Nina Makosa kweli hapa?? Nishauri tafadhari!

Nina Makosa kweli hapa?? Nishauri tafadhari!

Thegame

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2011
Posts
2,273
Reaction score
2,402
Wana MMU, salamu kwenu!
Hii ni thread yangu ya kwanza kwenye kwenye hili jukwaa, imenilazimu kuja kuomba ushauri kwa hili lililonikuta. Issue iko hivi,
Mwaka 2010 nilikutana na binti mrembo mmoja hapa mtaani kwetu, alikuja kukaa kwa mama yake Mdogo hapa mtaani. Binti alikuwa mrembo kweli kweli, basi kama ambavyo wanaume tulivyoumbwa nikaomba mchezo, akazingua! Nikaimba nyimbo zote za kinyakyusa lkn binti bado akadai ana boyfriend wake na anampenda sana. Nikaona isiwe shida nikaachana nae baadae akaondoka mtaani akarudi kwao mwanza na mawasiliano yakafa!
January mwaka huu siku moja nikiwa njiani natoka ofisini simu yangu ikaita, kupokea ni yule mrembo! Akaanza maneno, umeoa, nikamjibu bado! Hapo ndipo tulipoanza tena mawasiliano, nikashangaa binti mwenyewe ndiye anataka uhusiano! Baada ya kama wiki moja ya mahusiano ya kwenye simu, tukiwa tumepanga tuonanie Mkoa fulani, akaniuliza swali kama nitaweza kuoa mwanamke mwenye mtoto??
Nikamuuliza kwani una mtoto?? Akajibu ndio, wa umri wa miezi sita na aliyempa mimba kamkataa! Baada ya kunieleza hivyo nikashangaa ule Upendo wote niliokua nao juu yake ukaisha ghafla! Kichwani kwangu nikawakuta nawaza huyu binti anajisogeza kwangu Kwasababu yuko matatizoni, hasa financially! Anataka anipe majukumu ya kumlelea mtoto!
Baada ya kuwaza hivyo nikampiga chini! Tatizo eti kila siku ananipigia simu analia, eti ananipenda! Wadau hapa mnaona Upendo kweli hapa???
Au nakosea jamani, hebu niambieni, nimuoe au nimpotezee??
 
Mwanamke aliyezaa c screpa futa kwnz hyo kauli!lkn pia jiulize km kweli unamhitaji kwasasa?kabla ujatumbukia kwenye hilo penzi!
 
Kumbe mwanamke aliyezaa ni screpa?..... kwa hiyo mama yangu screpa!!!!! banghead::::::banghead:::::
 
Mwanamke aliyezaa c screpa futa kwnz hyo kauli!lkn pia jiulize km kweli unamhitaji kwasasa?kabla ujatumbukia kwenye hilo penzi!

Uko sahihi, mwanamke aliyezaa sio screpa! Maana yangu ni hii, nilimu-approach akiwa hana mtoto, akatoa nje! Na nakiri kwamba angenikubali wakati ule ninge muoa, lkn sasa watu wameshakula wameshiba pale, na mtoto wamemzalisha! Baada ya kutendwa ndio aje anikubali??
 
Acha ubwege basi akaolewe na aliye mp mimba yaani hata usidhubutu huyo analia na shida zake kwanini asiolewe na baba mtoto?!
 
mtoa mada hata wew umezaliwa na screpa.ebu badilisha kauli hyo ndiy 2tiririke..
 
Acha ubwege basi akaolewe na aliye mp mimba yaani hata usidhubutu huyo analia na shida zake kwanini asiolewe na baba mtoto?!

Hicho ndio nilicho waza! Shida zimemlemea!
 
