mie nimeingiwa na huruma...msamehe,mwache aendelee na kazi atakuwa amejifunza...nakusihi usimrudishe anaweza ht kujiua...
hahahaa ila hapo uliposema ulimuona anatoka chumbani kwa kaka yako ulinichanganya kidogo,almanusura nianze kumlaumu yeye ndio anampa kiburi hapo kwenu kwa kuduu naye..LOL :A S 13::A S 13::wink2::wink2:
Kinacho nishangaza ukikaa nao vizuri ndo wanakudharau, kule wanako teswa ndo wanadumu.
Samahani mamushka, lakini huyo mtot ulimuweka hapo ulitegemea yeye hahitaji ile huduma???? Mwanzoni ulimchukua akiwa mdogo hata yale mambo yetu alikuwa hajui sasa amekua bado unataka a-behave kama mtoto mdogo??? Hebu kuweni na utu kidogo, naona wote mnachangia kumpiga chini huyo binti ila jueni kuwa hata yeye ashakuwa mtu mzima hivyo anahitaji raha kama nyie. Msikilize kwanza uone may be tatizo lake lilikuwa ni ukosefu wa huduma wa muda mrefu sasa akaenda kupata kwa raha zake... Msamehe arudi nyumbani ila mwambie mdogo wako aache kumchakachua......
inaelekea huyo alitarajia kwenda kuhamia
kwa kidume lakini jamaa amemchomolea
(usishangae akiwa tayari ana kabebi kwa tumbo).
wewe msamehe na mpokee kisha hakikisha anapima ujauzito
akiwa hana ujauzito endelea nae kwani atakuwa amejifunza kwamba
vidume haviko tayari kumchukua jumla jumla hivyo atakuwa ameweka akili.
swali: kweli unaamini mdogo wako wa kiume hakujua kwamba binti aliingia
chumbani kwake? wewe ndio unamfahamu vyema mdogo wako. si vibaya
ukaangalia uhusiano wao kwani anaweza akawa nae anajipumzisha kwa huyu
binti na ndio kiini cha dharau kwani wewe ni wifi. yote yanawezekana.
Dah wafanyakazi wa nyumbani hua wanachosha wakati mwingine!!!
Ukishaona hivyo jua kuna mtu anamjaza kichwa mahala and there is no telling ni mtu wa aina gani!!
Bora umrudishe kwao mapema kabla hujapishana na pick up ikitokea nyumbani kwako!!!!
Mrudishe kwao huyo ameshalijua jiji so atakusumbua saaana tuu, vivulana vinamdanganya huyo msichana wa kazi akishakuwa na simu tu baasi kazi ndani hazitafanyika, wauza magenge, mchicha, wauza maji, akina mangi ndo wanawabadilisha hawa mabinti siku hizi hakuna wasichana wa kazi wazuri kabsaaaa
Kweli kabisa....Hawa wahudumu hata hawaeleweki. Ukienda kwa waarabu na wahindi...wanafanyakazi nyigni sana na wanakaaa muda mrefu hadi migongo inapinda...Labda kwa kuwa wanalazimishwa kunywa chai zao kwenye vikombe vidogo kama vifuniko vya bia kabla ya kuanza kazi.
Binadamu hawana jema...Achana na huruma. Rudisha binti kwa ndugu zake.
Mh ukweli inawezekana pia, ila lizzy kumbuka hata kusoma hakijui, halafu haijui dar kwani hata outing nimpaka tukitoka wote pamoja ndo tunamchukua, ila unalosema ni kweli, yaweza kua ashapata walimu.
Mamushika,
Ukicheka na nyani utavuna mabua.
Rudisha bintii kwao..ikibidi vaa bukta ufanya usafi wa nyumba yako mwenyewe. Saidiana na hao wadogo zako kazi wakati unatafuta msaidizi mwingine. Ukigeuka nyuma ujue unaweza kugeuka jiwe...utalia na kusaga meno.
Hivi lakini watu mnakuwa na huruma kiasi gani kuwapa hawa wahudumu wa kazi uhuru kwa kuchezea DSTV 100% kama vile wako likizo? Nyumbani kwangu, mwanafunzi na mhudumu wa kazi hana muda wa kuchezea TV labda vipindi maalum tu...Hata watoto wangu hawana hiyo nafasi ya kuchezea TV 100%. Inakuwaje beki tatu anakuwa kwenye TV wakati wote?
Hawa wasichana bana ukitaka akae sana usiweke mazoea sana nae mfanye rafiki mliipe kwa wakati mpe zawadi ikibidi ila mpe sheria unazotaka, na ukiona kakosea mseme kwa ukali kama unamsema mdogo wako, na baada ya hilo sahau endelea kuongea nae vizuri kama kawaida. mimi nishaona na inafanya kazi. unaweka sheria kama vile kufunga tv saa tatu au nne week end. hiyo ni nyumba yako na kila mtu anayeishi chini ya dari la nyumba yako lazima afuate sheria yako hapo utaishi kwa amani na upendo.
DC Umenipa ukweli ndugu yangu, leo ungeona wenyewe, tumegawana kazi na tukazifanya mapema tumemaliza na msosi wa moja kwa moja bila shida. Ila ulosema ni kweli hata tukipata msichana mwingine itabidi tufanye utaratibu huo wa Tv no.