Ningetawala...........

mzawahalisi

JF-Expert Member
Jan 11, 2010
752
237
Habari za asubuhi ndugu zangu watanzania. Tumekuwa walalamikaji tuu mda mwingi bila ta kutoa majibu ya matatizo yetu yanayo tukabil. Kwa lugha ya picha, tupo ndani ya gari tunasafiri. Ila limekwama kwenye matope. Na wenye jukkumu ya kuliendesha wamebakia kukanyaga mafuta tuu, gari inaslip tuu na kumaliza mafuta, tunachangishwa tena nauli na kunulia mafuta na kuwalipa posho za ziada hawa madereva ili hali Hatuendi popote. Sasa wewe kama mmoja wa abiria wa gari hili umefika wakati wakusema hapana, hatuwezi kesha hapa hapa kila siku. Tufanye hivi ili tutoke hapa kwenye matope tuendelee na safari.
Je wewe Ungepata nafasi ya kuendesha hili gari, ambalo ni Nchi yetu nzuri, ungefanyaje?
Ningetawala ............
Karibuni wadau kwa mitazamo yenu tofauti tofauti.
 
Habari za asubuhi ndugu zangu watanzania. Tumekuwa walalamikaji tuu mda mwingi bila ta kutoa majibu ya matatizo yetu yanayo tukabil. Kwa lugha ya picha, tupo ndani ya gari tunasafiri. Ila limekwama kwenye matope. Na wenye jukkumu ya kuliendesha wamebakia kukanyaga mafuta tuu, gari inaslip tuu na kumaliza mafuta, tunachangishwa tena nauli na kunulia mafuta na kuwalipa posho za ziada hawa madereva ili hali Hatuendi popote. Sasa wewe kama mmoja wa abiria wa gari hili umefika wakati wakusema hapana, hatuwezi kesha hapa hapa kila siku. Tufanye hivi ili tutoke hapa kwenye matope tuendelee na safari.
Je wewe Ungepata nafasi ya kuendesha hili gari, ambalo ni Nchi yetu nzuri, ungefanyaje?
Ningetawala ............
Karibuni wadau kwa mitazamo yenu tofauti tofauti.

Toa maoni yako kwanza nini cha kufanya kabla hujapata maoni ya wengine
kama mnaenda sawa.Inawezekana ni wewe peke yako unaona gari imekwama kwenye
matope wakati wengine wana 4WD wanakatiza matope,milima,mito bila wasiwasi.
Je,ungetawala kwa misingi gani tofauti na Azimio la Arusha ambalo limepigwa teke na chichiem kule zenji?
Tupe uroda MZAWAASILI
 
mimi ningetawala ningefuta vyama vyote vinavyoendekeza udini na ukabila(chadema, kasikazini) na (cuf, zanzibar). Nasema hivo kwa sababu udini umetawala sana katika hivi vyama na viongozi wao hawataki kuguswa! Ukiwagusa tu wanakulowa kama samaki kwenye maji na kukutupa nje! Ningebaki na chama kimoja tu cha CCM na kuruhusu wagombea binafsi na ninaamini hii ingekuwa bora zaidi ili kupunguza udini na ukabila.:A S 465:
 
Technician, Ukiangalia mijadala Mingi hapa jamvini inaonyesha kwamba wanchi hatujaridhika na spidi ya maendeleo ya nchi yetu. mara nyingi tunalaumu na wengine kufikia kuwatukana Madereva wanao tuendesha. Sasa ningependa Kupata Mitazamo tofauti kutoka kwenu waungwana. Let keep our Great Mind at work. Usigope kutoa mawazo yako, hata kama mtu ata yacopy na kuyafanyia kazi ni kwa maendeleo ya taifa letu sote. Nothing to lose.
Jakubumba ndugu nimekupata, huo nimtazamo wako, je unafikiri hiyo inatosha kulikwamua taifa letu linaloonekana Kukwama kuanzia level za chini kabisa? Sasa hivi kila kitu Dar kina udalali, hata ukienda karume kwenye mitumba unapokelewa na madallali!!!!!
Twende kazi sasa...
 
mimi ningetawala ningefuta vyama vyote vinavyoendekeza udini na ukabila(chadema, kasikazini) na (cuf, zanzibar). Nasema hivo kwa sababu udini umetawala sana katika hivi vyama na viongozi wao hawataki kuguswa! Ukiwagusa tu wanakulowa kama samaki kwenye maji na kukutupa nje! Ningebaki na chama kimoja tu cha CCM na kuruhusu wagombea binafsi na ninaamini hii ingekuwa bora zaidi ili kupunguza udini na ukabila.:A S 465:
Mawazo yako yanafanana na ya ccm kweli. Hivi kuna chama unaoendekeza udini kama CCM hapa nchini kupitia kwa mwenyekiti wako JK. Angalia jinsi anavyoteuwa waislam wengi kwenye nafasi mbalimbali, angalia jisnsi anavyotumia BAKWATA visivyo. Wewe acha bwana. Tulioko kwenye system tunafahmu everything.
 
Ndugu CHIETH, huo nimtazamo wa Ndugu yetu, hapa ni Brain storming, hilikataliwi wazo, cha msingi tupe Mawzo yako kama moja ya Magreat Thinker wa kizazi chetu Hiki.

