Ossaessa
Member
- Feb 22, 2020
- 17
- 9
Salam wana JF
Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la wananchi, wanasiasa, viongozi wa dini, taasisi mbalimbali pamoja na baadhi ya Viongozi wastaafu kutaka iundwe Tume Huru ya Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu, 2020. Upande wa pili kumeibuka kundi linalopinga uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya Oktoba mwaka 2020. Kundi hili limejaa wanasiasa watupu hususan wa Mrengo fulani.
Hoja ya kundi la kwanza imejikita kwenye haki, wanasema Tume Huru ya Uchaguzi itasimamia uchaguzi ulio huru na haki na kuondoa kasoro kama zilizojitokeza kwenye chaguzi ndogo za marudio na ule wa Serikali za Mitaa. Wanakazia hoja yao kwa wakurugenzi ambao ni wanachama wa chama fulani kinachoshiriki Uchaguzi na ni wateule wa mmoja ya wagombea kusimamia uchaguzi hauwezi kuwa huru na wa haki. Upande wa pili unaopinga tume huru hoja yao wanasema huu sio wakati wa kuunda Tume Huru ya Uchaguzi.
Wanaenda mbali kwa kusema kama tume sio huru mbona wapinzani wanashinda?
Nihitimishe kwa kuuliza nini maoni yako juu ya Tume Huru ya Uchaguzi in faida gani au hasara gani kwa taifa letu?
Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la wananchi, wanasiasa, viongozi wa dini, taasisi mbalimbali pamoja na baadhi ya Viongozi wastaafu kutaka iundwe Tume Huru ya Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu, 2020. Upande wa pili kumeibuka kundi linalopinga uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya Oktoba mwaka 2020. Kundi hili limejaa wanasiasa watupu hususan wa Mrengo fulani.
Hoja ya kundi la kwanza imejikita kwenye haki, wanasema Tume Huru ya Uchaguzi itasimamia uchaguzi ulio huru na haki na kuondoa kasoro kama zilizojitokeza kwenye chaguzi ndogo za marudio na ule wa Serikali za Mitaa. Wanakazia hoja yao kwa wakurugenzi ambao ni wanachama wa chama fulani kinachoshiriki Uchaguzi na ni wateule wa mmoja ya wagombea kusimamia uchaguzi hauwezi kuwa huru na wa haki. Upande wa pili unaopinga tume huru hoja yao wanasema huu sio wakati wa kuunda Tume Huru ya Uchaguzi.
Wanaenda mbali kwa kusema kama tume sio huru mbona wapinzani wanashinda?
Nihitimishe kwa kuuliza nini maoni yako juu ya Tume Huru ya Uchaguzi in faida gani au hasara gani kwa taifa letu?