Nimrod Mkono aitisha CCM

CCM tutatangatanga na kubembelezana mpaka lini juu ya watu kama hawa akina Mkono. Humu yamesemwa mengi juu yake ya UONGO usababishao tabasamu (a lie that draws a smile) kama vile:

1. Kwamba ana nguvu sana kifedha kiasi kwamba hakuna anayeweza kumfanya chochote ktk Chama wala Serikali ni uongo unaofurahisha. Fedha za kifisadi huendelea kuwepo pale anapoendelea kuruhusiwa kutufisadi. Kata bomba la malipo makubwa ya kesi anazosimamia mf. dhidi ya IPTL na apewe kibano cha kodi juu ya biashara zake; mbona ni wa kawaida sana?

2. Kwamba ana siri kubwa (mbaya) za Chama / Serikali kwamba hakuna anayeweza kumfanya chochote ktk Chama wala Serikali ni uongo unaofurahisha. Apewe mic na aseme analolijua mapema ili aturahishishie mchakato wa kumvua kama gamba na yeyote waliyeshirikiana naye katika ufisadi wowote maana hakuna mtu ambaye ni indispensable.

3. Kwamba anapendwa sana wa wananchi wa eneo lake ni uongo unaofurahisha. Adhibitiwe katika kutoa rushwa wakati wa uchaguzi hata jina tu kupita ili agombee halitatoka! Na wananchi sasa wameshamshutukia kipindi kichacho wako tayari kula kwake na kumnyima kura!

Lakini, yapo ambayo pia yaliyosemwa au hayajasemwa ambayo ni UKWELI udondoshao chozi (the truth that draws a tear) kama vile:

1. Ni fisadi. Hata baba wa taifa (J. K.Nyerere) hakumpenda tokana na kutokuwa na uadilifu na Butiama yote hili linajulikana; ingawa leo anaweza kujitanabisha (kwa vijana wa leo) kuwa alikuwa karibu sana na baba waTaifa.

2. Hana kabisa sifa za uongozi maana mtu anayetanguliza fedha mbele kununua haki au kupata umaarufu ni hatari sana. Je ni mara ya kwanza kusikia kuwa Mkono kanunua mgombea wa upinzani ili apate mteremko? Aidha ana tabia ya kulazimisha agenda zake binafsi bila kujali taratibu zilizokubalika popote iwe katika Halmashauri au Mkoani kwake. Ushirikiano wake na Wabunge wenzake ni hafifu sana. Aidha uwezo wake wa kuchambua mambo na kutoa maamuzi ni wa mashaka pia. Fanyenyeni uchunguzi, ukisikia analia, ujue kaguswa mahala ambapo alipakumbatia kwa maslahi yake binafsi na si ya Taifa.

Huu si wakati za zama zile; ni kizazi tofauti kabisa ambacho si fedha yako, wala wafadhili wako, wala kiburi kitakachokuweka madarakani katika ngazi zozote bali sifa za ukweli zinazokubalika na nguvu za umma. CCM haiwezi kuendelea kutangatanga kuendelea kusimamisha wababaishaji wasio na sifa na mwendo ndio huo hata katika nafasi ya Urais. Atasimamishwa yule msiyemtegema asiyetajwa jina lake sasa na wa ukweli.

Endapo, Mh. Mkono anaona katoswa asitoe vitisho basi ajitose mapema kuelekea anakostahili. Kuwapa watu wa namna hii nafasi yoyote hata za ujumbe ni kuendeleza mkakati wa kuiua CCM kitu ambacho hakikubaliki and this is the truth that draws a tear!
 
Hi wakati wa ujio wa vyama vingi Mkono alikuwa wapi?
Sina uhakika alikua wapi, kwa kuwa ni Mwanasheria, nadhani alikuwa anajishughulisha na Kampuni yake ya Uwakili. Kampuni yake imwjuipenyeza Uingereza na ina soko kubwa tu kule. Ila kitu kimoja ninachikifahamu, Mwalimu Nyerere aliuchukia Ubepari wa Mkono, hivyo wakati ule asingeweza kupenya kwenye shughuli za Siasa!
 
Hawawezi kumuengua kwa sababu yeye ni mmojawapo wa Wahisani wakuu wa chama ndio maana anajiamini kuwa hilo hawaliwezi.
 
There is no FUTURE for CCM, there is only PAST & PRESENT;

Bro,...a ton and a half statement, naona umedhamiria sasa! Lakini je, wenzako ThinkTank-CCM watakubaliana na hoja hii? Na je, wafanye nini ili njozi za uwepo wa 'future' zirejee? Je, muda unawatosha, au ni baada ya 2015?
 
Kiranga,
Mkono anaongea kwa jeuri kwasababu anajua kila kitu kuhusu CCM ikiwa ni pamoja na viongozi wake. Mfano, utaongea nini kuhusu Meremeta, Richmomd ambacho mkono hakijui?
Yupo mchangiaji aliyesema jumuiya ya wazazi haina nguvu. Inaweza kuwa kweli jumuiya haina nguvu, lakini ieleweke mkono anataka 'access' katika vyombo vinavyofanya maamuzi.

Jumuiya ya wazazi ina wawakilishi katika CC na NEC kwahiyo anachotaka Mkono ni kuwa na access iwe yeye au mtu wake wa kuleta habari. Ndio maana akaamua kujielekeza huko. The point is, he would like to remain within the 'inner circle'.

Mchambuzi, nakubaliana nawe kuwa chama kimekuwa cha tycoon na kupoteza ile maana halisi ya chama cha siasa.
Nisipokubalina nawe ni kuwa CCM inatakiwa ifanye reform ndani ya chama hasa jumuiya zake sambamba na chaguzi.

Utakumbuka kuwa watu kama Nape waliingia kwa nia hiyo, na unakumbuka kuundwa kwa tume ya Wilson Mukama ilikuwa ni kwa nia hiyo. Utakubaliana nami kuwa wote wenye kutaka kuleta mabadiliko wamesalimsu amri.
Mukama ambaye ndiye alitakiwa aongoze mageuzi inaonekana kama amebwaga manyanga, na kijana Nape ndio ameachana na mageuzi na kutafuta adui wa badnia CDM ilimradi kibarua kiendelee.

Kushindwa kwao ni kutokana na tycoons kumiliki sehemu kuu za maamuzi ya chama. Ni ukweli kuwa wote wanaotakiwa kufanya mageuzi wamekalia kuti kavu kama tunavyoona guko NEC wanavyosakamwa.

Ninachotaka kusema hapa ni kuwa huwezi kufanya reform au kuwa na chaguzi za maana tycoon wakiwa ndani ya chama.
Ili CCM irudi kwenye mstari ni lazima hawa tycoon waondolewe kwanza ili kuruhusu reform na mengineyo kuendendelea.
Midhali wapo ndani ya chama basi chaguzi ni zao na umiliki wa chama ni wao, na hapo hakuna jingine ila 'natural death'

Yupo mchangiaji ameuliza mbona 'tycoon' wamekuwepo kuanzia TANU na hakukuwa na tatizo?
Ikumbukwe kuwa enzi hizo chama kilishika hatamu na tycoon walichangia kama sehemu ya kujisalimisha.
Sikuhizi wanachangia ili kumiliki chama, kwamba chama kimejisalimisha kwao.

Kwanini imetokea hivyo? Jibu rahisi ni kuwa ukiwa na uongozi uliojengwa katika mazingira ya rushwa hakuna misingi ya uongozi au uadilifu. Ni 'chain of command ya corruption' inayofanya kazi i.e tumetumia pesa kukuweka, sasa tumika kutulinda.
 
Mkuu Nguruvi3 uchambuzi mwingine mzuri sana. Umenikumbusha mambo mengi hasa kuhusu reforms ambazo tulikuwa tunategemea kuletwa na Secretariat mpya baada ya ile ya Makamba kuenguliwa na kuingia Mkama na akina Nape na Mwigulu. Ukweli inaonekana kana kwamba Katibu Mkuu Mkama amekata tamaa na ameamua kukaa kimya kama vile hayupo. Afdahali hata wakati wa Makamba kwa kuwa alikuwa akipiga vikelele.

