simplemind
JF-Expert Member
- Apr 10, 2009
- 16,697
- 9,590
Hivi TZ tukitana kujitoa EAC tunapaswa kufanya nini? ni Bunge kupiga kura au wananchi kupiga kura ya Maoni tujitoe kabisa EAC na tujikite SADC haswaaa!!
Zanzibar can go. Tanzania will always prevailIli kumaliza fitina zoezi hili lienda sambamba na kura ya maoni kuendelea au kusitisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Zanzibar haina masilahi yeyote SADC ukilinganisha na EAC.
Zanzibar can go. Tanzania will always prevail
Kama ilivyokuwa mwaka 1977 ambapo wajuaji walikuja na majigambo yao na kuubeza umoja wa Afrika Mashariki leo hii nauona huu wa sasa siyo ushirikiano wa Afrika Mashariki bali ndani yake viongozi hawa wamejaa mate ya hasira kwa Tanzania. Ushauri wa Kikwete kwa Kagame ilikuwa sababu tu lakini fukuto lilishakuwepo pale Tanzania ilipokataa ardhi isiwepo kama kitu halali kwa wanajumuuiya kurithi.
Naunga mkono sana ardhi yetu isiwe shamba la bibi kila mwana Afrika Mashariki akarithi nasema heko Jakaya Kikwete kwa kupinga hilo na hilo ndilo linalowauma sana. Sasa hivi wameanza kubuni mbinu za kupanga uzazi ili kuwe na limit za kuzaa kisa ni uhaba wa ardhi. Niafadhali Tanzania ijitoe katika muungano huu wa mashaka. Wakati Rwanda ikiomba kujiunga Jumuiya ya Afrika Mashariki wengi walitabiri kuwa huu utakuwa ni mwisho wa uwepo wa Jumuiya Halisi ya Afrika Mashariki, sasa nakubali.
Jana katika majarida inasemekana Kikwete alialikwa kuhudhuria mkutano wa wakuu kule Rwanda, hakika Mh. Kikwete alifanya jema kukataa kwenda. Mh. Rais bado tunakupenda sana. Jumuiya hii ya Afrika Mashariki iko ICU hatuna haja nayo, turudi zetu SADC. Yule kiongozi wa waasi M23 amerudi kwao Uganda kujipanga upya nasema karudi kwao kwasababu Uganda na Rwanda wanakifadhili kikundi hiki kuivuruga DRC ya Kabila.
Kama Museveni aliishi hapa Tanzania kule Bukoba na kupatia urais wake kwa msaada wa Tanzania laana itamkuta tu. Kama Kagame aliishi hapa Mtoni Kwa Aziz Ally na kutulia akupanga namna atakavyoitawala Rwanda hapo baadaye basi naye huyu hii laana ya kujitenga haitamuepuka.
Sisi Watanzania hatushangai kamwe kuona tabia hii ya ubaguzi inavyoshamiri kwani HAO WAMEZOEA KUBAGUANA. Hadi sasa wanajaribu kuwa wamoja lakini muziki huu hawatauweza roho zao zimeumbwa zikiwa na vyumba vya uhasama. Tanzania ni nchi ya mfano kwa umoja wake. We are BIG NATION MEEEEEN!!!
Kiburi cha Kagame + Usugu wa Museveni X Uwepo wa Uhuru = Hila, Hasira, Kutiliana Shaka, Viburi na Mwisho wake KUSAMBARATIKA. Muda si mrefu Uhuru Kenyatta ataota kiburi cha kujifanya ndiye mwezeshaji wa utengemao wa Jumuiya yao mpya. Baba yake Mzee Jomo Kenyatta aliiheshimu sana Tanzania.
Mh. Samwel Sitta ametoa tamko zuri sana kwamaba sisi siyo wakupewa talaka bali ni wa kutoa talaka kwa hao wanawali, Tanzania ilikuwa na wazo la kuunda umoja huu Kenyatta akalikubali akafuatia Milton Obote. Hivyo ni sisi tunatakiwa tutoe talaka kwamba hatuwataki.
TANZANIA IS A GREAT NATION FOREVER.
i fear to call you stupid but you are!ma Tanzania bana,
Yes Sir, it will prevail as an unpleasant bundle wrapped up in itself.
Zanzibar can go. Tanzania will always prevail
Hizi akili za kibwege ndio matatizo yote,ndio maana wameamua kuendelea na mipango yao kivyao na anayelalmika na maneno ya kidwanzi ni watu kama wewe,...second world my azz!!!
