Habari wadau!
Mimi nimekuwa mmoja wa watu wanaofuatilia kwa karibu siasa za Tanzania.Kutokana na ukaribu huo nimejikuta namiliki kadi za vyama mbali mbali na kujikuta nafikisha jumla ya kadi saba za vyama tofauti vya kisiasa.
Kadi yangu ya kwanza ilikuwa ya CHADEMA niliipata mwaka 2008 kupitia operation Sangara mkoani Mwanza na alinipa ndugu Zitto Kabwe.
Kadi yangu ya pili ilikuwa ya TLP ambayo nilipewa mh. Agostino Mrema ambapo siku hiyo ilikuwa kama utani vile na jamaa zangu na tukajikuta utani wetu ukiishia mtaa wa Jogoo,Magomeni katika ofisi ya TLP.
Kadi yangu ya tatu ni ya CUF ambayo niliipata kiutani utani tena mwaka 2013 ambapo tuliliona gari la ndugu Mtatilo likiwa sheli na yeye akiwa chini tukamfuata na baadae tukaishiwa kupewa kadi,Magengeni Bunju.
Kadi ya nne ni ya CCM hii tulikuwa tunabisha ni nani mwenyekiti wa CCM mtaani kwetu na mwisho tukajikuta tupo kwake na kupewa kadi.
Kadi ya tano ni ya ACT-Wazalendo,hii nilipewa tu.
Kadi ya sita ni ya UDP.
Kadi ya saba ni ya kupewa ya NCCR-Mageuzi.
Mimi nimekuwa mmoja wa watu wanaofuatilia kwa karibu siasa za Tanzania.Kutokana na ukaribu huo nimejikuta namiliki kadi za vyama mbali mbali na kujikuta nafikisha jumla ya kadi saba za vyama tofauti vya kisiasa.
Kadi yangu ya kwanza ilikuwa ya CHADEMA niliipata mwaka 2008 kupitia operation Sangara mkoani Mwanza na alinipa ndugu Zitto Kabwe.
Kadi yangu ya pili ilikuwa ya TLP ambayo nilipewa mh. Agostino Mrema ambapo siku hiyo ilikuwa kama utani vile na jamaa zangu na tukajikuta utani wetu ukiishia mtaa wa Jogoo,Magomeni katika ofisi ya TLP.
Kadi yangu ya tatu ni ya CUF ambayo niliipata kiutani utani tena mwaka 2013 ambapo tuliliona gari la ndugu Mtatilo likiwa sheli na yeye akiwa chini tukamfuata na baadae tukaishiwa kupewa kadi,Magengeni Bunju.
Kadi ya nne ni ya CCM hii tulikuwa tunabisha ni nani mwenyekiti wa CCM mtaani kwetu na mwisho tukajikuta tupo kwake na kupewa kadi.
Kadi ya tano ni ya ACT-Wazalendo,hii nilipewa tu.
Kadi ya sita ni ya UDP.
Kadi ya saba ni ya kupewa ya NCCR-Mageuzi.