Nina Shaka na mwaka 2015, tuweke akiba

Nina Shaka na mwaka 2015, tuweke akiba

Muite

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2013
Posts
3,192
Reaction score
7,112
Wana JF wenzangu kutokana na hali ya kisiasa inavyobadilika kila kukicha ninaona picha fulani ya maisha na huduma za kijamii kuwa ngumu kwa wananchi wa kipato cha kawaida kwa mwaka ujao. Mambo matatu yanayosababisha mashaka haya ni:-
1. Mvutano wa katiba mpya
2. Uchaguzi mkuu.
3. Wahisani kusitisha misaada
Nadhani sina haja kuyaelezea hayo yote matatu kuwa yanawezaje kuyumbisha hali ya maisha ya wananchi.

Ushauri wangu ni kwamba ifikapo mwk 2015 ni vema katika familia zetu tukaandaa utaratibu wakuweka Akiba ya Chakula cha kutosha ndani. Na sio chakula tu ila hata Akiba ya Fedha ya dharura. Ingawa tunashauriwa kuweka fedha Bank ila ni vema kuwe na akiba yako fulani kwani sector za Kibenki hazitabiriki muda wote. Mfano migomo nk
 
umesahau na akiba ya vidonge vya maradhi yote tena uweke dozi ya ukoo wako wote, maana hiyo ndio bidhaa muhimu kuliko zote na ishaanza kupotea kabla ya 2015, sijui linawezekana hilo?
 
Wacha kutisha watu kijinga, wewe unajijuwa kuwa utafika hiyo 2015?
 
Anyways suala la kujiwekea akiba ni muhimu sana kila wakati sio la msimu la siivyo utaishia kulalamika tuu kila siku.
 
hakuna anayeombea vurugu ila hao viongozi ndiyo wanataka kutuletea balaaa.
 
Mbona tunaanza kutishana tena jamani, sasa huyo anaetaka tuanze na mazoezi ya kungfu, judo,kareti na mieleka ana maana gani
 
Msihau na kukodi kajumba pale isibania,kisumu na hata mombasa.
hali ngumu sana.
 
Tusisahau na kuanza mazoezi ya kung-fu au ya kutafuta pumzi ili mbio zikusaidie inapobidi.

mkuu mi zamani nimeashaanza hizi mambo za jeti lee na van damme,bado za bolt mapema mwakani,ikifika tu steji ya mabaka kuingia uraiani nitakuwa fresh,ngoma dar-lindi-mtwara-msumbiji-nyumbani S.A
 
Wacha kutisha watu kijinga, wewe unajijuwa kuwa utafika hiyo 2015?

At least kila binadamu ana matarajio ya kuishi miaka mingi duniani.
Hata yeye amejielezea kama binadamu anaeishi mwenye sifa ya kuwa optimistic.
 
Wana JF wenzangu kutokana na hali ya kisiasa inavyobadilika kila kukicha ninaona picha fulani ya maisha na huduma za kijamii kuwa ngumu kwa wananchi wa kipato cha kawaida kwa mwaka ujao. Mambo matatu yanayosababisha mashaka haya ni:-
1. Mvutano wa katiba mpya
2. Uchaguzi mkuu.
3. Wahisani kusitisha misaada
Nadhani sina haja kuyaelezea hayo yote matatu kuwa yanawezaje kuyumbisha hali ya maisha ya wananchi.

Ushauri wangu ni kwamba ifikapo mwk 2015 ni vema katika familia zetu tukaandaa utaratibu wakuweka Akiba ya Chakula cha kutosha ndani. Na sio chakula tu ila hata Akiba ya Fedha ya dharura. Ingawa tunashauriwa kuweka fedha Bank ila ni vema kuwe na akiba yako fulani kwani sector za Kibenki hazitabiriki muda wote. Mfano migomo nk

Watu wanaweza wakakuchukulia poa kumbe ndo ushawaambia tayari.
Yamkni maneno yako yanaweza kuwa yana ukweli kwa kiasi fulani cha kutilia maanani
 
At least kila binadamu ana matarajio ya kuishi miaka mingi duniani.
Hata yeye amejielezea kama binadamu anaeishi mwenye sifa ya kuwa optimistic.

Matarajio na kujuwa ni vitu tofauti.

Hakuna ajuwae la kesho itakuwa 2015?

Kuwaambia watu leo warundike vyakula na fedha za akiba kwa hofu yako ya mwaka 2015 ndio kuwa "optimistic"?

Amma kweli.
 
Back
Top Bottom