Mashakamnyaka
New Member
- Jun 25, 2021
- 1
- 5
Habari zenu ndugu zangu.
Nakuja kwenu na Id mpya ili niweze kuwa muwazi kwenu nipate msaada. Naona karma inaninyemelea na sielewi nifanye nini ndugu zangu.
Mimi ni kijana wa miaka 31. Sijaoa lakini nimekuwa na girflriend wengi kwa wakati mmoja bila wao kujuana.
Shida yangu ni hii: Katika wasichana wote niliowahi kuwa nao, kuna huyu msichana A. Kwa kweli tumekaa naye kwenye mahusiano zaidi ya miaka 5. Tangu nikiwa chuo. Msichana huyu sijapishana naye umri sana. Nimemzidi kwa miezi kadhaa. Ila amekuwa akiniheshimu kwa muda mrefu, akinijali tangu sina kazi hadi sasa.
Ila niseme ukweli ndugu zangu. Huyu msichana kwanza mguu wake mmoja ni mfupi mwingine ni mrefu, hivyo anakuwa kama anachechemea fulani. Licha ya hayo mapungufu ya kimaumbile, ni mtu mwenye elimu yake, mzuri sana (kwa macho yangu), hanitegemei kwa chochote hadi pale mimi ninapoamua kumnunulia kitu au kumtoa out. Otherwise hata mimi muda mwingine ananipiga tafu.
Shida ni kwamba sasa nimepata mtu mwingine ambaye nahisi tunaweza kuendana zaidi ya A. Ingawa simjui vema msichana huyu maana ni mwanafunzi wa chuo ambaye nimemzidi miaka zaidi ya 7. Tupo mikoa tofauti. Yeye ni tegemezi kwangu kwa kila kitu. Na kiukweli mara nyingi tunagombana sana na tumeshaachana mara kwa mara sababu ya huyu msichana A ambaye naye imefikia hatua kuwa sasa nichague jambo moja. Kumuacha ama kuendelea naye pasipo mimi kuwa na wasichana wengine. Jambo ambalo kwangu ni gumu sana.
Nimejaribu mara kadhaa kuongea na A na at the same time nakuwa na B kwa simu. Jambo ambalo A amekuwa mkali na sasa ninashindwa kuwa huru hata kuongea na B.
Kiukweli B naona ni msichana mdogo na pia kabila letu ni moja hivyo ninapata amani sana kuwa nitaweza kuwa na huyu binti kuliko kuwa na A. B anamaliza masomo mwaka huu na tunategemea mwakani tuanze safari ya kukaa karibu ili kujuana na hàtimaye tufunge ndoa.
Migogoro hii kwangu imekuwa kero na nimemtamkia maneno mabaya sana A ambaye amekata tamaa nami kabisa. Hanipigii tena simu na kiukweli najihisi kama nipo mwenyewe inspotokea ninapata changamoto fulani.
Naombeni ushauri wenu wadau. Je nipo sawa ama nimeyumba?
Nakuja kwenu na Id mpya ili niweze kuwa muwazi kwenu nipate msaada. Naona karma inaninyemelea na sielewi nifanye nini ndugu zangu.
Mimi ni kijana wa miaka 31. Sijaoa lakini nimekuwa na girflriend wengi kwa wakati mmoja bila wao kujuana.
Shida yangu ni hii: Katika wasichana wote niliowahi kuwa nao, kuna huyu msichana A. Kwa kweli tumekaa naye kwenye mahusiano zaidi ya miaka 5. Tangu nikiwa chuo. Msichana huyu sijapishana naye umri sana. Nimemzidi kwa miezi kadhaa. Ila amekuwa akiniheshimu kwa muda mrefu, akinijali tangu sina kazi hadi sasa.
Ila niseme ukweli ndugu zangu. Huyu msichana kwanza mguu wake mmoja ni mfupi mwingine ni mrefu, hivyo anakuwa kama anachechemea fulani. Licha ya hayo mapungufu ya kimaumbile, ni mtu mwenye elimu yake, mzuri sana (kwa macho yangu), hanitegemei kwa chochote hadi pale mimi ninapoamua kumnunulia kitu au kumtoa out. Otherwise hata mimi muda mwingine ananipiga tafu.
Shida ni kwamba sasa nimepata mtu mwingine ambaye nahisi tunaweza kuendana zaidi ya A. Ingawa simjui vema msichana huyu maana ni mwanafunzi wa chuo ambaye nimemzidi miaka zaidi ya 7. Tupo mikoa tofauti. Yeye ni tegemezi kwangu kwa kila kitu. Na kiukweli mara nyingi tunagombana sana na tumeshaachana mara kwa mara sababu ya huyu msichana A ambaye naye imefikia hatua kuwa sasa nichague jambo moja. Kumuacha ama kuendelea naye pasipo mimi kuwa na wasichana wengine. Jambo ambalo kwangu ni gumu sana.
Nimejaribu mara kadhaa kuongea na A na at the same time nakuwa na B kwa simu. Jambo ambalo A amekuwa mkali na sasa ninashindwa kuwa huru hata kuongea na B.
Kiukweli B naona ni msichana mdogo na pia kabila letu ni moja hivyo ninapata amani sana kuwa nitaweza kuwa na huyu binti kuliko kuwa na A. B anamaliza masomo mwaka huu na tunategemea mwakani tuanze safari ya kukaa karibu ili kujuana na hàtimaye tufunge ndoa.
Migogoro hii kwangu imekuwa kero na nimemtamkia maneno mabaya sana A ambaye amekata tamaa nami kabisa. Hanipigii tena simu na kiukweli najihisi kama nipo mwenyewe inspotokea ninapata changamoto fulani.
Naombeni ushauri wenu wadau. Je nipo sawa ama nimeyumba?