MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,232
- 22,314
Wakuu namshukuru Mungu kwa hii pumzi na kwa riziki zake. Mimi ndugu yenu siku za hivi karibuni nimeona ni muda muafaka wa kuanzisha chanzo kingine cha mapato ila bado sijafanya maamuzi kamili. Nimekuwa nikiwaza sana nifanye biashara gani tofauti na ninayofanya kwa sasa ndo nikapata mawazo mawili kulingana na mtaji nilio nao.
Wazo la kwanza ninataka nifungue sehemu ya kuuza fabrics (materials za kushonea). Na pia niweke cherehani kama 3 za mafundi hapo nitakapokuwa nauzia fabrics. Wazo la pili ni kufungua duka la kuuza pombe na vinywaji vingine (LIQUOR STORE). Hizi biashara zote mbili kwa tathmini yangu binafsi ninaona yoyote nitakayochagua kuanza nayo nitaimudu. Mji niliopo ni mkubwa na ni halmashauri ya manispaa.
Karibuni tushauriane. Yawezekana huu uzi ukasaidia mtu mwingine pia.
Wazo la kwanza ninataka nifungue sehemu ya kuuza fabrics (materials za kushonea). Na pia niweke cherehani kama 3 za mafundi hapo nitakapokuwa nauzia fabrics. Wazo la pili ni kufungua duka la kuuza pombe na vinywaji vingine (LIQUOR STORE). Hizi biashara zote mbili kwa tathmini yangu binafsi ninaona yoyote nitakayochagua kuanza nayo nitaimudu. Mji niliopo ni mkubwa na ni halmashauri ya manispaa.
Karibuni tushauriane. Yawezekana huu uzi ukasaidia mtu mwingine pia.