Wana jamii hembu come up. Unaweza ukawa na fikra nyingi ama mawazo mapana ya nini kifanyike, na wewe sio mwana siasa wala hutegemia kuja kuwa. Yafaa nini kufa na mawazo yako ambayo unayaamini ndio sahihi Juu ya uelekeo wa nchi Yako!
Jimwage hapa jamvini, bila kizuizi, hapa kuna watu wa kilaaina, huwezi jua mchango wako unaweza saidia siku moja kati ya hawa wanasiasa na Viongozi waka ya kubali na kuyatumia. Nafasi ni hii........
 
masaburi yamekuelemea hata mawazo yako ni ndani ya masaburi na umerogwa na mwendawazimu aliye kufa sio bure
 
masaburi yamekuelemea hata mawazo yako ni ndani ya masaburi na umerogwa na mwendawazimu aliye kufa sio bure

Okeeee, haya ndo mawazo yako, kwa kuwaa tumeiita hii ni brain storming huwa hatukatai wazo hata kama halieleweki. Mwisho wa yote ndo tuta analyse na kuona mchele ni upi. Thank you.
 
kuna abiria wanapenda mwendo kasi, wastani na wengine polepole. kukwama kunategemea hali ya barabara (barabara ndio wananchi) ikoje pengine ni mbovu( pengine wananchi si wazalendo)
 
unadhani wakati wote dereva akikwama ni makosa yake peke yake bila kuzingatia miundombinu? uimara wa gari ulilopewa kuendesha pia ni sababu labda kama ni gari jipya. Kikwete kapewa gari (tanzania) si jipya. gari lilishatembelewa na kufanya safari kibao ni mkweche sasa.
 
Ukifika ubungo chagua gari (basi) jipya kwani basi linaloitwa Tanzania lina miaka hamsini barabarani unampa lawana dereva aliyeanza kuendesha gari likiwa na miaka 40 barabarani?
 
dereva yuko makini labda mmiliki wa gari ambaye ni mwananchi na yeye ni wa kutazamwa. usikute mmiliki wa gari hapendi kununua vipuri kwa ajili ya matengenezo. think twice
 
jipange sawasawa kabla hujarusha thread. Hata kama umelipwa posho kwa kazi hiyo kibarua kitaota mbawa na kupepea. kulipwa posho ndogo ndio iwe sababu ya kulipua.
 
Samahani wadau nilipata Dharula kidogo, ndiomanaana nikawa kimya kidogo.
Tuendelee...
Naona tayari watu wamesha kuja na mawazo Hasi.
Nieleweke, siko hapa kumlaumu mtu. Weka imani katika kujenga na sio wakati wote katika mapambano ama malumbano.
1.Mama porojo, sasa wewe Ndo dereva umepewa hili gari na kama maelezo yako yanavyo sema, labda 'barabara' Ndio mbovu, kwamba wananchi wamekosa uzalendo, ama gari imechoka, kwamba imepitia mikononi mwa madereva wengi. Sasa wewe na mimi nayule wote ni familia moja na hili gari ni letu la Urithi haliuziki. Labda niweke lugha ya picha pembeni. Hii ni nchi yetu sote, kila mmoja ana wajibu wa kufikiri ni nanmna gani Nchi hii itaendelea. Wakore Kusini baada ya vita yao na Korea Kaskazini walikuwa na hali mbaya kuliko sisi, lakini leo wameenda mbali sana zaidi yetu ndani ya miaka hamsini hii hii.
Sasa tutimize wajibu wetu kufikiri juu ya Maendeleo yetu sote.
Speak Your Mind out here.
2. Mbu sugu, mimi na wewe ndo wamiliki wa hili gari, tufanyaje tuendelee? Tuzungumze.
3. Fofofo, sio madhumuni ya Thread hii kumwangalia mtu wala taasisi yoyote, hapa ni nchi kwa ujumla bila vipande vipande. Nani anaweza nituma kuja kuandika hapa? Ama thread hii unaona kama inamlengo wa taasisi yeyote? Kama kunakitu kinaelekea huko, basi uniwie radhi na unionyeshe hicho kitu kwa maana sio nia ya thread hii. Naona Vyama vimetudumaza hata kimitazamo, kilakitu tunaanza kuangalia hichi ni chama hiki ama kile? Hapana just be neutral na hatuzungumzii taasisi yeyote hapa. Karibu kwa mchango wako kimtazamo chanya juu ya taifa letu.
4. Mwisho niwape mfano kuna kundi moja la mziki wa kizizi kipya kUtoka wanaitwa Necessary Noise toka kenya, waliimba wimbo unaitwa Nikitawala... Wakatoa mtazamo wao, hhaswa mwanadada Anaitwa Naazizi kamasijakosea. Nahitaji kitu kama hicho kutoka kwenu Viongozi.
I LOVE MY COUNTRY TANZANIA.
 
Ningefuta leseni za madeleva kutoka ccm

Je kiongozi, kufuta lesseni basi yatosha kutuendeleza? Tupe nini ungefanya kusukuma gurudmu letu la Maendeleo?
Labda ningefanya hivi kwenye kilimo, vile kwenye elimu, na ili kururdisha uzalendo na maadili ya kitaifa yanayoonekana kumomonyoka ungefanya nini kuyajenga haya yoye?
 
Back
Top Bottom