Hallelujah YESU Kristo ni Mungu, ndani ya dakika chache umemkiri YESU kwa kulisoma neno lake.
Hapo ndipo mnapo shindwa akili na wakristo
Wewe hutaki kulifuata neno lake unalifuata neno la mchungaji wako , hapo ndiyo unapomsaliti Yesu
Yesu anasemaje katika Injili
Yohana 17:3 imeandikwa hivi –
…uzima wa milele ndiyo huu wakujue Mungu wa pekee na Yesu uliyemtuma.
Katika Aya hii Yesu anasema kwamba ili kupata uzima lazima tumjue kwanza Mungu wa pekee na umjue Yesu Kristo aliyetumwa na Mungu, hapa Yesu hasemi lolote kuhusu yeye kuwa nafasi ya pili ya Mungu ila anakiri wazi yeye ametumwa na Mungu mmoja wa pekee.
Luka 2:40 imeandikwa hivi: -
Yule mtoto akakua akaongezeka nguvu amejaa hekima na neema ya Mungu ilikua juu yake.
Katika Aya hii tunaambiwa kwamba Yesu alijaa hekima na neema ya Mungu. Tahadhari ufikirie vizuri kwa makini sababu hapa inayonyesha kwamba bila ya Mungu kumpa neema Yesu asingelikuwa na hekima hii inaonyesha wazi Yesu ni kiumbe aliyeteuliwa na Mungu na hii ni kawaida yake Mwenyezi Mungu kwa Mitume na Manabii wake kuwapa neema na hekima.
Yohana 13:13 imeandikwa hivi: - Nanyi mwaniita Mwalimu na Bwana nanyi mwasema vema maana ndivyo nilivyo. Maneno hayo yatueleza wazi kwamba alikuwa anajua wazi kwamba yeye ni Mwalimu na Bwana ndiyo maana anawasifu wanafunzi wake, NANYI MWASEMA VEMA.