Hot27
JF-Expert Member
- Oct 31, 2020
- 308
- 422
Habarini za muda huu nduguzangu wa Jamii Forum.
Niende moja kwa moja kwenye Mada kuelezea vile nimepata kujionea utofauti wa jiji la Mwanza tangu siku yangu ya kwanza tu kufika.
Safari ilikuwa ngumu mpaka nikajiuliza nina mkosi maana gari liliharibika mara tatu, hatimaye majira ya saa nane za usiku ndio nikafika Mwanza, Jiji nililokuwa nalisikia tu na kupata sifa nyingi ila sijawahi kufika.
Siku yangu ya kwanza niliona mambo mengi tafauti na Dar es salaam au jiji la Daudi. Watu wa Mwanza ni wakarimu mno ani ukimuuliza anaweza kukujibu vizuri, Makonda na Madereva daladala wako vizuri nilipanda daladala nakaribia kufika kituoni nikasimama akaniambia kaa mpaka gari lisimame ani nilishazoea Dar gari hata halijasimama vizuri utasikia konda anamwambia dereva twende.
Mwanza kuna mandhari nzuri na hali ya hewa safi. Navutiwa zaidi na mawe hasa yaliyo karibu na nyumba, unakuta nyumba imejengwa nyuma kuna bonge la jiwe..
Enewei nina wiki tu jijini Mwanza anayejua maeneo mazuri ya kuvutia maana napenda sana kutalii. Ahsanteni
KichWa bOX
Niende moja kwa moja kwenye Mada kuelezea vile nimepata kujionea utofauti wa jiji la Mwanza tangu siku yangu ya kwanza tu kufika.
Safari ilikuwa ngumu mpaka nikajiuliza nina mkosi maana gari liliharibika mara tatu, hatimaye majira ya saa nane za usiku ndio nikafika Mwanza, Jiji nililokuwa nalisikia tu na kupata sifa nyingi ila sijawahi kufika.
Siku yangu ya kwanza niliona mambo mengi tafauti na Dar es salaam au jiji la Daudi. Watu wa Mwanza ni wakarimu mno ani ukimuuliza anaweza kukujibu vizuri, Makonda na Madereva daladala wako vizuri nilipanda daladala nakaribia kufika kituoni nikasimama akaniambia kaa mpaka gari lisimame ani nilishazoea Dar gari hata halijasimama vizuri utasikia konda anamwambia dereva twende.
Mwanza kuna mandhari nzuri na hali ya hewa safi. Navutiwa zaidi na mawe hasa yaliyo karibu na nyumba, unakuta nyumba imejengwa nyuma kuna bonge la jiwe..
Enewei nina wiki tu jijini Mwanza anayejua maeneo mazuri ya kuvutia maana napenda sana kutalii. Ahsanteni
KichWa bOX