Sasa mkuu inaonekana matycoon wamekimiliki Chama, utawaondoaje ili kuleta mageuzi? Naona kama ndio sasa wanataka kujiimarisha kwenye vyombo vya maamuzi ndani ya Chama.
 
Last edited by a moderator:
Hawezi kufanya chochote, ataenguliwa na atatulia kimya. Yeye bora aendelea na biashara zake kuliko kuleta domo domo.
 
Mkuu Nguruvi3 uchambuzi mwingine mzuri sana. Umenikumbusha mambo mengi hasa kuhusu reforms ambazo tulikuwa tunategemea kuletwa na Secretariat mpya baada ya ile ya Makamba kuenguliwa na kuingia Mkama na akina Nape na Mwigulu. Ukweli inaonekana kana kwamba Katibu Mkuu Mkama amekata tamaa na ameamua kukaa kimya kama vile hayupo. Afdahali hata wakati wa Makamba kwa kuwa alikuwa akipiga vikelele.
Sasa mkuu inaonekana matycoon wamekimiliki Chama, utawaondoaje ili kuleta mageuzi? Naona kama ndio sasa wanataka kujiimarisha kwenye vyombo vya maamuzi ndani ya Chama.
Kiranga na hapo ulipouliza ndipo tatizo lilipo haswaa!
Labda nikumbushe kuwa hizi mbio za NEC, jumuiya za chama n.k. ni sehemu ya kujipanga.
Haitoshi tu kuwa mjumbe wa NEC ili mtu awe salama. Ni lazima awe na kundi litakalosimama naye. Hapo ndipo unaona fedha inapofanya kazi kwa sasa huko UVCCM, Wazazi, UWT n.k

Kosa kubwa walifanya CCM miaka mitano iliyopita. Ilipobainika kuwa chama kimetekwa nyara na tycoons, 'vijana' watiifu wa mwalimu waliiomba kikao cha NEC kifanyike Butiama ili kuondoa 'mzimu' unaokitafuna chama.
Katika kikao kile kulikuwa na kila ushahidi wa kuwatuhumu na kuwahukumu wanaokichafua.

Nakumbuka wazee walliamu vinara wa genge hilo wafukuzwe uanachama. Ile ndio ilikuwa nafasi pekee iliyojitokeza ya kusafisha chama ili mageuzi yafanyike. Mwenyekiti alikataa si kwasababu ya masilahi ya chama ni kwasababu wote waliopaswa 'kuchinjiliwa baharini' ndio waliompa huo uenyekiti.

Ni baada ya kosa kosa hiyo tycoon wakapata mwanya wa kuwarudi wanaoleta 'vurugu' dhidi yao.
Kwa bahati mbaya wale waliotaka kusafisha chama hawana nguvu ndipo tukashuhudia wabunge wakitoswa kiaina.
Hilo tu likavunja nguvu ya wapigania mgeuzi na wale waliojaribu wameshapewa onyo.

Unakumbuka pia NEC iliyopita ilitaka mageuzi ndani ya sekretariati mpya. Maana ya hii ni kuwa umiliki wa tycoon haukuwa kamilifu na wanataka kuhodhi kila kitu kwa asilimia mia moja. Na ili kuhakikisha kuwa hakuna mabaki ya Nyerere ndani ya chama chao, vijana wa Mwalimu wameundiwa kitu kinaitwa baraza la ushauri. Baraza hili halina nguvu ya kisheria ndani ya chama. Kwa utaratibu huo safisha safisha imekamilika, sasa hivi tycoons wanajpanga katika maeneo muhimu 'strategic position' ili kukidhibiti chama kikamilifu kuanzia bungeni, ndani ya chama na serikali.

Kwasasa hivi hakuna njia ya kukisafisha chama ndio maana nasema kitakachoisafisha CCM ni 'natural death'
Historia inafundisha kuwa vyama vilivyoondoka madarakani kwa mtazamo wa kiCCM kama KANU, UNIP vimetokomea katika ulimwengu wa siasa.

