Nimsaidieje x-girlfriend wangu

sifongo

JF-Expert Member
Jun 5, 2011
4,896
5,302
Habari wanajamvi, naomba nikiri na kujutia dhambi niliyofanya mimi na mwenzangu (aliyekuwa girlfriend wangu). Miaka kadhaa nyuma nilikuwa na girlfriend nilimpenda naye alinipenda japo nilikuwa najua ananichiti coz sikuwa na hela ya kutosheleza mahitaji yake, kiukweli alikuwa anapenda maisha juu.

Tulidumu kwa miaka 4 katika uhusiano wetu na katika dhambi kubwa tuliyofanya ni kuwa tulitoa mimba 3, mbili niliridhia na ilipokuja ya 3 nilimuambia tuzae kwani tatizo ni nini, nyumba ya kukaa bure ipo, yeye anafanya kazi na mimi namaliza masomo muda si mrefu nitakuwa na ajira ya kudumu kwani hapo mwanzo nilikuwa naunga unga kazi, huyu binti alikataa kata kata tuzae na akaja kuitoa hiyo mimba.

Siku moja akanimbia wanakwenda kwenye sherehe ya kiofisi hivyo hatutakuwa wote wikiend hiyo nikamuambia poa, na mimi nikamtafuta mshikaji wangu mmoja nikijua wikiend nyingi anakuwaga na kazi za shooting kwenye maharusi, japo nikampe tafu hata ya kuvuta waya wa taa na ikawa hivyo, ishu ilikuwa ni ISTANA pale victoria.

Sitaisahau hii siku, mmoja wa waalikwa katika hiyo harusi ni demu wangu na alikuwa na mshikaji mwenye hadhi ya juu si kama mimi nakiri hivyo, tukaonana uso kwa uso akaduwaa nikajitahidi kumpotezea nikiogopa nisije kutambulishwa kama kaka mtu, jamaa yangu aliona mchezo wote akajua kabisa siwezi kumudu kukaa pale na ilikuwa hivyo, nikatoka nikaenda home, nilipata uchungu wa ajabu lakini sikuwa na jinsi, nilijaribu kupiga simu iliita na kukatwa kisha ikazimwa na ukawa ndio mwisho wa uhusiano wetu.

Miaka imepita nina mke na binti wa miaka miwili na yeye bado hajaolewa, maisha yanasogea ni juzi tu nimekutana na rafiki yake pale jojis akaniuliza kama bado nawasiliana na shoga yake nikamuambia sio sana, japo kuna muda tunasalimiana kwa simu, basi katika maongezi ndio akaniambia kuwa hata jana yake walikuwa wote hospital kwani ana matatizo ya kutopata mimba, amejaribu mara kadhaa na ishu imekataa kabisa, roho iliniuma nikikumbuka tuliyofanya huko nyuma yeye hajaniambia hilo tatizo ila natamani kumpigia nisikie toka kwake.......nisaidieni wanajamvi kufanya maamuzi, nimpigie au nitulie nisijeonekana mwanga.
 
Wewe now deal na mungu wako tu...

Yeye akiona umuhimu wa kukushirikisha atakuita...
kama hujaitwa....endelea na maisha yako

unajuaje hizo mimba zote alizotoa zilikuwa zako?
 
hivi kwann Mungu hakukunyima na wewe mtoto?? anyway nisiingilie kazi ya Mungu.
sina ushauri wa kukupa kwani sitaki kukushauri wewe ila nataka kupitia ubao huu ulioko hapa uliouweka wewe niseme na mabinti wadogo wa hapa jf.

siku zote athari za kuharibu mimba huwa ni mzigo wa mwanamke. unayekwenda kuchokonolewa ni wewe binti na wanaokuchokonoa mida mingine hata nyenzo nzuri hawana sasa wewe unazibwa mirija kwa makosa ambayo ungeweza kuyaepuka. sion sababu ya kuharibu mimba kama tayari umeipata zaa mwanao kisha maisha yatasonga mbele. sikazi hata huyo unayemlinda hana mpango wa kuwa na wewe ukishaharibika kwa utoaji wa mimba.

kwanza jueni kizazi cha mwanamke kinaakili sana kama uki-inhibit the stimulus basi kita jijengea kwamba njia hii ndo sahihi basi hakikubali tena kushika mtoto manake ulisha kiambia mtoto akiingia lazima atoke.

angalia mtu ambaye yuko prone to conception, huwa anakuwa hivi hivi na kizazi kinajua hivyo so akigusa tu inanasa kadhalika na yule ambaye ni mtoaji kizazi kina- act hivyo hivyo akiingia tu kinatoa ama kinakataa kabisa kupokea. kutoa mimba mara 3 ni nyingi sana.
 
Kumbe ni kweli haya mambo yanatokea! Eeh Mungu, niepushie balaa hili..!

Ushauri.: endelea tu na mambo yako mkuu, hata wewe ulikuaffected sema kwakuwa ni Mwanaume siyo rahisi kuona impact zake waziwazi..

Don't trust a woman even if she is dead
 
Habari wanajamvi, naomba nikiri na kujutia dhambi niliyofanya mimi na mwenzangu (aliyekuwa girlfriend wangu). Miaka kadhaa nyuma nilikuwa na girlfriend nilimpenda naye alinipenda japo nilikuwa najua ananichiti coz sikuwa na hela ya kutosheleza mahitaji yake, kiukweli alikuwa anapenda maisha juu.