Hello kwanza napenda kukwambia tatizo hilo jibu lipo kwako, kuzaa sio issue kuna watu wametumika mbaya na hawaja zaa lakini wamepoteza mbaya pima mapenzi yako kama yapo nae nenda nae sawa mwombe mungu atawabariki
 
Wew kama una uwezo msaidia kama rafiki yako ni sio huanze kuhudumia kam mke wanawak wajinga sana atakufanyia ktu baadae utajuta
Unaeza leo mtot na mama kama mpenz then ltr mchiz anamit nae anamuomb msamah warudian wamlee mtot..demu anakukimbia.hapo hujapendw kaka...kuw macho
 
Hawa ndio walivyo mwanzon nyodo nyingi yakizalishwa tu yanaanza kukumbuka mwanzo. Hapo ukimuona anakuganda msubir mtoto akue na ww mtandike mimba nyingne halafu mtose ila mtoto uje umchukue na akome ***** yanaboa sana haya
 
Ukiamua kuishi na mtu mwenye mtoto, ukubali changamoto nyingi.... sisemi hivyo kuwananga wadada/wakaka waliozaa kabla/nje ya ndoa, nasema tu kwa sababu zipo changamoto, hasa kihisia, kama ni mtu asiyetulia, utaumizwa sana hisia zako.... you better weigh pros and cons before jumping the broom buddy!!!
 
^^
Mambo mawili yako wazi hapo,
Moja, wewe unaongozwa na kumtamani wala sio kumpenda. Na nia yako ilikuwa atakapokurudia umtumie na kila mmoja aende zake!
Mbili,
Mwanamke anatafuta matunzo tu ya mtoto. Utakapomkubali au yeyote awae yule atakapomkubali awe tayari ama kupendwa kupita kiasi au kuachwa shida itakapoisha.
SIONI KUPENDANA BAINA YENU
^^
 
  • Thanks
Reactions: RR
Alikuwa wapi mwanzo yamemshinda ndo anajua anakupenda??????, hafai huyo anatafuta kwa kuponea shida zake.
 
Hawa ndio walivyo mwanzon nyodo nyingi yakizalishwa tu yanaanza kukumbuka mwanzo. Hapo ukimuona anakuganda msubir mtoto akue na ww mtandike mimba nyingne halafu mtose ila mtoto uje umchukue na akome ***** yanaboa sana haya
Hapa unazungumzia manini hayo?
Na huyo mtoto unayemwambia amzalishe kisha aje amchukue ina maana huyo Bint amekuwa ni mtambo wa kufyatulia watoto? Kama yanaboa sana mnayazalisha ya nini? Jifunze kuheshimu wanawake.
Huyo Bint amezaa mnampa majina yote mabaya,angetoa mimba ndio angeonekana msichana anayejua kujitunza!!!
 
1. Mwanadada hana kosa lolote kwani mwanzoni alikuwa na sababu ya kukataa mahusiano nawe kwa kuwa alikuwa na mtu. (Inaonekana ni mwaminifu kwa mahusiano anayokuwa nayo).

2. Hakuna mahali ambapo imeandikwa kuwa mwanamke hawezi kuanzisha mahusiano na mwanaume.
Watu wengi hawajui kuwa wanawake pia hutongoza isipokuwa wanaume wengi hushindwa kutambua lugha wazitumiazo.
Huyo wako katumia lugha inayoeleweka ambayo hata wewe ungeliweza kuitumia pia.

3. Kinachokushangaza ni kipi mkuu, mbona wanaume nasi huwa tunafanya kama hivyo mara kibao kurudi nyuma na kukagua zile sehemu tulizopita pindi tunapotoswa tulipo.
Inavyoonekana huyo dada alikupenda awali na anachofanya sasa ni kukupa nafasi kabla hajaamua kumove on.
Kama unaona mtoto ni kikwazo mueleze kwa ufupi pasipo kumuumiza roho naamini atakuelewa.

NB:

Nimeshangazwa na comments nyingi za wadada humu ndani wanaomnanga mdada mwenzao.

Nimehisi ni wanafiki kwa kuwa wanawake wengi sana hufanya kama alivyofanya huyo mwanamke.
 
Back
Top Bottom