Pamoja na hayo kuna nafasi moja tu ndogo iliyobaki. Wazee wa chama kusimama kidete.
Hili ni gumu lakini likifanyika mapema na kumshinikiza mwenyekiti ambaye ni kikwazo kingine cha mageuzi, wanaweza kurudi 'mwaisela' . Kwasasa wapo ICU wanapumulia mashine.
 
Mkuu Nguruvi3 kwa mara nyingie umefunguka vizuri. Nimekuelewa na nimejua tatizo. Hakika product life cycle inainyemelea CCM. Je CCM ikitoka madarakani hao tycoon watakuwa salama bila serikali ya CCM? Wao hawalioni hili hadi wakiingize Chama ICU? Au wao wana strategy nyingine kwa ajili ya kulinda maslahi yao?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 kwa mara nyingie umefunguka vizuri. Nimekuelewa na nimejua tatizo. Hakika product life cycle inainyemelea CCM. Je CCM ikitoka madarakani hao tycoon watakuwa salama bila serikali ya CCM? Wao hawalioni hili hadi wakiingize Chama ICU? Au wao wana strategy nyingine kwa ajili ya kulinda maslahi yao?
Mkuu Kiranga, tycoons hawana ndoto za CCM kuondoka madarakani. Wao wanafahamu kuwa salama yao ni CCM ibaki madarakani.

Tycoons wameshafanya jaribio la pesa na limefanikiwa sana. Chaguzi za mwaka 2000 zilizomrudisha BWM madarakani zilikuwa ni mwanzo wao wa kujipanga. Wkafanya hivyo 2005 na kuingiza 'jeshi lao' NEC, CC na Bungeni kwakutumia rasilimali zao za pesa. Bado wanaamini kuwa kikwazo kikubwa ni ndani ya chama,huko nje wanajua pesa itafanya kazi ya kununua kila kitu. Kwa upande wao wakidhibiti chama mambo mengine yatakwenda yenyewe kwasababu uwezo upo, nyenzo zipo na watu wao wapo.

Kuna nyakati tycoons wapo njia panda, kwamba wakubali mageuzi ndani ya chama ili watoswe au watumie silaha yao ya mwisho hadi watakaponyang'anywa na kuwa mateka! Hili la kukubali yaishe wakiwa na silaha mikononi si hawalikubali, na lile la kupigana hadi risasi ya mwisho ndilo linalofanyika sasa hivi katika vinyang'anyiro vya NEC

Wanachokisahau ni kwamba nchi imebadilika na wananchi wanayaona, kuyasikia na kuyasoma mabaya yao yote.
KANU walionywa na hawakusikia kilichowapata tunakijua. Leo KANU imebaki maktaba kama sehemu ya historia.

Wanachoamini ni kuwa hakuna nguvu kubwa zaidi ya pesa! na kikwazo cha mwanzo ni ndani ya chama wakivuka hicho wataweza mengine. Wanayo mifano kama walivyoweza ku-survive Richmond, Kagoda, Meremeta, Dowans, Maliasili n.k.
Wanafahamu kuwa kwa wao kuwa ndani ya chama chenye serikali tawala kelele zote zimezimwa kuanzia serikalini hadi bungeni. Wananchi wa Tanzania ni wapole hata kama anakwenda hospitali kwa ugonjwa wa kukosa lishe, ukimwambia 'Mambo' atakujibua Poa sana. Tycoons wanategemea kuwa nje ya chama pesa itaweka mambo poa yawe pooooa zaidi.
 
Shukrani sana kwa Mchambuzi na Nguruvi kwa kutoa uchambuzi unaonyesha weledi wa mambo ya kisiasa unaoendelea katika nchi yetu.Vilevile nakushukuru mtoa hoja iliyochochea mjadala Kimbunga,hakika mjadala huu unajadili issue sio watu kama mijadala mingi inayoendelea hapa JF.
 
