Nimfanyeje mwanamke huyu?

Nimfanyeje mwanamke huyu?

Mimi ni mtanzania mwenye jinsia ya kiume nina umri wa miaka 33, nina tatizo lina nipa shida katika maisha naomba ushauri wenu wana JF. nlipata msichana ambae alikua amezalishwa na mwanmme asiyekua na msimamo wa maisha na yeye msichana akiwa kaishia kidato cha nne na matokeo mabovu....tulipendana na na huyo mwanamke nikawa na matarajio ya kufunga nae ndoa japo alikua na mtoto, ili awe mke mwenye manufaa nikajitolea kumpeleka shule akachagua chuo cha wanyama pori ambacho ni bei mbaya na kinalipiwa kwa dola, kipato changu ni kidogo ila nikajitahidi kujibana kumuandikisha hapo chuo na kutokana na kutokidhi kiwango cha kujiunga na chuo akatakiwa kuanza na Foundation course ambayo nililipa zaid ya mil. 2 akajitahidi akafaulu na kujiunga na cheti mwaka 2008, kwa bahat nzuri baba yake mdogo akasaidia kuchangia ada hadi akamaliza cheti, mungu akasaidia akapatikana mfadhali wa kumsomesha toka marekani ambapo alimlipia ada ya Diploma aliyomaliza mwaka jana,na atamsomesha DIGRII.
katika kipindi hiko chote alinifanyia vitimbi vingi ambavyo nilivivumilia kiasi kikubwa, kwan alidiriki hadi kunisaliti lakini nilisamehe na kuvumilia kwani nilijua na kuwekeza kwake kua atakua mke wangu. mwaka huu amepata ajira serikalini ana mwezi wa 6 sasa cha ajabu amekua akinifanyia vitimbi vingi japo yupo mbali na mimi ila anavionyesha mfano mdogo ni kwenye sikukuu iliyopita amtoka kwenye kituo chake cha kazi na kwenda mjini kulewa akidai amelala chumba kimoja na rafiki yake wa kike na mumewe, kifadha hana msaada na huku anajua mim kwa sasa ni mwanafunzi chuoni.
WADAU NIFANYEJE?? NIMKWAMA MKE NATAKA ILA NDIO HUYO NMECHOKA JAMANI

Binadamu tunajifunza kutokana na makosa. Kwa maelezo yako, inaonekana mchumba wako huyo hana upendo wa kweli na wewe na ndiyo maana alidiriki kukusaliti na anaendelea kukufanyia vituko bila kujali ni kwa namna gani ambavyo umehangaika kumtunza na kumsomesha. Inawezekana kabisa alikukubali kwa sababu ya shida zake, na sasa amepta elimu haoni tena umuhimu wa kuwa na wewe na hivyo anaanza vitimbwi taratibu.

Ni vyema sasa hivi ukaconcentrate na mambo yako ya chuo na kuanza kumsahahu taratibu maana dalili kubwa inaonyesha hana mpango wa muda mrefu na wewe. Si busara kuendelea kuinvest na kutegemea kuvuna kwenye shamba la aina hii, ni bora uache kulima na kutafuta shamba lingine lenye uwezo wa kutoa matunda yasiyo na sumu.

Pole na kila la kheri huko chuoni.

HP
 
Mimi ni mtanzania mwenye jinsia ya kiume nina umri wa miaka 33, nina tatizo lina nipa shida katika maisha naomba ushauri wenu wana JF. nlipata msichana ambae alikua amezalishwa na mwanmme asiyekua na msimamo wa maisha na yeye msichana akiwa kaishia kidato cha nne na matokeo mabovu....tulipendana na na huyo mwanamke nikawa na matarajio ya kufunga nae ndoa japo alikua na mtoto, ili awe mke mwenye manufaa nikajitolea kumpeleka shule akachagua chuo cha wanyama pori ambacho ni bei mbaya na kinalipiwa kwa dola, kipato changu ni kidogo ila nikajitahidi kujibana kumuandikisha hapo chuo na kutokana na kutokidhi kiwango cha kujiunga na chuo akatakiwa kuanza na Foundation course ambayo nililipa zaid ya mil. 2 akajitahidi akafaulu na kujiunga na cheti mwaka 2008, kwa bahat nzuri baba yake mdogo akasaidia kuchangia ada hadi akamaliza cheti, mungu akasaidia akapatikana mfadhali wa kumsomesha toka marekani ambapo alimlipia ada ya Diploma aliyomaliza mwaka jana,na atamsomesha DIGRII.
katika kipindi hiko chote alinifanyia vitimbi vingi ambavyo nilivivumilia kiasi kikubwa, kwan alidiriki hadi kunisaliti lakini nilisamehe na kuvumilia kwani nilijua na kuwekeza kwake kua atakua mke wangu. mwaka huu amepata ajira serikalini ana mwezi wa 6 sasa cha ajabu amekua akinifanyia vitimbi vingi japo yupo mbali na mimi ila anavionyesha mfano mdogo ni kwenye sikukuu iliyopita amtoka kwenye kituo chake cha kazi na kwenda mjini kulewa akidai amelala chumba kimoja na rafiki yake wa kike na mumewe, kifadha hana msaada na huku anajua mim kwa sasa ni mwanafunzi chuoni.
WADAU NIFANYEJE?? NIMKWAMA MKE NATAKA ILA NDIO HUYO NMECHOKA JAMANI

mapenzi hayalazimishwi, ogopa mwanamke asipokupenda anaweza hata kukuua pale anapoona anakufanyia vitimbi lkn bado umemng'ang'ania kama kupe

mwombe MUNGU atakupa mke mwema ambaye atakuwa faraja ya moyo wako kwani mke mwema hutoka kwa Mungu na sio kwa mbinu unazoumia. ukimwomba Mungu i happens automatically, hata ww utashangaa jinsi gani ilitokea hata ukakutana na mtu huyo ambaye hata amekuwa mke wako

Biblia inasema ni heri kuishi jangwani/nyikani kusiko na miti wala maji wala mazao ya chakula kuliko kuishi na mwanamke mgomvi/mpumbavu

hapo hakuna mke bali naona kahaba yuko mbele yako ukichelewa atakuua kwa ukimwi huyo
 
fanya uamuz ambao ni wa busara na ambao utakufanya uwe confortable huyo mwanamke hujazaliwa naye chukua hatua haraka coz itakucost.
 
i WISH NINGEPATA MUME KAMA WEWE AMBAYE UNAVULUNDA, UNAFANYA MADUDU LAKIINI UNANISAMEHE, MAISHA YANAKWENDA lOH! RAHA ILIOJE!!!!
 
pole mdau, huwezi lazimisha penzi hesabu tu kwamba ni challenge ya kimaisha na kwamba ni among the mistakes that you ever made.
Songa mbele piga moyo konde maisha uyashinde.
Mimi nina rafiki yangu yeye si raia wa tz lakini anafanya kazi hapa tz akapata mwanamke akanunua nyumba kwa jina la mwanamke, magari 2 kwa jina la mkewe. Mwisho alinyanganywa yote
 
Unataka afanye nini ujue hakutaki tena? Kwamba shida zake ushazitatua.....hakuhitaji tena!
Chapa lapa kijana....
 
Hilo si la kuomba ushauri! Labda nasaha tu kwako km unataka kuwaolea watu waje kukugongea baadae sawa.....
 
Ndo maana wengine tunachukua readymade (ambaye tayari ameshamaliza masomo) kuepuka mambo ya kutupa gharama halafu mwisho wa siku unaletewa dharau. Nukta.
 
Maelezo yako yamenikumbusha wimbo wa nani yule sijui........yanini malumbano, ya nini manenoo..... tena na yule mwingine aliyekubali yaishe....."ingawa rohoni.......namuomba mola anisadie, niweze kukusahau kabisa...nipate mwingine kukushinda wewe....". Pole best but that is the right thing to do.
 
Pole kaka just let her go atakuzingua sana kwenye ndoa malipo ni hapa duniani mbona yatamkuta mazito ye mnjanja sasa hivi ila baadae atakukumbuka,

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ulishawahi kujiuliza mtangulizi wako aliachana na huyo mwanamke kwa sababu zipi? Au unaposema huyo mtangulizi wako alikosa msimamo wa maisha unamaanisha nini? Kumbuka kwenye kila wanaoachana, kuna mchango wa kila mmoja. Hivyo ulitakiwa utafute sababu zilizochangiwa na huyo demu hadi akaachana na X wake.

Kwa sasa piga chini tu, we hesabu ile hela ulikunywa bia tu. Huyo ni pasua kichwa.
 
kuna dem mmoja nilipiga chini faster baada yakungundua ni kirusi ndani ya maisha yangu alipata zero meta sec. Nikamtafutia chuo cha ufundi cha ajabu alipohitimu siku tu amepata cheti kesho yake na kutana naye nyondo ilikuwa kubwa sana nikamwambia wewe utakula jeuri yako nilimwapia nikamwambia cheti hakika hutakitumia alicheka sana nikamwambia nenda kakifiche kuanzia leo ila nitakuja kukichukua. nilikichukua hakuamini alipokuja kuangalia alipoweka hakukikuta kesho asubuhi alikuwa kwangu. Viatu miguuni vilikuwa vimeshindikana kuvaliwa, aliliya kama amefiwa lakini hakika cheti hakukiona hadi leo. na huo ndio ulikuwa mwisho wa mimi kuwa karibu nami.
 
avatar47832_10.gif
huyu jombaa siku hizi yuko wapi? i hope atakuwa mzee sasa
 
kuna dem mmoja nilipiga chini faster baada yakungundua ni kirusi ndani ya maisha yangu alipata zero meta sec. Nikamtafutia chuo cha ufundi cha ajabu alipohitimu siku tu amepata cheti kesho yake na kutana naye nyondo ilikuwa kubwa sana nikamwambia wewe utakula jeuri yako nilimwapia nikamwambia cheti hakika hutakitumia alicheka sana nikamwambia nenda kakifiche kuanzia leo ila nitakuja kukichukua. nilikichukua hakuamini alipokuja kuangalia alipoweka hakukikuta kesho asubuhi alikuwa kwangu. Viatu miguuni vilikuwa vimeshindikana kuvaliwa, aliliya kama amefiwa lakini hakika cheti hakukiona hadi leo. na huo ndio ulikuwa mwisho wa mimi kuwa karibu nami.

Kamanda umenichekesha na kuniacha na maswali mengi sana!!

1. Ina maana mpaka leo hujampa tu hicho cheti chake?
2. Hivi unajua kuwa anaweza kupata cheti kingine kama akifuata process na kuripoti kuwa original kimeibiwa?
3. Vipi unafahamu alipo sasa? una mawasiliano nae?
 
::
Hata kama unampenda kuliko maisha yako
Weka distance nae utafute uamuzi unaokufaa.
::
Ndivyo walivyo wanawake wakijua unawapenda jeuri na sanaa haziishi.
=
 
The best solution drop her and forget all about her na kama cm yako ina namna ya kublock namba mblock kabisa au badili line asiweze kuwasiliana na wewe. Well unataka mke lakini sidhani kama huyo anafaa kuwa mke ila unamnganinia ili uokoe hasara ya tuition fee. kungangania kutakupeleka kwenye maisha ya kutatua matatizo na kuvumilia shida daily. wanawake ni wengi na huhitaji kusomesha ili upate mke. tulia maliza chuo rudi mtaani panga maisha siku ikifika Mungu atakupa wa kwako kwani hapo unaonekana unalazima ubavu wa mtu mwingine uwe wako kitu ambacho kitakucost maisha. Drop her and make the best for yourself hana hata mwaka atakuja kwako analia na wakati huo utakuwa umeshampata madam right so utakachoweza kufanya ni kumwekea mikono na kumwombea kwa Mungu akili itoke tope la usaliti na ujinga ili akapate maisha mazuri huko mbele.
 
Back
Top Bottom