisia
 
Hatma ya CCM kama itashindwa ni kitakua chama pinzani.unaulizaje swali la kitoto kama hili?
 
Hatma ya ccm kama itashindwa ni kitakua chama pinzani.unaulizaje swali la kitoto kama hili?

Sasa hilo swali lako la kiutu uzima unadhani chadema ikishindwa itakuaje, basi CHADEMA itakua kampuni
 
Akili za kuambiwa changanya na zako kaka. Aliyekwambia CHADEMA wakishindwa ndio mwisho wa upinzani Tanzania kakudanganya na wewe ukayachukua kuchwa kichwa kuleta umbea wako wa Lumumba. CHADEMA iko imara mpk kesho.
 
Hatma ya ccm kama itashindwa ni kitakua chama pinzani.unaulizaje swali la kitoto kama hili?

Huwezi kusustain mdahalo ndiyo maana ukakuwa too defensive! Unauliza swali la kitoto unajibiwa kiutu uzima unaishia kutokwa na povu!
 
bukoba boy hili swali hata mamako juzi kaniuliza hivyo hivyo! Wewe nendeni mkaulizane hapo home kwamba nini hatima ya ccm mwaka huu?
 
Story za "mwana mpotevu" haziko applicable hapa...hatutapokea mafisadi makapi ya uchaguzi mkuu
 
Akili za kuambiwa changanya na zako kaka. Aliyekwambia CHADEMA wakishindwa ndio mwisho wa upinzani Tanzania kakudanganya na wewe ukayachukua kuchwa kichwa kuleta umbea wako wa Lumumba. CHADEMA iko imara mpk kesho.

Wazee wa mihemko.Hata lumumba penyewe sipajui mimi.
 
Kwatarifa yako hawa farasi wa kijani tushawachoko😦 bukoba boy.
 
Wazee wa mihemko.Hata lumumba penyewe sipajui mimi.

Sasa kama haupajui utumbo wa nini? Wewe unashindwa kujiuliza swali dogo tu la darasa la kwanza? Wewe umeona CHADEMA ndio chama tawala nini mkuu? Au ndio mara ya kwanza wapinzani kushiriki uchaguzi, kwamba wakishindwa itakuwa ndio mara ya kwanza au? Mimi nadhani swali lako ulitakiwa ujiulize je CCM ambao wako madarakani wakishindwa itakuaje. Maana CCM ndio chama tawala na chaguzi zote huko nyuma tangu 1995 wamekuwa wakishinda. Kinyume na hapo ni umbeya tu wa Lumumba. Tanzania mpya inakuja!
 
CHADEMA AIJAANZA KUSHINDWA LEO AU JANA TANGU VIANZISHWE VYAMA VINGI NAZANI SWALI LINGEKUWA YULE ALIYE ZOEA USHINDI AKIJASHIDWA ITAKUAJE?:bange:
 
Sasa kama haupajui utumbo wa nini? Wewe unashindwa kujiuliza swali dogo tu la darasa la kwanza? Wewe umeona CHADEMA ndio chama tawala nini mkuu? Au ndio mara ya kwanza wapinzani kushiriki uchaguzi, kwamba wakishindwa itakuwa ndio mara ya kwanza au? Mimi nadhani swali lako ulitakiwa ujiulize je CCM ambao wako madarakani wakishindwa itakuaje. Maana CCM ndio chama tawala na chaguzi zote huko nyuma tangu 1995 wamekuwa wakishinda. Kinyume na hapo ni umbeya tu wa Lumumba. Tanzania mpya inakuja!

Kwani mara zote wameshiriki uchaguzi walikua na momentum kama ya mwaka huu? Ukipata jibu njoo.Hilo swali lako la ccm mshalijibu kuwa wakishindwa watakua wapinzani kila mtu anajua.mbona roho inakuuma nikiongelea hatma ya cdm endapo watashindwa?
 
Back
Top Bottom