Nimwambie Ukweli?

Nimwambie Ukweli?

Madam umemaliza yote,huyu bado hajapigwa kikimkolea hatotaka kushauriwa na mtu! Mimi yule mdogo wangu aliyepigwa last wk mpaka akazimia alikua akipigwa hivyo hivyo unamshauri lakini baada ya siku mbili tatu mapenzi moto wanarudiana na bwanake ila kipigo cha juzi nilikua kiboko maana mpaka kuzimia juu bibie mweupe lakini akawa mwekundu kwa kuvilia bwana anapiga usoni kichwani,sasa hivi amepata nafuu na yeye mwenyewe ndio ameagiza akachukuliwe vitu vyake kwa bwanake hana shida ya kesi tuliyoripoti polisi hivi nnavyoongea Jana jioni tumemsafirisha kwenda Mwanza kwa ndugu yetu mkubwa,hataki hata kumsikia. Hivyo hata huyu siku kikimkolea kipigo hatotaka hata ushauri

Sent using Jamii Forums mobile app
LadyAJ mapenzi hatari sana ila kwa nn upigwe hivo? Me namuombea tu afunguke akili yake ajijue thamani yake

Madame S
 
Mpuuzi tuh uyo,mpige chini..wakurya hatuna sifa hizo sasa hivi..!dunia imebadilika.atakuua kwa ujinga wake wa wivu alafu asingizie ukurya.
 
story bado anatunga huyo jamaa au kaacha maana alivyohack account yako akajifanya ni wewe aliongea mengi humu lakini mi nkajua shabiki mwenzangu wa yanga hawezi kufanya hvyo lazima yule mwandika story kafanya kitu
 
Duh tutake radhi wakurya.
Naombeni mpuuze hilo neno "Mkurya" kama alivyolitumia mtoa mada.
Wakurya ni wakarimu na wenye upendo sana.
 
Habari zenu?
Mimi ni member mkongwe humu.Nimebadili ID baada ya Id yangu ya zamani kubadilishwa password na 'kutekwa' na mwanamme alokuwa Mpenzi wangu.

Sitopenda kuitaja kwa kuwa ameshabadilisha user name na sihitaji kujitafutia matatizo kwa Kuwa hata huu uzi atausoma.Najua dude ninaloliamsha sio la dunia hii lakini nimeamua kama mbwai na iwe mbwai!

Nije moja kwa moja kwenye mada.Nimekuwa na mpenzi wangu huyu kwa muda wa miaka miwili.Kwa kweli mapenzi yetu yalianza kama utani tu humu jukwaani.Nakumbuka ilikuwa mada nachangia.Akani' quote' aisee mwanamme mkorofi huyu,alinitukana matusi ambayo sikujua chanzo chake.Kisa nilitetea mwanamke kuomba hela kwa mpenzi wake.
Sikumjibu mkurya yule.

Ikawa tabia yake akikuta hata like tu lazima ani harass!Nikawa namu ignore.Kitabia mimi ni mpole sana siwezi kujibishana.Nakumbuka mara ya mwisho yalinishinda nikamvaa na mimi hapa,libeneke lilichezwa nikaambulia ban ya mwezi.
Ban yangu ilivyoisha akanifuata Pm kwa upole akaniomba msamaha.Nikajikuta tu namsamehe.Mawasiliano yalianza na kupamba kasi kwa mwendo wa farasi.
Tukawa karibu mno mpaka baada kama ya mwaka hivi ndio nikawa huru japo kutoa namba yangu maana kwa kipindi hiko nilikuwa nimetoka kuachana na mtu sikutaka ukaribu wa haraka.
Baada ya kuonana na mawasiliano ya karibu sana tukajikuta tunapendana.Kwa kweli sikuwahi kujua kama kuna wanaume wakarimu kama huyu kaka nimwite 'Y'.

Yani He was so romantic,charming and loving.Alinipa madeko,alinipa mapenzi ya hali ya juu.Muda wa libeneke nilikuwa naomba 'po'.
Alikuwa mshauri wangu,rafiki yangu.
Nitake nini nisipewe,tofauti kabisa na nilivyomchukulia.Alinihamisha Sinza akanipeleka Mbezi karibu na kwake na kodi juu yake.Zaidi aliwapenda ndugu zangu wote alopata bahati ya kuwafahamu.Alikuwa sio bahili juu yangu kabisa.

Sikuwa mwepesi kutaka kumpeleka kwetu wala mimi sikukubali anipeleke kwao kwani niliwahi mpaka kutolewa barua ya uchumba alafu uchumba ukaisha baada ya mwanamme nilokuwa naye kuzaa na rafiki yangu kipenzi.