Tulidumu kwa miaka 4 katika uhusiano wetu na katika dhambi kubwa tuliyofanya ni kuwa tulitoa mimba 3, mbili niliridhia na ilipokuja ya 3 nilimuambia tuzae kwani tatizo ni nini, nyumba ya kukaa bure ipo, yeye anafanya kazi na mimi namaliza masomo muda si mrefu nitakuwa na ajira ya kudumu kwani hapo mwanzo nilikuwa naunga unga kazi, huyu binti alikataa kata kata tuzae na akaja kuitoa hiyo mimba.

Siku moja akanimbia wanakwenda kwenye sherehe ya kiofisi hivyo hatutakuwa wote wikiend hiyo nikamuambia poa, na mimi nikamtafuta mshikaji wangu mmoja nikijua wikiend nyingi anakuwaga na kazi za shooting kwenye maharusi, japo nikampe tafu hata ya kuvuta waya wa taa na ikawa hivyo, ishu ilikuwa ni ISTANA pale victoria.

Sitaisahau hii siku, mmoja wa waalikwa katika hiyo harusi ni demu wangu na alikuwa na mshikaji mwenye hadhi ya juu si kama mimi nakiri hivyo, tukaonana uso kwa uso akaduwaa nikajitahidi kumpotezea nikiogopa nisije kutambulishwa kama kaka mtu, jamaa yangu aliona mchezo wote akajua kabisa siwezi kumudu kukaa pale na ilikuwa hivyo, nikatoka nikaenda home, nilipata uchungu wa ajabu lakini sikuwa na jinsi, nilijaribu kupiga simu iliita na kukatwa kisha ikazimwa na ukawa ndio mwisho wa uhusiano wetu.

Miaka imepita nina mke na binti wa miaka miwili na yeye bado hajaolewa, maisha yanasogea ni juzi tu nimekutana na rafiki yake pale jojis akaniuliza kama bado nawasiliana na shoga yake nikamuambia sio sana, japo kuna muda tunasalimiana kwa simu, basi katika maongezi ndio akaniambia kuwa hata jana yake walikuwa wote hospital kwani ana matatizo ya kutopata mimba, amejaribu mara kadhaa na ishu imekataa kabisa, roho iliniuma nikikumbuka tuliyofanya huko nyuma yeye hajaniambia hilo tatizo ila natamani kumpigia nisikie toka kwake.......nisaidieni wanajamvi kufanya maamuzi, nimpigie au nitulie nisijeonekana mwanga.

sijui kwanini mtu akiongelea habari za ex..friend wake moyo unanienda mbio kwa hasira,..yaani mtu umeoa na mtoto/watoto bado unafikiria,....uuuuuuuuuuuuuuuuuh puuuuuuuf
 
Wewe now deal na mungu wako tu...

Yeye akiona umuhimu wa kukushirikisha atakuita...
kama hujaitwa....endelea na maisha yako

unajuaje hizo mimba zote alizotoa zilikuwa zako?

Hili nalo neno mkuu, nilichukulia kitanda hakizai haramu......thanks kwa ushauri.
 
Wewe endelea na maisha yako maana una mke na watoto wako na yeye huko aliko ana yake
Kama angetaka ushauri kwako au kumsaidia asingeshindwa kukupata
Na hapo huwezi jua ulikuwa unashikishwa hata hizo mimba inawezekana hazikuwa zako
So songa mbele na maisha yake kama alivyosema The Boss hapo juu
 
Last edited by a moderator:
jaman mkuu kafunguka kama muwazi na amekiri makosa aliyofanya,sasa hivi anaitaj ushauri,siyo kumkemea kwa mambo ya zamani
 
Daaah inaskitisha sana! Muombe na umshukuru mungu kwani umezaliwa mawanaume sijui ungejisikiaje kama wewe ungekuwa umepatwa na tatizo hilo?
 
Hizo mimba zilikuwa za wachina ndo maana ali insist kuomba mnyofoe, na wewe bila kujua ukaingia mkenge.

Mkuu mwanamke akisema mtoe mimba ujue kishacheza rafu na anakuwa anaogopa atazaliwa mwarabu wa dubai wakati wewe ni mwarabu wa kigoma!
 
--- roho iliniuma nikikumbuka tuliyofanya huko nyuma yeye hajaniambia hilo tatizo ila natamani kumpigia nisikie toka kwake.......nisaidieni wanajamvi kufanya maamuzi, nimpigie au nitulie nisijeonekana mwanga.
We kaka naona sio roho inakuuma bali umechanganyikiwa sasa, what the hell on earth is that.Hivi wewe unataka kumpigia ili umwambie nini.Unataka kumpigia mkafukue watoto wale watatu umwekee tumboni ama unataka kumpigia kana kwamba akisikia tu sauti yako mimba itatungwa ghafla.Dont call her maana hauna msaada at the moment and forever in the situation your x is facing
 
We kweli una dhambi yani unataka kwenda kuendelea ku uwa wengine, yani ukimgusa tu ana beba mimba afu anauwa faida yake nini.
 
kama unataka kuharibu familia yako anza ushauri wako coz da moment ur wife recognize dat u will be in trouble. achana nae we endelea na mingo zako.
 
Sasa unataka umpigie ili iwije??

Umshauri kuhusiana na tatizo lake??

Au mkumbushie vitu vya awali? Mkuu u married .. Move on with ya marriage achana na hivi vitu ambavyo badae vitaleta tafran katika ndoa yako.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom