Valentine Yusuph
Member
- May 5, 2019
- 6
- 2
Wadau wa JF, nimetokea kumpenda msichana mmoja ambaye nasoma naye chuo. Nilishamwelezea hisia zangu juu yake akanielewa na kukubali tuanzishe mapenzi, ilikuwa 2017. Mpaka leo bado nawasiliana naye lakini sipati kitu, nikimuita kwangu anakuja lakini hataki hata nimguse, nikimuomba anasema nikatoe mahari kwanza. Sio kwamba hajawahi kufanya mapenzi (alinambia alishawahi kupendana na mtu wakaachana baada ya yeye kuja chuo 2016). Nimeanza kupoteza hisia kwake. Nifanyeje?