Ushimen
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 42,566
- 105,395
Salam kwenu wana jamvi.
Mtanivumilia kwa urefu wa habari hii.
Niliwahi kuwa kwenye mahusiano na mdada ambae alikua na mtoto mmoja, huku nami nilikuwa na watoto wawili (mapacha). Wakati wote wa mahusiano wetu tulikubaliana kuwapeleka watoto wetu wakasome kwenye shule moja na niliamua kua namlipia ada pia kama wanangu.
Na wakati wote wa mahusiano yetu tulikua tukiishi mbali mbali nikimaanisha kila mmoja akiwa nyumbani kwake.
Shida ilikuja baada ya kuhisi ninachepuka na mdada mwingine hali iliopelekea kutofautiana na kuvunja mahusiano yetu kabisa. Baada ya muda x-wangu alipata mchumba na pasipo kuchelewa jamaa akamuoa na maisha yakaendelea.
Matatizo yalianza pale mume wa x-wangu alipogundua kua namlipia ada mtoto wa mke wake na kipindi cha likizo ya watoto waliporudi toka shule, yule mtoto wa x-wangu aligoma kwenda kwa mama yake na alikatalia kubaki nyumbani kwangu kwakua walikua tayari wamezoeana na watoto wangu, huku wakimuita dada kwani alikua amewazidi umri.
Hali hii ilianza kuleta mgogoro kwenye ndoa ya x- wangu hadi kupelekea yule jamaa kuanza kutoa maneno ya vitisho kwangu. Na wakati haya yakitokea kuhusu migogoro mimi sikuwepo Tanzania, zaidi nilikua nikipata taarifa kutoka kwa watu wa karibu.
Niliona isiwe tabu, nikaamua nimtext x- wangu kwamba nikirudi likizo nitamtoa mtoto wake shuleni na nitamrudisha kwake maana sihitaji wema uniponze.
Kipindi niliporudi likizo nilifanya taratibu zote na nikamfuata mtoto shuleni na nikaenda kumkabidhi kwa wazazi wa x, mbele ya mjumbe, x na mumewe na wazazi wa x. Pia niliomba tukabidhiane kwenye maandishi kwa sababu ya kujiweka upande salama.
Cha kushangaza mtoto yule (binti) alilia sana na huku aking'ang'ania kwamba nisimuache, hakika mtoto yule alilia hadi wote tukajiskia huzuni kubwa. Ilibidi nimdanganye mtoto kwamba nitamfuata baada ya kuwasalimia bibi na babu yake.
Siku ya tatu sasa imepita, naambiwa binti (mtoto) yule amefariki dunia kwa kujirusha kwenye kisima cha maji.
HAKIKA NIMEUMIZWA SANA NA TUKIO HILI
Mtanivumilia kwa urefu wa habari hii.
Niliwahi kuwa kwenye mahusiano na mdada ambae alikua na mtoto mmoja, huku nami nilikuwa na watoto wawili (mapacha). Wakati wote wa mahusiano wetu tulikubaliana kuwapeleka watoto wetu wakasome kwenye shule moja na niliamua kua namlipia ada pia kama wanangu.
Na wakati wote wa mahusiano yetu tulikua tukiishi mbali mbali nikimaanisha kila mmoja akiwa nyumbani kwake.
Shida ilikuja baada ya kuhisi ninachepuka na mdada mwingine hali iliopelekea kutofautiana na kuvunja mahusiano yetu kabisa. Baada ya muda x-wangu alipata mchumba na pasipo kuchelewa jamaa akamuoa na maisha yakaendelea.
Matatizo yalianza pale mume wa x-wangu alipogundua kua namlipia ada mtoto wa mke wake na kipindi cha likizo ya watoto waliporudi toka shule, yule mtoto wa x-wangu aligoma kwenda kwa mama yake na alikatalia kubaki nyumbani kwangu kwakua walikua tayari wamezoeana na watoto wangu, huku wakimuita dada kwani alikua amewazidi umri.
Hali hii ilianza kuleta mgogoro kwenye ndoa ya x- wangu hadi kupelekea yule jamaa kuanza kutoa maneno ya vitisho kwangu. Na wakati haya yakitokea kuhusu migogoro mimi sikuwepo Tanzania, zaidi nilikua nikipata taarifa kutoka kwa watu wa karibu.
Niliona isiwe tabu, nikaamua nimtext x- wangu kwamba nikirudi likizo nitamtoa mtoto wake shuleni na nitamrudisha kwake maana sihitaji wema uniponze.
Kipindi niliporudi likizo nilifanya taratibu zote na nikamfuata mtoto shuleni na nikaenda kumkabidhi kwa wazazi wa x, mbele ya mjumbe, x na mumewe na wazazi wa x. Pia niliomba tukabidhiane kwenye maandishi kwa sababu ya kujiweka upande salama.
Cha kushangaza mtoto yule (binti) alilia sana na huku aking'ang'ania kwamba nisimuache, hakika mtoto yule alilia hadi wote tukajiskia huzuni kubwa. Ilibidi nimdanganye mtoto kwamba nitamfuata baada ya kuwasalimia bibi na babu yake.
Siku ya tatu sasa imepita, naambiwa binti (mtoto) yule amefariki dunia kwa kujirusha kwenye kisima cha maji.
HAKIKA NIMEUMIZWA SANA NA TUKIO HILI