Hizi akili za kibwege ndio matatizo yote,ndio maana wameamua kuendelea na mipango yao kivyao na anayelalmika na maneno ya kidwanzi ni watu kama wewe,...second world my azz!!!
Unaandikanini tazama uchumi wa KENYA na RWANDA ndipo ujue
Nakuheshimu. Shikamoo.Bubu Msemaovyo,
Nakubaliana na wewe kwa yote uliyosema kasoro moja tu; nalo hiyo kutimia kwa heading yako! Sina shaka kabisa kwamba ingekuwa ni Rais mwingine, EAC isingechukua hata miezi sita ijayo!! Lakini kwa JK, I doubt unless movie ianzie bungeni!
Hata tusivyompenda, JK ana busara sana yule mzee! Kwa bahati mbaya, busara zikizidi zinageuka na kuonekana kama udhaifu na ndio maana sikushangaa Mnyika alipomuita JK ni dhaifu! Pamoja na busara, JK ana sifa nyingine isiyo na shaka kabisa! Hii ni ile ya ustahimilivu! Ustahimilivu wake ni too much to the extent ni rahisi ku-conclude kwamba ni udhaifu! JK ana sifa nyingine; sifa hii ndiyo inayowagharimu wana-CHADEMA! Mnamwa-undermine sana yule mzee kumbe yule mzee ni very smart katika ku-beat up external pressures! Hebu rejea mlivyopigwa(au umehakama CHADEMA??!!) changa la macho kwenye suala la katiba hivi karibuni pale akina Lissu walipoenda Ikulu! Kwa hiyo, kwa ujanja wake ule ule wote watatulizwa! Ukichanganya hayo yote; sifa za mtu kama huyo zinakuwa kutofanya maamuzi ya haraka; si kwamba ni slow learner, watu wa aina hii huwa hawayumbishwi na external pressures! Kashikashi anazokutana nazo JK ingekuwa ndo Mkapa; ingekuwa watu wengi hivi sasa wamefungwa na wengine kuuawa kuliko wale ambao inaonekana leo hii wameuawa kipindi cha JK! Mkapa alikuwa anatingishika sana na external pressure; wenyewe tunaita ni ukali; alikuwa hataki masihara kumbe ule nao ni udhaifu; defensive mechanism! likuwa hawawezi how to overcome pressure psychologically!
Kutokana na hayo, sina shaka kwamba JK atajaribu kuvuta vuta kidogo, na ikibidi EAC isife kwenye mikono yako! Na ukiona na yeye anahidhinisha kujitoa EAC leo; basi angekuwa mwingine angefanya hivyo miezi sita kabla! Lakini yote kwa yote; na sisi tusidakwe kati kati ya hii psychological torturing iliyoasisiwa na Kenyatta na kupata uungwaji mkono na akina Kagame ambao tayari waliyakuwa na yao nyoyoni! Hii ni psychological attack anayoifanya Kenyatta ili Tanzania tu-loose focus na kukurupuka kwa kuamini kwamba wenzetu wanatuacha! Wenyewe wanasema tunasuasua, kumbe wanafahamu kusuasua kwetu ni kwa ajili ya kulinda maslahi yetu! wanataka tufanye faster, kwahiyo lazima watushitue!
Bubu Msemaovyo, je jinsi yako ni sawa na hiyo avatar yako? Let me assume so! Je, unajisikiaje pale unapomtisha Boyfriend wako kwa kumwambia kwa ukali "kuanzia leo usinifuate fuate na wala simu usinipigie!" Halafu jamaa ndo kwanza anakuambia "safari njema mama!" Ulifanya yote ukidhani atatishika, na kwamba pale utakapoanza kuondoka ulitarajia atakushika mkono! Kutahamaki ndo kwanza jamaa anaingia kuoga! Hawa jamaa wanatarajia sisi tu-panic ili tuwashike mkono tuwaambie wasituache!
Ndugu zangu Watanzania,ni rai yangu kwamba tunapotengwa na majirani zetu,tutumie tukio hilo kujenga mshikamano mkubwa ndani ya nchi na kuondoa tofauti zetu.
Tukifanikiwa kujenga umoja huu wa familia ya Taifa letu,tutakuwa tumejenga ulinzi mkubwa wa Taifa dhidi ya majirani zetu wanaotutenga kwa sababu tumekataa kuwapa ardhi yetu ambayo walikuwa wakiitafuta kwa nguvu zao zote.
- Tofauti zetu katika masuala ya siasa zisitutenganishe bali zituunganishe na tukosoane kwa nia ya kujenga nchi.
