nimwelewe vipi?

sijui kama umeshaona rangi sawasawa, huyo ni muuaji mzoefu, hata wewe atakuua.
Kimbia mbali ili ujiepushe naye, wala usiutamani uzuri alionao.
 
Mmmh! Pole sana ndugu yangu!
Mpende akupendaye( sijui nani aliisema hii).
Kaka hapo utaumiza moyo bure na utapoteza nguvu, mda na mafanikio ambayo umehangaika nayo muda wote kwa kipanga kama huyo !! huyo anaonyesha ni kiruka njia mzoefu hawezi kubanwa kwenye ndoa bana!
Cha msingi we piga moyo konde endelea mbele kama Mungu amekupangia utapata mwingine bila ubishi, wala hali ambayo we unadhani kwamba itakuwa kizuizi!!
We mwanaume bana!!
 
mmh jamani watu wanapata tru love wanachezea, na mtoto analelewa kweli wanawake wengine cjui wanawaza nini ili tusimhukumu pengine mimba ya kwanza alishasemwa sana kwao kuzaa bila ndoa hivyo akaoogopa wazazi kurudia kosa kwa kua limeshatokea jaribu kuongea nae nadhani utagundua nini kilimsibu kutoa mimba then mkielewana jaribuni kutumia kinga, kiukweli mapenzi tunapenda lakini kuzaa nje ya ndoa kwa mtoto wa kike ni fedheha home haytuna jinsi tukishabeba mimba yatupasa kuzaa tu ila kwa wenzetu wanaume kwao ni urijali kupata mtoto kabla ya ndoa, life is not fair
 
That woman is a killer. Achana nae! wapi wengi wenye akili timamu.

Kabisa. Aachane nayr haraka sana. Unawezekana kabisa mimba aliyotoa sio ya jamaa yetu.

Cha muhimu ndugu yangu zingatia kazi na Mungu atakuonyesha mwingine. Huyu hakufai kabisa. Ni kawaida kwen maisha
 
Huyo alikuwa ana KUCHEZEA tu, Mungu atakupa mwingine ambaye mtaISHI naye mkiCHEZA pamoja kwa uzuri.
 
kwanza pole sana mkuu,pili mbona kutoa mimba ni kama fashion karne hii? Sio kitu cha kushangaa saana ila wengi wanatoa kwa sababu ya matatizo ya aidha aliyempa hiyo mimba ameikataa au sababu nyingine nyingine zinazojulikana. Cha kujiuliza ni kwamba iweje aende kuitoa hiyo mimba ilhali wewe ulishakubali kuihudumia?
Kuna kitu kimefichika hapo,mtafute na ujaribu kuongea naye vizuri na kama majibu yake yatakuridhisha basi uamuzi ni wako umrudishe ndani ama la.
 
Watu hukusoea mno kusema
'sijui kama nitaweza penda mwingine'
ukishajifunga hivyo utateseka mno....

rule ya maisha..ni moja tu
ukiona mtu anakutesa move on..

Hakuna kitu kibaya kama kuishi kwa kutegemea uwepo wa mtu flani hasa mpenzi wako... .
 
Tatizo lako la kwanza ni kujiona huwezi k'kupata yeyote unaemtaka'
sasa kwa kuwa huyo alijitokeza na wewe ukaona umebahatika kumpata..

kumbe huyo ni kicheche tu kama vicheche wengine...sanasana angekusummbua kwenye ndoa

kuhusu kumuelewa..nani aliekuambia tunatakiwa kuwaelewa watu woote tunaokutana nao????

wengine wao wenyewe hawajielewi,why wewe uumize kichwa kuwaelewa?

just move on..tafuta mwingine....fast
mkuu nashukuru kwa haya. lakini hebu nikueleze kitu kidogo nilitaka nikiweke siri ila sasa naona sina jinsi n naomba sana sana hunijui sikujui nishauri kwa utashi wako wote.

