Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 22,801
- 43,177
Habarini za jioni,
Wengi wenu JF wanafahamu Kasie si mdau wa siasa, imetokea tu nipo mahali nikajikuta nashuhudia hii habari ya Mh. Sumaye kurudi CCM. I was like what the hell is going on!
Mchana wa leo nimeshuhudia Mheshimiwa Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya tatu Bw. Fredrick Sumaye akipokea kadi ya CCM huko Dodoma huku amevaa vazi la CCM.
Akili ya Kasie ikaniambia, huyu baba ni mmoja wa waliotumwa kwenda CHADEMA kuvuruga?
Ina maana CHADEMA ilikuwa ni tishio kiasi hicho? au watu wanafata maslahi? na kama wanafata maslahi inamaana CHADEMA pia kulikuwa na maslahi na sasa yameisha na wanarudi CCM?
Hivi hata mtu aliyefika nyadhifa za juu bado anatafuta maslahi huku na huko?
Kama ndivyo mbona hakuna wanaotoka vyama upinzani na kwenda kuvuruga CCM kisha warudi CHADEMA? au wapo ila nilipitwa.... yaani najiuliza maswali halafu nakosa majibu khaaaah...
Nimejikuta nakumbuka usemi wa, ukianza kula nyama ya mtu huachi kamwe.... na ukianza kuhama hama makanisa, huachi kamwe, na huku kuhamahama vyama vya siasa jee.
Acha nirudi kwenye kada yangu ya Mahaba.
Kwaherini na muwe na siasa njema maana hata sielewi.
NB: Natumai mnajihadhari na mlipuko wa gonjwa la Covid19 linalotikisa dunia tangu mwaka jana mwishoni. Naomba niendelee kusisitiza, msiache kunawa mikono, kutokutoka nje ya nyumba yako / ofisi iwapo mtoko huo sio lazima.
Na unapokuwa eneo la mjumuiko kilazima basi jitahidi kuwa walau mita moja mbali na binadamu mwingine na kutogusagusa mahala mahala (surfaces), bila kusahau kunawa mikono na sabuni kila mara kwa maji yanayotiririka. Sanitaiza iwe mbadala wa maji na sabuni.
Kasinde.
Wengi wenu JF wanafahamu Kasie si mdau wa siasa, imetokea tu nipo mahali nikajikuta nashuhudia hii habari ya Mh. Sumaye kurudi CCM. I was like what the hell is going on!
Mchana wa leo nimeshuhudia Mheshimiwa Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya tatu Bw. Fredrick Sumaye akipokea kadi ya CCM huko Dodoma huku amevaa vazi la CCM.
Akili ya Kasie ikaniambia, huyu baba ni mmoja wa waliotumwa kwenda CHADEMA kuvuruga?
Ina maana CHADEMA ilikuwa ni tishio kiasi hicho? au watu wanafata maslahi? na kama wanafata maslahi inamaana CHADEMA pia kulikuwa na maslahi na sasa yameisha na wanarudi CCM?
Hivi hata mtu aliyefika nyadhifa za juu bado anatafuta maslahi huku na huko?
Kama ndivyo mbona hakuna wanaotoka vyama upinzani na kwenda kuvuruga CCM kisha warudi CHADEMA? au wapo ila nilipitwa.... yaani najiuliza maswali halafu nakosa majibu khaaaah...
Nimejikuta nakumbuka usemi wa, ukianza kula nyama ya mtu huachi kamwe.... na ukianza kuhama hama makanisa, huachi kamwe, na huku kuhamahama vyama vya siasa jee.
Acha nirudi kwenye kada yangu ya Mahaba.
Kwaherini na muwe na siasa njema maana hata sielewi.
NB: Natumai mnajihadhari na mlipuko wa gonjwa la Covid19 linalotikisa dunia tangu mwaka jana mwishoni. Naomba niendelee kusisitiza, msiache kunawa mikono, kutokutoka nje ya nyumba yako / ofisi iwapo mtoko huo sio lazima.
Na unapokuwa eneo la mjumuiko kilazima basi jitahidi kuwa walau mita moja mbali na binadamu mwingine na kutogusagusa mahala mahala (surfaces), bila kusahau kunawa mikono na sabuni kila mara kwa maji yanayotiririka. Sanitaiza iwe mbadala wa maji na sabuni.
Kasinde.