- Tofauti zetu za kikabila zituweke pamoja kama ndugu wa Taifa moja.
- Tofauti zetu za kidini zitujengee mshikamano wa kupendana na kushikamana pamoja kila mtu akiheshimu dini ya jirani yake.
Hebu tujadili kwa uwazi;mimi nimeanza na wengine waendelee.
Ardhi yenyewe watanzania tunayojivunia imegubikwa na migogoro chungu nzima ya wakulima na wafugaji. Serikali imeshindwa hata kutengeneza mgawanyo mzuri wa ardhi kati ya wakulima na wafugaji matokeo yake ni migogoro kila kukicha. Miaka mitano ijayo tutaingia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe kugombea ardhi wakulima na wafugaji, hali ni mbaya.
Ni bora watanzania tungejikita katika KUSAFISHA NYUMBA YETU kuliko kuumizwa kichwa na hao jamaa wanaofanya mambo ambayo wanaona yanafaa kwa nchi zao na kutunyima sisi usingizi na kufanya tunayoona yanafaa kwa nchi yetu. Kama lengo la umoja wao wa mashaka ni ku FRUSTRATE Tanzania naona wametimiza maana frustration kila kona. Kuna watu saizi hadi wanasikiliza radio za Rwanda kwa frustration. Sisi tunaweza kuwashinda hawa kwa kujiimarisha kiuchumi watakuja wenyewe, bahati mbaya ndio hivyo hata kutumia rasilimali tumeshindwa
Marahaba mjukuu wangu Annael, hujambo!!Nakuheshimu. Shikamoo.
Mkuu jana nilijaribu kutafuta data kuhusu individual economies among EA Countries lakini nikaishia njiani. Lakini kama data ulizotoa ni sahihi; basi kuna kila sababu kwanini Kenya wameanza kuwa na hofu. Yaani Kenya's GDP USD 66.03 millions; Tanzania USD 58.4 millions! Hawa jamaa walikuwa wamenitupiga gap la kutisha!!Pitia attachment hapo chini inaonyesha uchumi wa nchi tano za EAC na muungano wao kabla na baada ya kauli ya Sita
Waziri wa East africa wa Tanzania Bwana Samwel Sita amekiri kuwa EAC iliyopo tayari tumeingia hasara kwani tumeshasusa baada ya dalili za kutengwa. Kauli hiyo inakwenda mbali kwa kuanza mashauriano ya muungano mwingine kati ya Burundi, DRC na Tanzania.
Makovu haya bado hayajapona, kwanini tusiangalie kwanza faida na hasara ambazo tayari zimetupata kwa kuishi ndani ya EAC na kushindwa kuendelea. Tukumbuke tunatoa michango, tuna wabunge wa EAC wanakula kodi za wananchi, ofisi, nk ambapo hakuna faida yeyote mlipa kodi amepata zaidi ya hasara.
Miungano hii isiwe njia ya kutafutia watu ajira za ubunge, ukurugenzi, ukatibu na uwaziri tu.
Uchumi wa nchi zote hizi tano na idadi ya watu pamoja na rasilimali ambazo kila nchi inazo ungetumiwa na wananchi wa nchi zote hizi tano wangefaidika sana kuliko viongozi ambao wengi wao wanataka madaraka na ajira za kisiasa.
Imefika wakati kuanza kutumia akili, maono, na werevu wa hali ya juu kuiamulia nchi na jamii badala ya kukurupuka kila mara.
Maamuzi ya kutumia matumbo, wizi, ufisadi na faida binafsi ndio yanatutumbukiza gizani kila mara. Mwaka 1977 umoja huu ulikufa na kuacha majeraha mengi ambayo miaka 36 sasa hayajapona mojawapo mafao ya wafanyakazi. Sijui na huu msambaratiko utaumiza wangapi, najua kwa uhakika wanasiasa wao lazima watapata keki yao, sie walala hoi waamka hoi ndio tutasoma namba.
Tujenge uchumi wetu, tuzidishe uhusiano mzuri na majirani zetu kuwavutia wafanyabiashara wao kufanya biashara na sisi. Kodi zetu na urasimu tuupunguze, ulinzi wa mali uongezwe, raia wakipenda kitu hakuna kiongozi anaweza kukataa. Tuonyeshe tunakitu cha kuwafanya watutake kuliko sisi kila siku kuwa na bakuli mbele.
Malighafi tunazo, bandari tunazo, watu tunao viongozi ndio hatuna kabisa.
Change has to begin with you and me.
Fue Fue