Nina Makosa kweli hapa?? Nishauri tafadhari!

Nina Makosa kweli hapa?? Nishauri tafadhari!

Kaka alikuweka akiba asee, so fanya yako hapo hajakupenda kacheka wee ndo mbadala wake kwa sasa kuziba pengo la kipenz wake
 
Achana nae na ikiwezekana namba yake
Iblock





Finish!!!!!!!!!!!
 
1. Mwanadada hana kosa lolote kwani mwanzoni alikuwa na sababu ya kukataa mahusiano nawe kwa kuwa alikuwa na mtu. (Inaonekana ni mwaminifu kwa mahusiano anayokuwa nayo).

2. Hakuna mahali ambapo imeandikwa kuwa mwanamke hawezi kuanzisha mahusiano na mwanaume.
Watu wengi hawajui kuwa wanawake pia hutongoza isipokuwa wanaume wengi hushindwa kutambua lugha wazitumiazo.
Huyo wako katumia lugha inayoeleweka ambayo hata wewe ungeliweza kuitumia pia.

3. Kinachokushangaza ni kipi mkuu, mbona wanaume nasi huwa tunafanya kama hivyo mara kibao kurudi nyuma na kukagua zile sehemu tulizopita pindi tunapotoswa tulipo.
Inavyoonekana huyo dada alikupenda awali na anachofanya sasa ni kukupa nafasi kabla hajaamua kumove on.
Kama unaona mtoto ni kikwazo mueleze kwa ufupi pasipo kumuumiza roho naamini atakuelewa.

NB:

Nimeshangazwa na comments nyingi za wadada humu ndani wanaomnanga mdada mwenzao.

Nimehisi ni wanafiki kwa kuwa wanawake wengi sana hufanya kama alivyofanya huyo mwanamke.

Nimekupenda bure
 
I concur with watu8 ila nina nyongeza kidogo:

1. hayo yenu yalishatokea na mimi nimejifunza jambo hapa...to all young men and women out there in relationships...paka wa jirani hakaribishwi jikoni. mmekutana tu na mtu amesema anakupenda and all that isiwe sababu ya wewe kumuamini kiasi cha kumruhusu hadi ajipakulie na kujiwekea akiba (mimba). tuwe werevu kama nyoka...anauma na kurudi nyuma kwanza akihakikisha amedhuru ndipo hujongea kula.

sisi binadamu wenye utashi tunashindwa kujifunza hili..tunaenda kichwa kichwa kisa amekutamkia anakupenda. anyway...am not judging kwa kuwa mdada amepewa mimba hilo lishatokea na hatujui (and maybe we wil never know) ilikuwaje..but iwe funzo kwetu ambao bado.


mwisho ni kwako mtoa mada..ukweli ni hukuwa na nia yeyote kwa huyo binti kubali hili...ulitaka kumega na kusepa! so, kistaarabu tu usimuumize zaidi muache aende kwa amani alee mwanaye baadaye atakuja kumpata atakayempenda na ua lake.


namba 3. ya watu8 ni very debatable ila kwa maudhui ya kutochakachua thread ya watu naomba niachie hapa.
alamsik.
 
Last edited by a moderator:
!
!
2010 na leo ni 2014......no way. Mtoto ana miezi sita,na baba wa mtoto kamkataa mtoto. Kwa nini baba kamkataa mtoto?
kuna maswali bado kiaina.
Kuhusu kukupenda kwa sababu fulani ni kawaida...mfano unaweza pendwa kwa umbile lako au jinsi unavyoongea au hata pesa pia muda fulani.
Angalia kama unaweza hiyo gharama ya kuwa naye. Jibu unalo mwenyewe
 
how do u fell about her????kam unampnda muoe,bt kam u feel nothing 4 her,muache kuliko kuoa m2 ambae huna fellings nae,ndoa haitadumu
 
mambo vp ushapata uahaur

Ushauri umepatikana wa aina tatu!
1. Wengi wananishauri nimpige tu chini
2. Kundi lingine wanashauri nimpe nafasi
3. Baadhi wameniachia mwenyewe !
Nikichambua zaidi napata picha ya kwamba yawezekana kweli niliwekwa kwenye reserve list na huyu binti na kama mambo yake yangemuendea vizuri basi asingekuwa na time na mimi, hivyo basi, kwa kuzingatia ushauri wa watu wengi walionishauri hapa, mimi Thegame, bila kulazimishwa na mtu yeyote, nimeamua kuachana naye rasmi.
 
kama ulimpenda kweli,mkubali tu mwenzio yupo njia panda bana...!nini hamu ikuishe kisa ana mtoto mkuu!
 
Hapo unataka uachiwe majukumu tu broda,hapo hajakupenda amekutaka ili umtimizie mahitaji yake yeye na mwanae,mwambie atafute kituo kingine broda!
 
Wewe ulimtamani tu,

Angekubali kukupa game sidhani kama ungekuwa naye mapaka sasa.
 
mtoa mada hata wew umezaliwa na screpa.ebu badilisha kauli hyo ndiy 2tiririke..

Mtoa mada ana haki ya kumwita huyo binti screpa kwani alipotongozwa alimtolea nje, na sasa amezalishwa,anatafuta mteremko kwa mshikaji! Mama mzazi hawezi kuitwa screpa.! Majibu unayo nadhani juu ya hili!
 
mmmhh... sometimes kuwa single ni raha!
 
Achana nae na ikiwezekana namba yake
Iblock

Finish!!!!!!!!!!!

utajisikiaje kama ni ww ndio unafanyiwa hivyo na huna mahali pengine pa kwenda?

mwanamke mwenzio huyo endapo atatupa mtoto utakuwa wa kwanza kwenda kumlaumu!

mshawishini mtoa mada amsaidie mwanadada mwenzenu kulea huyo mtoto.. hilo ni taifa la kesho..
 
Hapa unazungumzia manini hayo?
Na huyo mtoto unayemwambia amzalishe kisha aje amchukue ina maana huyo Bint amekuwa ni mtambo wa kufyatulia watoto? Kama yanaboa sana mnayazalisha ya nini? Jifunze kuheshimu wanawake.
Huyo Bint amezaa mnampa majina yote mabaya,angetoa mimba ndio angeonekana msichana anayejua kujitunza!!!

sio kwamba hatuwaheshim wanawake ila kuna baadhi yenu wanapelekea mdharaurike. Hebu fikiria umemkataa mwanaume umesema una mtu wako halafu baadae umetoswa unakuja tena kwa huyo uliyemkataa ili umtwishe mzigo wako, vp inakuja hapo?? Tatizo mnakimbilia kupokea mimba kabla hata hujausoma msimamo wa mwenzako
 
@watu8 kibofyo cha like kimepotea ila nakupa hata draw ya man u iwe zawadi yako.Unajua kuongea kwa kuangalia kaka sio kushtuliwa tu.
I salute you..

"Nlikuwepo":bolt:
 
Nionavyo miye huyo mwanamke pamoja na kuwa mwamonifu hapo mwanzo kwa mpenzi wake na kutoswa baada ya kuzalishwa kuna uwezekano mkubwa pia akawa mwaminifu kwako na hasa pale atakapoona wewe umemkubali yeye na mtoto wake
Kuna kitu amejifunza kwa huyo aliyemtosa
 
cha msingi hem angalia moyo wako! kama bdo unampenda mi sion kama kunattz hapo! cz unawez mkataa mtt huyo thn ukaja kuoa na ukakosa mtt kbsaa! mwsho wa ck ikawa bora ungelea huyo japo c wako! akikuwa atajua we baba ake!
 
Back
Top Bottom