Uamuzi wa kiume huo!! Bravo!!Ndio maamuzi niliayoamua na hapa nafanya mpango kukusanya vyangu huku nilipo, najua life litazonga ila kipimo cha akili ni ugumu wa maisha, ipo siku nitatoka tu. Siwezi kuwa mtumwa kamwe.
Nilisimamia mitihani ya kidato cha pili, mtihani umeisha hatukulipwa hadi jana, jana watu wanalipwa nakuja kufatilia pesa yangu naambiwa jina langu halipo, leo nimuone afisa elimu, namuona leo anasema hakuna fungu nilisahaulika niandike Barua kufungua madai nitalipwa kwa OC (other chages) mafungu ya mkurugenzi.
Tafsiri yake ni kuwa limeshakuwa deni tayari hili, jasho langu, kila siku nilitumia tsh 8000 kwenda na kurudi kusimamia mitihani kwa siku saba. Kuja hapa halimashauri kutoka nnakoishi nakodi pikipiki elf 8 kwenda na kurudi kila siku, hapo bado kula, Nimetumia pesa eti leo nidai tena. HAPANA
Tangu nimeanza kazi nna miaka mitatu sasa ninaidai serikali, alafu leo niongeze tena kudai?
Kwa dhati ya moyo wangu nimeamua na sirudi nyuma, nimeachana na ualimu Rasmi, siwez kuwa mtumwa kwa haki yangu. Nita fight, nitatoka, sio wote wenye kazi ndio wanamudu maisha .
Hongera sana sana, mimi niliacha zamani kidogo, na niliweka thread miaka ya baadae hapa jamvini na nilitoa sababu, wengi walinipinga lakini kweli sijawahi kujuta! Yalikua maamuzi ya "kijinga" kwa kipindi kile ila nashukuru Mungu naendelea mbele
Naomba link yako y thread yako mkuu
mkuu masuala yote hayo tunasababisha walimu wenyewe hongera! kuna halmashauri nyingine walimu hawakulipwa hela ya semina, wakaenda kusimamia hivyo hivyo kigumu wakaahidiwa watapewa hela mwisho wa kazi, siku wamemaliza jamaa wanakusanya mitihani wanadai "mtaletewa pesa kwenye vituo vyenu" imagine mtu umeenda kukaa sehemu zaidi ya wiki ukitegemea utalipwa! mbaya zaidi siku ya malipo unaambiwa ufuate hela halmashauri tena kwa gharama zako!>>>>>>> but walimu hao wala hawalalamiki... mimi nadhani ukipata nafasi ya kuchomoka ni bora kuliko unyonyaji huu wa wazi
vijana wanachezea maisha hawa, huku mtaani ni kugumu sana kabla ya kuchukua maamuzi hayo ungeomba kwanza ushauri ili watu tukupe uhalisia wa huku unakotaka kuja. huku kugumu mkuu pambana huko huko. unaweza kuwa mjasiliamali huku bado ukawa mwalimu kwa sababu mwl leo anakopeshwa hadi milion 15 kwa makato ya 5 yrs
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...nilikimbia-ualimu-kuepuka-matatizo-print.htmlNaomba link yako y thread yako mkuu
Ndio maamuzi niliayoamua na hapa nafanya mpango kukusanya vyangu huku nilipo, najua life litazonga ila kipimo cha akili ni ugumu wa maisha, ipo siku nitatoka tu. Siwezi kuwa mtumwa kamwe.
Nilisimamia mitihani ya kidato cha pili, mtihani umeisha hatukulipwa hadi jana, jana watu wanalipwa nakuja kufatilia pesa yangu naambiwa jina langu halipo, leo nimuone afisa elimu, namuona leo anasema hakuna fungu nilisahaulika niandike Barua kufungua madai nitalipwa kwa OC (other chages) mafungu ya mkurugenzi.
Tafsiri yake ni kuwa limeshakuwa deni tayari hili, jasho langu, kila siku nilitumia tsh 8000 kwenda na kurudi kusimamia mitihani kwa siku saba. Kuja hapa halimashauri kutoka nnakoishi nakodi pikipiki elf 8 kwenda na kurudi kila siku, hapo bado kula, Nimetumia pesa eti leo nidai tena. HAPANA
Tangu nimeanza kazi nna miaka mitatu sasa ninaidai serikali, alafu leo niongeze tena kudai?
Kwa dhati ya moyo wangu nimeamua na sirudi nyuma, nimeachana na ualimu Rasmi, siwez kuwa mtumwa kwa haki yangu. Nita fight, nitatoka, sio wote wenye kazi ndio wanamudu maisha .