toka nipooze miguu ni mwaka wa sita sasa na ni miaka miwili tu uume wangu umeweza kusimama japo kidogo. lakini kutokana na hali hii bado dr alinihakikishia kwamba ninaweza kuzaa kwani mbegu zangu ziko salaa sema tu uume wa kuitisha ndo hauna nguvu sana.

kwa miaka hii miwili binti huyu nilimwambia na alikubali kabisa hali halisi, na kwakujua kwamba ni mwanamke anahitaji nini wakati wa tendo basi nilitumia njia nyingine kuliko kumpandia ingawa pia nilipanda mara moja moja. kwa jinsi ambavyo binti alinipokea nilipata faraja sana juu ya jambo hili na sikuwaza tena upweke wala unyanyapaa juu yanu. sasa leo hii anapoharibu mimba tena kwa kulazimisha inanipa hofu labda hataki kuzaa na mm ama haikuwa yangu.

najaribu kukaa kutafuta jibu ambalo litanipa nafuu silioni, na nahofia sana kuanza uhusiano na mtu mwingine ajue tatizo langu je nifanyeje?

nisamehe kama hujanielewa.
 
Hakuna kitu kibaya kama kuishi kwa kutegemea uwepo wa mtu flani hasa mpenzi wako... .

mkuu usiseme hivyo. labda kama wewe umejitosheleza kwa kila kitu. wengine hao wapenzi wetu tunategemea watusaidie sana, hasa kwa matendo ya kimwili zaidi.
 
kwanza pole sana mkuu,pili mbona kutoa mimba ni kama fashion karne hii? Sio kitu cha kushangaa saana ila wengi wanatoa kwa sababu ya matatizo ya aidha aliyempa hiyo mimba ameikataa au sababu nyingine nyingine zinazojulikana. Cha kujiuliza ni kwamba iweje aende kuitoa hiyo mimba ilhali wewe ulishakubali kuihudumia?
Kuna kitu kimefichika hapo,mtafute na ujaribu kuongea naye vizuri na kama majibu yake yatakuridhisha basi uamuzi ni wako umrudishe ndani ama la.

naomba nieleweshe jambo hapa, kama mdada kaitoa mimba yako je anaweza kweli kuwa na mapenzi na wewe?
 
Huyo alikuwa ana KUCHEZEA tu, Mungu atakupa mwingine ambaye mtaISHI naye mkiCHEZA pamoja kwa uzuri.

amina.

Lakini je naweza kufanya vipi ili nisione ugumu wa kutafuta mwanamke mwingine hasa nikiangalia niliwah kupooza miaka 6 iliyopita na uume wangu umeanza kusimama miaka 2 iliyopita. nilijifungua kwa huyu na kumweleza ukweli wote na alikubali hali yangu. kiukweli wajua hali ya ulemavu ilivyo, kwahiyo nilifarijika sana kupata mtu kama yeye. sasa je niambie nitafanyeje?
 
Kabisa. Aachane nayr haraka sana. Unawezekana kabisa mimba aliyotoa sio ya jamaa yetu.

Cha muhimu ndugu yangu zingatia kazi na Mungu atakuonyesha mwingine. Huyu hakufai kabisa. Ni kawaida kwen maisha

nashukuru sana ila je nifanyeje sasa?
 
ninawashukuru wote waliotoa mchango wao kwangu. mbarikiwe sana. ila sasa ninaombi moja kwenu.

nitawezaje kuanza na mwanamke mwingine ukizingatia kwamba mimi ni mlemavu wa miguu, na uume wangu unasimama lakini sio sana kama ilivyo kawaida kwa wanaume wengine? huyu niliyekuwa nae nilimweleza na ndo alikuwa wa kwanza akakubali na nilifarijika sana sana kwa hilo, sasa linapotokea hili ndipo nazidi kuchanganyikiwa kwamba nitamwambiaje mwanamke ili anielewe?
 