Shukrani sana kwa Mchambuzi na Nguruvi kwa kutoa uchambuzi unaonyesha weledi wa mambo ya kisiasa unaoendelea katika nchi yetu.Vilevile nakushukuru mtoa hoja iliyochochea mjadala Kimbunga,hakika mjadala huu unajadili issue sio watu kama mijadala mingi inayoendelea hapa JF.

Mkui Nsaji Mpoki hata mimi nafarijika sana na weledi wa akina Mchambuzi na Nguruvi3. Mjadala huu umejikita zaidi katika issues na siyo watu. Hakika umekuwa ni mjadala mzuri usio na matusi wala kejeri bali kuonyesha weledi wa siasa hasa siasa ndani ya CCM. Lakini inaweza kwenda zidi ya siasa ndani ya CCM tu bali ikawa ni reflection ya siasa ndani ya vyama vya siasa nchini. Hao ma tycoon wameishakula nyama ya watu hivyo hawezi kuacha. Wakishindwa na CCM bahati mbaya ikapoteza uongozi wa nchi nadhani hawatakaa kimya tu wateketee na wao wawe historia kama CCM, wao nadhani watatafuta pa kuegemea ili kulinda maslahi yao. Hakuna pengine pa kuegemea bali kujiingiza katika chama cha siasa ama hata kuanzisha chama chao ili waweze kuwa madarakani. Siwaoni kwamba basi utakuwa ndio mwisho wao wakati siasa za nvhi zinaemdelea.
 
Last edited by a moderator:
Mkui Nsaji Mpoki hata mimi nafarijika sana na weledi wa akina Mchambuzi na Nguruvi3. Mjadala huu umejikita zaidi katika issues na siyo watu. Hakika umekuwa ni mjadala mzuri usio na matusi wala kejeri bali kuonyesha weledi wa siasa hasa siasa ndani ya CCM. Lakini inaweza kwenda zidi ya siasa ndani ya CCM tu bali ikawa ni reflection ya siasa ndani ya vyama vya siasa nchini. Hao ma tycoon wameishakula nyama ya watu hivyo hawezi kuacha. Wakishindwa na CCM bahati mbaya ikapoteza uongozi wa nchi nadhani hawatakaa kimya tu wateketee na wao wawe historia kama CCM, wao nadhani watatafuta pa kuegemea ili kulinda maslahi yao. Hakuna pengine pa kuegemea bali kujiingiza katika chama cha siasa ama hata kuanzisha chama chao ili waweze kuwa madarakani. Siwaoni kwamba basi utakuwa ndio mwisho wao wakati siasa za nvhi zinaemdelea
Well said Kimbunga. Baada ya uchaguzi wa CCM utaona mambo yatakavyobadilika. Itategemea mwelekeo ukoje, nakuhakikishia kuwa kutakuwa na wimbi kubwa sana la wananchama kuhama na tycoons kutafuta maeneo salama. Hawataweka wazi kuwa wametosa chama bali watakuwa na ushiriki usio rasmi katika vyama vyote ili kujenga mazingira ya 'mimi ni mwenzenu pia'.Wakibahatika kukimiliki chama tutarajie inflation ya hali ya juu sana kati ya mwakani na 2015 kwasababu wataingiza pesa zote za 'uswiss' katika mzunguko wakati wakijiandaa.
Tishio lingine ni ujio wa katiba mpya hili tycoons wanaliangalia kwa umakini sana kwasababu katiba hiyo inaweza kuja na mambo yatakayoharibu 'mipango yote'. Ngoja tusubiri tume zitakapoingia katika majiji na miji mikubwa yenye ushawaishi wa kisiasa tusikie maoni yao.
 
Mkuu Mchambuzi nashukuru kwa hoja mujarabu. Nilijua tu nitapata kitu toka kwako. Umenena vyema kuhusu matycoon wa CCM ambao inaonekana ndio wanakivuruga chama. Lakini nakumbuka kwamba matycoon walikuwepo tangia enzi za TANU wakichangia Chama lakini hawakuwa wakikemea na kuvuruga chama. Hivi watu kama akina Rupia enzi hizo si walikuwa matycoon ambao walifikia hata kumapatia mwalimu nauli ya kwenda UNO pamoja na kumpangia nyumba ya kuishi jijini lakini hawakuwa na makeke kama haya? Akina Al nuur Kasum vipi wao hawakuwa wachangiaji wa chama kweli?