Jamani nilipohamia karibu na 'Y' ndio nilijua kama maharage ni mboga au kiungo cha makande.
Alinipiga marufuku kupitia kokote nikitoka kazini.Hataki marafiki wala jamaa.
Nikae ndani nipike nile nilale.Kazi yake ilikuwa inamkeep bussy mpaka saa tatu usiku basi lazima aje,aniangalie mara nyingi alikula.
Nikasema ngoja nitii.Nikaachana na marafiki nikawa mtu adimu hata kwenye masherehe ya watu sitokei tena.
Akija atakagua simu,emails tena akiwa very calm.
Jamani akikuta namba ngeni nitawekwa kikaangoni!Nilimweleza mimi sio mtu wa namna hiyo wala siwezi kumsaliti.
Jamani akawa anafanya ambush sasa,mara aje kimya kimya kama jambazi,mara aje dirishani mpaka akawa ananistua.Alivyoona haitoshi akaniomba nihamie kwake.Sikukubali nikawa nalala kwake mara nyingi kwangu nafunga.Mpaka siku nikavunjiwa mlango wa mbele na kusombewa kila kitu.

Hapo ndio akapata kisingizio cha kunihamishia kwake.Nilivyohamia kwake akazidisha wivu.Akipiga simu mchana kama inatumika nikirudi jioni nazabuliwa kama mtoto.Kitu kidogo mpaka anipige vibao.Nilikaa naye chini mara nyingi na kumweleza kutoridhishwa kwangu na ile tabia.Lakini hakuacha,nisipojisikia sex ngumi.Nikipigiwa na mwanamme ngumi.Nikapoteza furaha na nuru kabisa.Nikaamua kumuacha.
Nikaendelea na maisha yangu.Nikamblock kila mahali.Akija sifungui aisee mlango utapigwa mateke mpaka nafungua akiingia anaomba msamaha.Nikaamua kuhama baada ya usumbufu kuzidi.Sio kwamba nilikuwa simpendi ila mateso yake yalizidi.Kipigo jamani.

Akawatumia ndugu na rafiki zangu.Nikakubali turudiane ila sikutaka kurudi kwake.Sasa akahack kila kitu changu.Akadai anataka kuwaona wazazi.Moyo ukasita.Jamani Y alizidisha wivu hadi message za kuforward anakasirika.Ananipiga na bado sex anataka.
Nilishindwa kwa kweli.Namiss treatments na sex lakini nikikumbuka yale mateke na mangumi nashindwa.
Sijui nifanyeje ananistalk kila mahali mpaka kazin muda wa kutoka unamkuta Getini.Sina raha bila yeye nampenda lakini naogopa kumrudia hawezi kuacha kunipiga kabisa.
Naomba ushauri wenu.
Wewe una matatizo! Kwani unafikiri hakuna mwanaume mwingine wa kukupa vitu km yeye au zaidi yake? Subiri uwe kilema akuache yeye!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
dadeek sijui nimtukane tusi gani uyu me mwenzangu pumbaaf
watu wengine tunamtafuta huyo mwanamke mwenye mapenzi ya kweli miaka yote hatuoni yeye anapiga ,,,,,shiit!!!!
 
Habari zenu?
Mimi ni member mkongwe humu.Nimebadili ID baada ya Id yangu ya zamani kubadilishwa password na 'kutekwa' na mwanamme alokuwa Mpenzi wangu.

Sitopenda kuitaja kwa kuwa ameshabadilisha user name na sihitaji kujitafutia matatizo kwa Kuwa hata huu uzi atausoma.Najua dude ninaloliamsha sio la dunia hii lakini nimeamua kama mbwai na iwe mbwai!

Nije moja kwa moja kwenye mada.Nimekuwa na mpenzi wangu huyu kwa muda wa miaka miwili.Kwa kweli mapenzi yetu yalianza kama utani tu humu jukwaani.Nakumbuka ilikuwa mada nachangia.Akani' quote' aisee mwanamme mkorofi huyu,alinitukana matusi ambayo sikujua chanzo chake.Kisa nilitetea mwanamke kuomba hela kwa mpenzi wake.
Sikumjibu mkurya yule.

Ikawa tabia yake akikuta hata like tu lazima ani harass!Nikawa namu ignore.Kitabia mimi ni mpole sana siwezi kujibishana.Nakumbuka mara ya mwisho yalinishinda nikamvaa na mimi hapa,libeneke lilichezwa nikaambulia ban ya mwezi.
Ban yangu ilivyoisha akanifuata Pm kwa upole akaniomba msamaha.Nikajikuta tu namsamehe.Mawasiliano yalianza na kupamba kasi kwa mwendo wa farasi.
Tukawa karibu mno mpaka baada kama ya mwaka hivi ndio nikawa huru japo kutoa namba yangu maana kwa kipindi hiko nilikuwa nimetoka kuachana na mtu sikutaka ukaribu wa haraka.
Baada ya kuonana na mawasiliano ya karibu sana tukajikuta tunapendana.Kwa kweli sikuwahi kujua kama kuna wanaume wakarimu kama huyu kaka nimwite 'Y'.

