Kabla ya kulala fanya mambo haya

Kabla ya kulala fanya mambo haya

Wakusolve

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2020
Posts
561
Reaction score
991
Kabla ya kulala fanya mambo haya

Kabla ujalala pangilia mambo yako vizuri, iwe ni sehemu ya jiko, sebuleni, na mazingira yote weka katika usafi na mpangilio.

Pia kabla ya kulala omba kwa Mungu, soma vitatu vya Mungu inafanya akili na moyo wako kutulia na asubuhi unaamka mwepesi

Unapoweka Mazingira katika usafi na mpangilio itakusaidia asubuhi unapo amka unakuwa unajisikia vizuri, utajikuta moyo wako una amani, utulivu wa akili, hauna mawazo.

Mazingira yenye usafi na mpangilio yanavuta nguvu chanya, yanafanya ubongo wako ufanye kazi vizuri hii inasaidia kujisikia mwepesi(light) unapo amka , mchangamfu na pia kujisikia vizuri.

Faida ya mambo haya yatakusaidia kwenye shughuri zako za kila siku, hiwe kazini kwako au sehemu ya biashara.

Unapokuwa unajisikia vizuri inapelekea kuvuta vitu chanya wakati huo, utajikuta siku hiyo unapata wateja wengi, mambo yako yanaenda vizuri sababu ya hali ulionayo.

Watu wengi wanajiuliza mbona siku hii ya leo nimepata wateja wengi sana kwenye biashara yangu

sababu kubwa ni siku hio unajisikia vizuri(wengine wanasema leo nimeamka vizuri ndio maana nimepata wateja wengi

Lakini ukweli ni kwamba unapojisikia vizuri, una amani na utulivu ndani yako basi ulimwengu unakuletea vitu chanya kama pesa kupitia wateja, watu kuvutiwa na kutaka kuwa karibu na wewe, watu kukupa offer siku hiyo .

Kwa ufupi nyota(aura) yako inakuwa ina n'gaa siku hiyo sababu ya hali ulionayo ndani inapelekea kuvuta vitu vizuri vya nje.

hivyo pia unapojisikia vibaya inakuletea mambo kama hayo mpaka utakapo badilisha hali na kuwa chanya.

tengeneza Mazingira kwa usafi na mpangilio ili uendelee kuvuta nguvu chanya kwenye maisha yako, usafi na mpangilio ni kitu muhimu sana kwenye maisha.
 
Shukrani sana 🙏🙏🙏
Ila wengine sisi tunajiegesha tu kama gari bovu
 
Yote hayo yanawezekan pindi tu uko na maelewano mazuri na mwenza wako au familia kiujumla na, uwe ktk mazingira bora, barabara zipitike, maji ya safi na salama, na afya njema
 
Back
Top Bottom