Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
Wadau, wakati nipo chuo nilikutana na mrembo mmoja tukiwa mwaka mmoja lakini vitivo tofauti, tukaanzisha uhusiano wa kimapenzi, tulipomaliza chuo mwaka jana tukawa tumepangwa vituo vya kazi ktk mikoa tofauti, lakini tukawa tunawasiliana huku kila mmoja wetu akimpa hope mwenziwe kuwa ndio wake wa maisha, lakini juzi nilimtaarifu kuwa naenda kwake(Iringa) ambako ndo kituo chake cha kazi kilipo, akanijibu kuwa ana safari hivyo nisije. Nikawa kichwa nazi nikaja jana, nikampigia simu akaja hapa hotelini nilipofikia, nikaanza kukagua simu yake ya mkononi ili nijiridhishe lakini nilikuta message za mapenzi kama za wanaume 6 tofauti huku message yangu hata moja hamna, zote kafuta. Nilipomuuliza kuhusu safari kajibu kuwa "pole sana kwa yote". Nimeshangaa zaidi jana alivyokuwa anarudi kwake jioni ile hakuthubutu hata kunikaribisha kwake, leo asubuhi kaja hapa chumbani(hotelini) asubuhi tangu saa 4 analia tu hadi muda huu huku hatoi hata neno moja kila nikimuuliza sababu ya kulia huku hata mimi akinitia woga, kajibu tu "sistahili kuwa hata mbwa wako, mi sikufai, pole kwa ukatili niliokufanyia". Je wadau huyu binti nimfanyeje? Na mimi nimependa?