Pole sana ndugu, ila usikate tamaa pambana sana tu, saka hizo hela hadi zianze kukusaka zenyewe tafuta mwanamke wa kuoa Mungu atakuonyesha, utampata tu, ila kwa huyo binti mi naona achana nae tu ile mimba sidhani kama ni yako, labda ungekaa nae uongee nae umsikilize kinagaubaga, ushauri wangu kwako ni
USIKATE TAMAA PAMBANA TU. yo in my prayers ndugu.
 
nina hisia/imani asilimia kubwa sana hiyo mimba haikuwa yako....katoa kupoteza ushahidi. pole mkuu, chunguza kwanza kabla ya kuoa.
 
Pole sana ndugu, ila usikate tamaa pambana sana tu, saka hizo hela hadi zianze kukusaka zenyewe tafuta mwanamke wa kuoa Mungu atakuonyesha, utampata tu, ila kwa huyo binti mi naona achana nae tu ile mimba sidhani kama ni yako, labda ungekaa nae uongee nae umsikilize kinagaubaga, ushauri wangu kwako ni
USIKATE TAMAA PAMBANA TU. yo in my prayers ndugu.

asante sana mkuu. ngoja niapambane tu ila ni ngumu kweli kumeza
 
nakubalina nawqe kwa asilimia kubwa,ila naomba niongezee hapo kwenye nyekundu....nafikiri upo uwezekano kuwa si yake,maana kama ni uhakika wa kuolewa alisha hkikishiwa ndo maana maadalizi ya posa yalishakuwepo,so hakuwa na haja ya kutoa mimba
Kwanza Pole Sana Mkuu, nilivyoeelewa ni hivi:

Huyo mdada analiwa mzigo na wanaume wenzio huko kwao kwa kuwa hana njia nyingine ya kupata mkwanja.. Anafanya hivyo ili kujikimu, kumbuka ushamzoesha maisha mazuri kutokana na juhudi zako kazini.

Kwa Upande wa kutoa mimba sijafikiria kiundani sana, ila acha nikwambie kitu, kulea mimba ni kazi sana.. Kumbuka tayari anamtoto, mbaya zaidi amemlea kwa miaka 4 mwenyewe kabla ya kukutana na wewe, hivyo anajua machungu na Karaha zote za kulea... Kuna uwezekano hataki kushika mimba hiyo kwa sasa kwakua hataki kukumbuka magumu na mabaya yaliyotangulia..

Pia tukiangalia kutokea ktk angle nyingine inawezekana anakuepusha na lawama za kudumu.. Kuna uwezekano ukawa siyo ujauzito wako kwa kuzingatia kua muda mchache baada ya kurudi kwao amekua tayari kushiriki tendo la ndoa na wanaume wengine, hii ni kusema kwamba ana uzoefu wa mambo hayo, so pia inawezekana pia ulipokua nae alikua pia anagawa pembeni..

Ushauri wangu ni huu; Unajua alievaa kiatu ndiye ajuae msumali unachomea wapi, wewe binafsi ndiyo unafahamu nafasi ya huyo malkia ndani ya nafsi yako..

Hayo ni matatizo ya kawaida tu katika maisha ya ndoa hasa katika kizazi hiki cha digital bila kuzingatia kabila la shemeji yetu.

Kaa chini muyazungumze wewe na yeye.. Atakavyokua anarespond hoja ma mitazamo yako utajua usuke au unyoe..

WANAUME TUMEUMBWA MATESO
 
Aliyeruhusu hilo Jaribu likupate, ambaye alikivusha kwenye huo mtihani na akakuletea huyo binti ndiye atakaye kupa nguvu, mke mwema, watoto na maisha yenye upendo, uvumilivu na amani.

Wasiwasi (mawazo) hautakusaidia kwani uzoefu unaonesha, huharibu zaidi ya kujenga!

Muamini Mungu, mengine yote yatakuja!
amina.

Lakini je naweza kufanya vipi ili nisione ugumu wa kutafuta mwanamke mwingine hasa nikiangalia niliwah kupooza miaka 6 iliyopita na uume wangu umeanza kusimama miaka 2 iliyopita. nilijifungua kwa huyu na kumweleza ukweli wote na alikubali hali yangu. kiukweli wajua hali ya ulemavu ilivyo, kwahiyo nilifarijika sana kupata mtu kama yeye. sasa je niambie nitafanyeje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom