Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Nimekuwa nikisikiliza nukuu mbali mbali za wanasiasa na wanaharakati wenye kiu ya kutaka mabadiliko ya kisiasa, utawala na uchumi. Wengi wanapenda kutumia maneno "tutaendelea kupiga kelele mpaka kieleweke" au "tutaendelea kupiga kelele mpaka mmilika wa kagoda ajulikane".
Na hii siyo siri. Hata Dokta wangu, president wangu, Dr. Wilbroad Peter Slaa huwa mara kwa mara anatamka maneno haya.
Mimi siyapendi kwa sababu kuna msemo wa wahenga "kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji". Itafika mahali hata mtu anazungumza jambo la maana kuhusu serikali na watawala akapuuzwa kwa sababu watasema "anapiga kelele tu...hana lolote"
Wataalamu wa lugha naomba mtupe namna nzuri ya ku-phrase maneno hayo ili wanaharakati wetu wapate maneno sahihi yenye vionjo vya kuwafanya mafisadi washituke pale yanapotamkwa.
Diyelelwa?.
Na hii siyo siri. Hata Dokta wangu, president wangu, Dr. Wilbroad Peter Slaa huwa mara kwa mara anatamka maneno haya.
Mimi siyapendi kwa sababu kuna msemo wa wahenga "kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji". Itafika mahali hata mtu anazungumza jambo la maana kuhusu serikali na watawala akapuuzwa kwa sababu watasema "anapiga kelele tu...hana lolote"
Wataalamu wa lugha naomba mtupe namna nzuri ya ku-phrase maneno hayo ili wanaharakati wetu wapate maneno sahihi yenye vionjo vya kuwafanya mafisadi washituke pale yanapotamkwa.
Diyelelwa?.