NIMR yagundua dawa ya UKIMWI, Tezi dume

NIMR yagundua dawa ya UKIMWI, Tezi dume

lukelo sakafu

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2015
Posts
2,938
Reaction score
517
Taasisi ya taifi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) imepiga hatua zake na kuweza kupata dawa itayoweza kutibu magonjwa hatari ya UKIMWI,tezi dume,maleria na baadhi ya magonjwa nyemerezi.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wake Dr.Mwele Malecela na kwamba NIMR ipo kwenye hatua za mwisho mwisho hili dawa hiyo ipatiwe jina na kuingizwa sokoni kwa matumizi ya binadamu.

Hatua hii itasaidia kupunguza maambukizi dhidi ya haya magonjwa hatari. karibuni jamvini.


Alisema miongoni mwa tafiti ambazo ziliwafanya wafanikiwe ni pamoja na utafiti wa majaribio ya chanjo ya ukimwi na malaria nchini.

Alisema katika utafiti wa chanjo ya ugonjwa wa Ukimwi, taasisi hiyo ilishiriki katika tathmini ya upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya na majaribio ya tiba ya virusi vya HSV-2(Herpes Simplex Virus2) katika kupunguza maambukizi ya Ukimwi.

"Pia tulifanikiwa kupata dawa ya usugu ya kurefusha maisha kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi(VVU).

"Tulifanikiwa kufanya uchunguzi wa vimelea vya Ukimwi katika maziwa ya mama anayenyonyesha,"alisema.

Chanzo: Mtanzania
 
Kwahiyo condom zitapigwa kibuti na hela ya kununua dawa inaandaliwa kabisa
 
taasisi ya taifi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (nimr) imepiga hatua zake na kuweza kupata dawa itayoweza kutibu magonjwa hatari ya ukimwi,tezi dume,maleria na baadhi ya magonjwa nyemerezi.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wake dr.mwele malecela na kwamba nimr ipo kwenye hatua za mwisho mwisho hili dawa hiyo ipatiwe jina na kuingizwa sokoni kwa matumizi ya binadamu.

Hatua hii itasaidia kupunguza maambukizi dhidi ya haya magonjwa hatari. Karibuni jamvini.
fitina ya kibiashara itahusika
trade mark etc
 
Taasisi ya taifi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu (NIMR) imepiga hatua zake na kuweza kupata dawa itayoweza kutibu magonjwa hatari ya UKIMWI,tezi dume,maleria na baadhi ya magonjwa nyemerezi.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wake Dr.Mwele Malecela na kwamba NIMR ipo kwenye hatua za mwisho mwisho hili dawa hiyo ipatiwe jina na kuingizwa sokoni kwa matumizi ya binadamu.

Hatua hii itasaidia kupunguza maambukizi dhidi ya haya magonjwa hatari. karibuni jamvini.

NIMRI ipi? Ile inayochakachua data? Waje humu watupe published evidence, e.g kati ya wagonjwa 1,000 waliojaribiwa 987 wamepona.
 
NIMRI ipi? Ile inayochakachua data? Waje humu watupe published evidence, e.g kati ya wagonjwa 1,000 waliojaribiwa 987 wamepona.

Kwa nini badala ya kusubiri hapa tusiwafuate kwenye tovuti yao?!
 
Title imekaa vibaya...hakuna ugunduzi wa hiyo dawa. Rudia
 
NIMRI imeshirkishwa kimataifa kufanya utafiti dawa ya ukimwi. Si yake. Acheni siasa
 
Nimr haina wataalam wenye uwezo huo....kila mtu pale anawaza pesa, hakuna scientist hata mmoja aliyeko pale mwenye uwezo wa kufikiri hata dawa ya maralia....
 
Nimr haina wataalam wenye uwezo huo....kila mtu pale anawaza pesa, hakuna scientist hata mmoja aliyeko pale mwenye uwezo wa kufikiri hata dawa ya maralia....

kwa hiyo unamaanisha pale kuna vilaza tu
 
mwele-malecela25.jpg

Dr. Mwale Malecela

TAASISI ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), imetengeneza dawa za asili zilizoboreshwa kwa ajili ya tiba kwa magonjwa mbalimbali, ikiwemo Ukimwi baada ya kuzifanyia utafiti kubaini uwezo na usalama wake.



Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Dk Mwele Malecela amesema iko katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa dawa asilia 11 ziingizwe sokoni.


Magonjwa mengine ambayo dawa hizo zilizoboreshwa zitatumika kwa ajili ya tiba ni kisukari na kupunguza mafuta (lehemu) mwilini, uvimbe wa tezi dume kwa wanaume na dawa inayoongeza nguvu za kijinsia kwa wanaume.


Dk Mwele alisema hayo jijini Dar es Salaam jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miaka 35 ya utafiti na maendeleo ya afya na kusema tafiti katika tiba asilia zilifanyika kubaini uwezo na usalama wa dawa hizo zinazotumiwa na jamii mbalimbali hapa nchini.


“Aidha taasisi imefanya utafiti kwa kuzingatia uwezo na usalama kwa watumiaji na kufanikiwa kutengeneza dawa asili zilizoboreshwa kwa ajili ya tiba kwa magonjwa ya malaria, Ukimwi na magonjwa nyemelezi, ugonjwa wa ini, shinikizo la damu…,” alisema.


Alisisitiza, “taasisi iko katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wa dawa asilia 11 ili ziweze kuingizwa sokoni.”


Akizungumzia tatizo la kupungua kwa nguvu za kiume, alisema linaonekana ni kubwa na hata katika maonesho wanayofanya, dawa inayoimarisha nguvu hizo hununuliwa zaidi.


Aidha alisema iko haja kwa wadau na serikali kuwekeza nguvu zaidi katika taasisi hiyo kufanya tafiti zitakazosaidia kugundua chanzo na tiba ya tatizo la uvimbe kwa matumbo ya uzazi ya wanawake wengi wenye asili ya kiafrika.


Kuhusu ugonjwa wa malaria, Dk Mwele alisema matokeo ya tafiti yanaonesha kupungua maeneo ya Kaskazini, Kaskazini-Mashariki, Kanda ya Kati na Kanda ya Ziwa Victoria kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya vyandarua na uelewa wa wananchi juu ya utunzaji wa mazingira.


Alisema utafiti wa chanjo ya malaria uliofanywa katika wilaya za Bagamoyo na Korogwe umeonesha uwezo mkubwa wa kinga kwa watoto.


Alisema taasisi inaendelea kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Kupitia Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria kufuatilia na kutathmini usugu wa mbu dhidi ya viuatilifu vinavyotumika katika vyandarua na katika kunyunyizia ukoko kwenye nyumba.


Alisema taasisi imeendelea kuishauri Serikali katika kuainisha mbinu sahihi za kupambana na usugu huo ambapo pia matokeo ya tathmini za ubora wa dawa za tiba ya malaria yameonesha kuwa dawa mseto ya ALU bado inao uwezo mkubwa wa kutibu ugonjwa wa malaria.

Chanzo:Habarileo
 
chanzo habari leo!!!!spinning hiyo kututoa kwenye miswada kandamizi inayopelekwa kwa hati ya dharura...mambo ya samunge!!!!
 
Kila kukiwa na mambo yabayogusa taifa hawakosi kuja na mbinu kuwaondoa watu kwenye mjadala,sasahivi tupo kwenye swala la daftari lawapiga kula na uchaguzi mkuu,au ni kick kwa kuwa hiyo kazi imeshindikana tusahau?
 
Back
Top Bottom