Nimsaidieje ndugu yangu huyu?

Njemba Soro.

JF-Expert Member
Oct 5, 2013
3,246
5,757
Habari za muda.....
Nipo moshi kwa ajili ya sikukuu hizi ila kuna jambo nimeona niombe ushauri hapa na najua kuna watakaojifunza kitu hasa vijana.

Kuna rafiki yangu wa utotoni, shule ya msingi, sekondari na mpaka pilikapilika za maisha tulianza wote.
Tulianza na biashara ya magadi, tunatoka kijijini kwetu tunaenda kule wanaita Rongoi tunachimba magadi tunakuja kuuza kijijini, baadaye tukaanza biashara ya malimao
Tunakusanya malimao mitaani halafu tunapelEKa soko la mbuyuni tunauza bei ya jumla kwa wanaoleta dar.
Tukakuza mtaji tukaingia kwenye biashara ya mpunga, tukaenda chekereni na mabogini tukapata faida sna kwenye hiyo biashara ya mpunga na maana ni biashara ya msimu ikabidi tubadilishe biashara.

HAPA SASA JAMAA AKAKURUPUKA. Mimi niliingia kwenye biashara ya matunda, nikawa nasafirisha mafenesi, mapapai, na maembe kulingana na msimu kutoka Moshi kwenda Dar, au Mombasa, au Nairobi.
Jamaa yeye akaniambia anakuja dar kupambana na ukawa mwisho wa kuonana naye na simu ilifika kipindi hatukuwasiliana tena.
Sasa juzi nimekuja Moshi jamaa nimemkuta anakula ugoro, mbege, sigara na kila pombe jamaa anabugia. Jamaa amezeeka sana na amechoka.
Ndugu yake ananieleza jamaa alifilisiwa na wanawake wa dar pamoja na waganga wa kienyeji......

Huyu jamaa analazimisha sana nirudi naye dar lakini sioni kama ana namna tena ya kujirekebisha hasa ukizingatia naogopa sana ushirikina na ulevi. Hata yeye nikiongea naye mambo mengi anazungumzia ushirikina na anapenda sana huo ujinga.

NIMSAIDIEJE HUYU JAMAA???
1-Nimpe mtaji abaki moshi?
2-Nikubali kuja naye dar....
3-NIACHANE NAYE TU.

Naombeni ushauri....
 
Habari za muda.....
Nipo moshi kwa ajili ya sikukuu hizi ila kuna jambo nimeona niombe ushauri hapa na najua kuna watakaojifunza kitu hasa vijana.

Kuna rafiki yangu wa utotoni, shule ya msingi, sekondari na mpaka pilikapilika za maisha tulianza wote.
Tulianza na biashara ya magadi, tunatoka kijijini kwetu tunaenda kule wanaita Rongoi tunachimba magadi tunakuja kuuza kijijini, baadaye tukaanza biashara ya malimao
Tunakusanya malimao mitaani halafu tunapelEKa soko la mbuyuni tunauza bei ya jumla kwa wanaoleta dar.
Tukakuza mtaji tukaingia kwenye biashara ya mpunga, tukaenda chekereni na mabogini tukapata faida sna kwenye hiyo biashara ya mpunga na maana ni biashara ya msimu ikabidi tubadilishe biashara.

HAPA SASA JAMAA AKAKURUPUKA. Mimi niliingia kwenye biashara ya matunda, nikawa nasafirisha mafenesi, mapapai, na maembe kulingana na msimu kutoka Moshi kwenda Dar, au Mombasa, au Nairobi.
Jamaa yeye akaniambia anakuja dar kupambana na ukawa mwisho wa kuonana naye na simu ilifika kipindi hatukuwasiliana tena.
Sasa juzi nimekuja Moshi jamaa nimemkuta anakula ugoro, mbege, sigara na kila pombe jamaa anabugia. Jamaa amezeeka sana na amechoka.
Ndugu yake ananieleza jamaa alifilisiwa na wanawake wa dar pamoja na waganga wa kienyeji......

Huyu jamaa analazimisha sana nirudi naye dar lakini sioni kama ana namna tena ya kujirekebisha hasa ukizingatia naogopa sana ushirikina na ulevi. Hata yeye nikiongea naye mambo mengi anazungumzia ushirikina na anapenda sana huo ujinga.

NIMSAIDIEJE HUYU JAMAA???
1-Nimpe mtaji abaki moshi?
2-Nikubali kuja naye dar....
3-NIACHANE NAYE TU.

Naombeni ushauri....
Kwanza kaa naye kwa muda ongea naye ujue anataka kufanya nini, pili mwambie kwa uwazi tabia zake na jinsi itakavyo kuwa ndoto kufanikiwa kama hatakuwa tayari kubadilika tatu hata akushawishi vipi mpe pesa achana naye ukija naye atakuwa mzigo kwako na anaweza kukuharibia michongo yako. Mwambie utamwita baada ya kuona mabadiliko yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza kaa naye kwa muda ongea naye ujue anataka kufanya nini, pili mwambie kwa uwazi tabia zake na jinsi itakavyo kuwa ndoto kufanikiwa kama hatakuwa tayari kubadilika tatu hata akushawishi vipi mpe pesa achana naye ukija naye atakuwa mzigo kwako na anaweza kukuharibia michongo yako. Mwambie utamwita baada ya kuona mabadiliko yake

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukurani....
 
Mosi tambua umeingia kwenye mtego ambao ukiuruka utakuwa komando kipensi. Huyo jamaa tayari ulevi umemkolea na si jambo dogo kumtoa kwenye hiyo hali. Hivyo wewe rafiki yake umekutana na changamoto ambayo ukicheza vibaya huwenda nawe ukawa na future mbaya.

Huyo jamaa anataka uangalizi je utakuwa tayari kuwa mwangalizi wake na ukianza kumpa mtaji tegemea kuwa anaanza upya hivyo kupata na kukosa ni sehemu yake. Ukimpa mtaji bila yeye kuwa tayari kufanya kile unacholenga au unachowaza ni sawa na kumpa hela ya kunywea gongo na kununulia ugoro.

Yeye anaonekana yupo tayari kufanya biashara au unataka kumpa msaada kwa sababu ya urafiki wenu? Pia ukija naye Dar ujue ni mzigo mwingine unakuja kuongeza. Sisemei mzigo kwenye gharama za matumizi wala chakula ila mzigo kwenye kumanage muda wako na yeye. Maana wewe utatumia muda wako kwake ili awe sawa. Je uko tayari kutumia muda wako kwa ajili yake na mambo yakawaenda sawa?

Ngoja niende NIDA nikasake kitambulisho cha Uraia kwanza.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Back
Top Bottom