Nimetukanwa jamani...msaada wenu.

Nimetukanwa jamani...msaada wenu.

Going Concern

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2011
Posts
1,071
Reaction score
1,213
Kuna mtu kanitukana, ni mtoto wa kike... nimetafuta kwenye kamusi ya kiswahili nimekosa...sina raha kabisa hapa nilipo, mpaka nijue maana yake... tunaongea vizuri tu mara akaniambia "Inahuu" ebu fanya yako....maneno mengine mie sina tatizo nayo, nataka nijue tu ili neno..........." inahuuu".
 
Hapana... kwani mtu anaetongoza mara nyingi upata jibu kama ilo?

Maana yangu ingekua unampa mistari , kisha ukapewa vijineno kama hivyo ningekushauri uendelee "kupiga mulemule" hizo ni ishara za kula mzigo mapema .
 
"...inahuu" ni msemo wa "kimpasho" imetokana na neno "inahusu" - inahusu!? Matumizi yake labda iwe yameanza kubadirika. Mfano: kituo cha 'drive-inn cinema' kuanza kuitwa 'drive inn' na hatimaye 'drai' (dry)...
 
"...inahuu" ni msemo wa "kimpasho" imetokana na neno "inahusu" - inahusu!? Matumizi yake labda iwe yameanza kubadirika. Mfano: kituo cha 'drive-inn cinema' kuanza kuitwa 'drive inn' na hatimaye 'drai' (dry)...

Ongeza na :
> Arusha - Chuga
> Marekani - Unyamwezini
> Tanzania - Bongo .
 
"...inahuu" ni msemo wa "kimpasho" imetokana na neno "inahusu" - inahusu!? Matumizi yake labda iwe yameanza kubadirika. Mfano: kituo cha 'drive-inn cinema' kuanza kuitwa 'drive inn' na hatimaye 'drai' (dry)...

kwanini sasa asinambie tu Inahusu mpaka aweke misemo yake ya mipasho? leo ntalala polisi we ngoja..
 
kwanini sasa asinambie tu Inahusu mpaka aweke misemo yake ya mipasho? leo ntalala polisi we ngoja..



Pole kaka mi jioni moja narudi home na kimkweche changu nasikia konda wa daladala ananiambia oya acha kumbwelambwela,nilitamani kushuka nipigane.Maana ni bora unitusi nikakuelewa kuliko kunitusi halafu nisielewe maana yake...
 
Pole kaka mi jioni moja narudi home na kimkweche changu nasikia konda wa daladala ananiambia oya acha kumbwelambwela,nilitamani kushuka nipigane.Maana ni bora unitusi nikakuelewa kuliko kunitusi halafu nisielewe maana yake...

umeona Mkuu? yani acha nikalale polisi.... Eti inahuu?
 
Pole kaka mi jioni moja narudi home na kimkweche changu nasikia konda wa daladala ananiambia oya acha kumbwelambwela,nilitamani kushuka nipigane.Maana ni bora unitusi nikakuelewa kuliko kunitusi halafu nisielewe maana yake...

shikamoo!za kupotea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom