Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,027
Baada ya kuapply tangazo lao la kazi huko Uranium Songea,fasta wakanipigia simu wakadai wapo kwenye mchakato wa kuita watu kwenye interview lakini tutangulize kwanza laki 2 kwa M-PESA, nikawakubalia...nikaja hapa jamvini kuhoji uhalali wa hii kampuni kwa kiasi kikubwa hivyo kabla hata hatuajiriwa. Nikachukua mawazo yote ya wanaJF, nikatengeneza maswali yangu kadhaa naomba uyajibu.
Halafu nikampandia hewani yule jamaa aliyejitambulisha kama Ishe Mboma, simu ikaitaaaa weeee, hadi ikakatika haikupokelewa. Baada ya kama dakika 5simu yangu ikaaza kuita, kucheki yule jamaa ananipigia. Nikapokea!!
Maongezi yakaanza kama ifuatavyo: Nilianza kumwambia kwamba nina fedha mkononi na nipo dukani Mpesa tayari kuzituma, ila nina mawali matatu tu naomba uyajibu kabla sijatuma.
Swali la kwanza nilimuuliza, Je hiyo ni kampuni au ni Recruitment Agent(RA)? Akanijibu yeye ni HR wa ndani ya kampuni na sio RA.
Nikamuuliza huo mgodi unaochimba Uranium upo wapi? Akanijibu upo songea na mpaka kijiji akanitajia...Nikamuuliza Wewe mwenyewe na hiyo kampuni mpo wapi(nikajua wapo dar)..akanijibu wapo Songea mjini 2 km kutoka pale mjini.
Nikamwambia kama upo Songea basi na mie nipo hapohapo Songea unaonaje tukionana halafu nikakukabidhi mzigo ana kwa ana....!!
Hapo jamaa aliniachia vumbi baya!! Akaniambia ''This thing is very confidential and we are not allowed to have personal meeting'' Nikamwambia NIMEKUKAMATA MWIZI MKUBWA WEWE. AKAKATA SIMU.
SO TUWENI MAKINI JAMANI NA HAWA JAMAA WANAOTOA KAZI HALAFU WANATAKA FEDHA KWANZA, BILA KUJA HAPA JF NISINGEPATA MAWAZO YA KUULIZA STRONG QESTION YULE BWANA,MANAKE ALISHANIBAMBA.
Halafu nikampandia hewani yule jamaa aliyejitambulisha kama Ishe Mboma, simu ikaitaaaa weeee, hadi ikakatika haikupokelewa. Baada ya kama dakika 5simu yangu ikaaza kuita, kucheki yule jamaa ananipigia. Nikapokea!!
Maongezi yakaanza kama ifuatavyo: Nilianza kumwambia kwamba nina fedha mkononi na nipo dukani Mpesa tayari kuzituma, ila nina mawali matatu tu naomba uyajibu kabla sijatuma.
Swali la kwanza nilimuuliza, Je hiyo ni kampuni au ni Recruitment Agent(RA)? Akanijibu yeye ni HR wa ndani ya kampuni na sio RA.
Nikamuuliza huo mgodi unaochimba Uranium upo wapi? Akanijibu upo songea na mpaka kijiji akanitajia...Nikamuuliza Wewe mwenyewe na hiyo kampuni mpo wapi(nikajua wapo dar)..akanijibu wapo Songea mjini 2 km kutoka pale mjini.
Nikamwambia kama upo Songea basi na mie nipo hapohapo Songea unaonaje tukionana halafu nikakukabidhi mzigo ana kwa ana....!!
Hapo jamaa aliniachia vumbi baya!! Akaniambia ''This thing is very confidential and we are not allowed to have personal meeting'' Nikamwambia NIMEKUKAMATA MWIZI MKUBWA WEWE. AKAKATA SIMU.
SO TUWENI MAKINI JAMANI NA HAWA JAMAA WANAOTOA KAZI HALAFU WANATAKA FEDHA KWANZA, BILA KUJA HAPA JF NISINGEPATA MAWAZO YA KUULIZA STRONG QESTION YULE BWANA,MANAKE ALISHANIBAMBA.