Yani He was so romantic,charming and loving.Alinipa madeko,alinipa mapenzi ya hali ya juu.Muda wa libeneke nilikuwa naomba 'po'.
Alikuwa mshauri wangu,rafiki yangu.
Nitake nini nisipewe,tofauti kabisa na nilivyomchukulia.Alinihamisha Sinza akanipeleka Mbezi karibu na kwake na kodi juu yake.Zaidi aliwapenda ndugu zangu wote alopata bahati ya kuwafahamu.Alikuwa sio bahili juu yangu kabisa.

Sikuwa mwepesi kutaka kumpeleka kwetu wala mimi sikukubali anipeleke kwao kwani niliwahi mpaka kutolewa barua ya uchumba alafu uchumba ukaisha baada ya mwanamme nilokuwa naye kuzaa na rafiki yangu kipenzi.

Jamani nilipohamia karibu na 'Y' ndio nilijua kama maharage ni mboga au kiungo cha makande.
Alinipiga marufuku kupitia kokote nikitoka kazini.Hataki marafiki wala jamaa.
Nikae ndani nipike nile nilale.Kazi yake ilikuwa inamkeep bussy mpaka saa tatu usiku basi lazima aje,aniangalie mara nyingi alikula.
Nikasema ngoja nitii.Nikaachana na marafiki nikawa mtu adimu hata kwenye masherehe ya watu sitokei tena.
Akija atakagua simu,emails tena akiwa very calm.
Jamani akikuta namba ngeni nitawekwa kikaangoni!Nilimweleza mimi sio mtu wa namna hiyo wala siwezi kumsaliti.
Jamani akawa anafanya ambush sasa,mara aje kimya kimya kama jambazi,mara aje dirishani mpaka akawa ananistua.Alivyoona haitoshi akaniomba nihamie kwake.Sikukubali nikawa nalala kwake mara nyingi kwangu nafunga.Mpaka siku nikavunjiwa mlango wa mbele na kusombewa kila kitu.

Hapo ndio akapata kisingizio cha kunihamishia kwake.Nilivyohamia kwake akazidisha wivu.Akipiga simu mchana kama inatumika nikirudi jioni nazabuliwa kama mtoto.Kitu kidogo mpaka anipige vibao.Nilikaa naye chini mara nyingi na kumweleza kutoridhishwa kwangu na ile tabia.Lakini hakuacha,nisipojisikia sex ngumi.Nikipigiwa na mwanamme ngumi.Nikapoteza furaha na nuru kabisa.Nikaamua kumuacha.
Nikaendelea na maisha yangu.Nikamblock kila mahali.Akija sifungui aisee mlango utapigwa mateke mpaka nafungua akiingia anaomba msamaha.Nikaamua kuhama baada ya usumbufu kuzidi.Sio kwamba nilikuwa simpendi ila mateso yake yalizidi.Kipigo jamani.

Akawatumia ndugu na rafiki zangu.Nikakubali turudiane ila sikutaka kurudi kwake.Sasa akahack kila kitu changu.Akadai anataka kuwaona wazazi.Moyo ukasita.Jamani Y alizidisha wivu hadi message za kuforward anakasirika.Ananipiga na bado sex anataka.
Nilishindwa kwa kweli.Namiss treatments na sex lakini nikikumbuka yale mateke na mangumi nashindwa.
Sijui nifanyeje ananistalk kila mahali mpaka kazin muda wa kutoka unamkuta Getini.Sina raha bila yeye nampenda lakini naogopa kumrudia hawezi kuacha kunipiga kabisa.
Naomba ushauri wenu.
Huo ukweli unaotaka kumwambia ni UPI?BTW pole.
 
Nawe ni mkurya,jina lako kama la dem wangu mtt wakikurya.
 
Ile tabia ya kwanza ya matusi aliyokuonyesha humu ndo ilikua yake huo upole aliokunyesha ilikua ana pretend sasa amerudia tabia yake baada ya kuzoeana mi nakushaur achana nae usiendekeze sana mapenz angalia what is best for u

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wivu ni ugonjwa mbaya alie nao aspojtambua na kuchukua hatua za kujidhibit hakuna afuen........ Muv on mapenz ya kupgna hayana nafas unless unatafuta kilema
 
Bora hayo... hachelewi kumkeketa kwa kisu...

Mkurya si mtu wa kispotispoti...

Ila kuna watu wengine wanafikiri vichaa ni lazima wawe wanaokota makopo barabarani... Afu wakija kuuliwa watu wanasingizia mapenzi ya Mungu. Mungu kashakupa akili unataka akufundishe namna ya kuitumia?
hahaàaaa
 
Wakurya wanajua kupenda, wana wivu, wanakurupuka kwene maamuzi hasa kwa mpenz/ au mke usiombe.....km unampenda hali ndo iyo iyo shouger angu akuna kitachobadilika itafikia ata ukiongea na mama anahisi unaongea na njemba
 
Back
Top Bottom