Haya tukija miaka ya tisini ndipo hapo nakumbuka wale pace makers nao waliamua kuingia kwenye chungu kuona kuna nini humo. Kumbuka yule pace maker wa Ifakara akiitwa Abbas Gulamali na akina Biku mbona wao hawakuwa kama hawa wa sasa? Nadhani kuna shida nyingine kubwa zaidi ya huu utycoon. Hivi tunaweza kusema kwamba CCM ina mkemeaji ambaye anaweza kusimama na kukemea na watu wakamsikia siyo kwa ukali wa sauti yake bali kwa historia na usafi wake?

Mkuu Kimbunga,

Ni kweli CCM ilikuwa na wachangiaji watanzania (WEUSI) huko nyuma lakini pia wenye asili ya kiasia; Lakini uchangiaji ule ulikuwa zaidi katika hatua za mapambano dhidi ya ukoloni ambapo watanganyika walihitaji kujitolea kwa hali na mali kufanikisha project ya independence; pia miaka y amwanzo ya uhuru, kulikuwa na wachangiaji wa namna nyingi (weusi, lakini hasa wahindi) katika hatua za mwanzo za TANU kuzidi kujiimarisha na baada ya kushika hatamu, hasa katika kipindi cha Ujamaa hadi miaka ya mwanzo ya tisini, CCM iliweza kujiendesha kupitia njia nyingine mbalimbali, lakini hasa kwa kutegemea fedha kutoka serikalini na pia kutoka kwa marafiki wa Ujamaa waliokuwa nje ya Tanzania;

Suala la Abbas Gulamali na wengine, uwepo wa Nyerere in my view ulisaidia sana kupunguza vituko tunavyoviona sasa, kwani Nyerere alikuwepo na alikemea sana mienendo ya ajabu ajabu iliyokuwa inakivuruga chama, kila ilipokuwa inajitokeza;

Kuhusu CCM kuwa na kiongozi mwenye moral authority, ni dhahiri mtu wa namna hiyo hatunae tena baada ya Nyerere kuondoka; kiongozi kuwa na moral authority maana yake ni kwamba kauli au tamko lake juu ya masuala ya maadili na uadilifu kuhusu mwenendo wa siasa za nchi, ina mamlaka ambayo yanatambulika na kukubalika na wananchi wengi, hasa katika mtazamo wa masuala yaliyo over and above politics; kiongozi wa namna hiyo ni lazima akubalike na makundi yote ya jamii bila ya kujali tofauti za kidini, kabila, jinsia, kipato,au political orientation; mtu wa namna hiyo lazima aheshimike, na aungwe mkono na walio wengi kwa mtazamo wa kitaifa zaidi kuliko kitu kingine chochote; baada ya kuondoka Nyerere, hata moral authority ya CCM kitaasisi imemomonyoka; haya hasa ni matokeo ya chama kuchafuka kwa rushwa/ufisadi, lakini muhimu zaidi chama ku-betray historia yake yenyewe; Hivi sasa ni vigumu kwa mtu kupinga hoja kwamba CCM imepoteza both Moral authority na Political legitimacy;

CCM is a cookie that crumbles; Chama hakiwezi tena kujinasua kutoka kwenye maporomoko ya sasa katika anga za siasa; kinachoiweka CCM madarakani sasahivi ni RULE BY LAW (sio RULE OF LAW) na pia vyama vya upinzani (hasa Chadema), kutokuwa na dira mbadala ya taifa inayo inspire watanzania walio wengi, hasa vijijini; Kitendo cha CCM kupita kwenye kampeni na kutamka majukwaani itajenga barabara na Chadema kufuata muda mchache baadae na kusema itatoa elimu bure msingi hadi chuo kikuu haitoshi;
 
Back
Top Bottom