Jana nilimuona ITV anaisifia CHADEMA "eti" hainaga longolongo kwenye chaguzi zake!
Sina uhakika alikua wapi, kwa kuwa ni Mwanasheria, nadhani alikuwa anajishughulisha na Kampuni yake ya Uwakili. Kampuni yake imwjuipenyeza Uingereza na ina soko kubwa tu kule. Ila kitu kimoja ninachikifahamu, Mwalimu Nyerere aliuchukia Ubepari wa Mkono, hivyo wakati ule asingeweza kupenya kwenye shughuli za Siasa!Hi wakati wa ujio wa vyama vingi Mkono alikuwa wapi?
There is no FUTURE for CCM, there is only PAST & PRESENT;
Kiranga na hapo ulipouliza ndipo tatizo lilipo haswaa!Mkuu Nguruvi3 uchambuzi mwingine mzuri sana. Umenikumbusha mambo mengi hasa kuhusu reforms ambazo tulikuwa tunategemea kuletwa na Secretariat mpya baada ya ile ya Makamba kuenguliwa na kuingia Mkama na akina Nape na Mwigulu. Ukweli inaonekana kana kwamba Katibu Mkuu Mkama amekata tamaa na ameamua kukaa kimya kama vile hayupo. Afdahali hata wakati wa Makamba kwa kuwa alikuwa akipiga vikelele.
Sasa mkuu inaonekana matycoon wamekimiliki Chama, utawaondoaje ili kuleta mageuzi? Naona kama ndio sasa wanataka kujiimarisha kwenye vyombo vya maamuzi ndani ya Chama.
Mkuu Kiranga, tycoons hawana ndoto za CCM kuondoka madarakani. Wao wanafahamu kuwa salama yao ni CCM ibaki madarakani.Mkuu Nguruvi3 kwa mara nyingie umefunguka vizuri. Nimekuelewa na nimejua tatizo. Hakika product life cycle inainyemelea CCM. Je CCM ikitoka madarakani hao tycoon watakuwa salama bila serikali ya CCM? Wao hawalioni hili hadi wakiingize Chama ICU? Au wao wana strategy nyingine kwa ajili ya kulinda maslahi yao?
Shukrani sana kwa Mchambuzi na Nguruvi kwa kutoa uchambuzi unaonyesha weledi wa mambo ya kisiasa unaoendelea katika nchi yetu.Vilevile nakushukuru mtoa hoja iliyochochea mjadala Kimbunga,hakika mjadala huu unajadili issue sio watu kama mijadala mingi inayoendelea hapa JF.
Well said Kimbunga. Baada ya uchaguzi wa CCM utaona mambo yatakavyobadilika. Itategemea mwelekeo ukoje, nakuhakikishia kuwa kutakuwa na wimbi kubwa sana la wananchama kuhama na tycoons kutafuta maeneo salama. Hawataweka wazi kuwa wametosa chama bali watakuwa na ushiriki usio rasmi katika vyama vyote ili kujenga mazingira ya 'mimi ni mwenzenu pia'.Wakibahatika kukimiliki chama tutarajie inflation ya hali ya juu sana kati ya mwakani na 2015 kwasababu wataingiza pesa zote za 'uswiss' katika mzunguko wakati wakijiandaa.Mkui Nsaji Mpoki hata mimi nafarijika sana na weledi wa akina Mchambuzi na Nguruvi3. Mjadala huu umejikita zaidi katika issues na siyo watu. Hakika umekuwa ni mjadala mzuri usio na matusi wala kejeri bali kuonyesha weledi wa siasa hasa siasa ndani ya CCM. Lakini inaweza kwenda zidi ya siasa ndani ya CCM tu bali ikawa ni reflection ya siasa ndani ya vyama vya siasa nchini. Hao ma tycoon wameishakula nyama ya watu hivyo hawezi kuacha. Wakishindwa na CCM bahati mbaya ikapoteza uongozi wa nchi nadhani hawatakaa kimya tu wateketee na wao wawe historia kama CCM, wao nadhani watatafuta pa kuegemea ili kulinda maslahi yao. Hakuna pengine pa kuegemea bali kujiingiza katika chama cha siasa ama hata kuanzisha chama chao ili waweze kuwa madarakani. Siwaoni kwamba basi utakuwa ndio mwisho wao wakati siasa za nvhi zinaemdelea
Mkuu Mchambuzi nashukuru kwa hoja mujarabu. Nilijua tu nitapata kitu toka kwako. Umenena vyema kuhusu matycoon wa CCM ambao inaonekana ndio wanakivuruga chama. Lakini nakumbuka kwamba matycoon walikuwepo tangia enzi za TANU wakichangia Chama lakini hawakuwa wakikemea na kuvuruga chama. Hivi watu kama akina Rupia enzi hizo si walikuwa matycoon ambao walifikia hata kumapatia mwalimu nauli ya kwenda UNO pamoja na kumpangia nyumba ya kuishi jijini lakini hawakuwa na makeke kama haya? Akina Al nuur Kasum vipi wao hawakuwa wachangiaji wa chama kweli?
Haya tukija miaka ya tisini ndipo hapo nakumbuka wale pace makers nao waliamua kuingia kwenye chungu kuona kuna nini humo. Kumbuka yule pace maker wa Ifakara akiitwa Abbas Gulamali na akina Biku mbona wao hawakuwa kama hawa wa sasa? Nadhani kuna shida nyingine kubwa zaidi ya huu utycoon. Hivi tunaweza kusema kwamba CCM ina mkemeaji ambaye anaweza kusimama na kukemea na watu wakamsikia siyo kwa ukali wa sauti yake bali kwa historia na usafi wake?
Nakubaliana na wewe. After all, Mkono ni mwizi tu na yeye. Acha aenguliwe akafilie mbali.Acha aenguliwe tu. Who cares?