Mdogo wako ana umri gani kwani? Muite mwambie hukupendezewa na ulichokiona, mkanye umpe hasara za hao vijana, kama anasoma umsisitizie kukazania masomo, mkumbushe kuhusu mimba na maradhi, usitumie hasira ila kuwa serious katika hayo maongezi, ukimaliza mfate yule kijana kaa nae umfahamishe kuwa hutapenda kumuona tena akiwa na mdogo wake, siku ukimuona utamfungulia kesi n.k. vitisho vya kawaida mpe, huyo mvulana mpe mkwara wa kisawa sawa, ila dada ongea nae kwa busara, mana sie watoto wa kike ukiongea kwa hasira ndo kama atakukomoa Zaidi kwa ulivyompiga au kumtukana yani ni kama unampa ujasiri wa penzi lake, ila ukiongea nae kwa busara kumuonyesha kiasi gani unampenda na hutaki aibu yoyote ataona huruma, na kuwaza mazuri unayomfanyia na upumbavu anaofanya, atajirekebisha na kuwa makini, na usione aibu kumeeleza anadeserve wanaume wa aina gani, mponde huyo kijana wake n.k.