kweli wewe sio mtu wa siasa ila huko ulikochagua kwenye mahaba kama panakufaa hivii, sasa kuhusu alichokifanya mh. Sumaye huku kwenye siasa wanaita DEMOKRASIA, na mh.hajakosea chochote ila ametumia haki yake vizuri.
Niendelee na moyo huu huu wakati sipewi kitu😜
Hata siku moja si mbaya ntakuwa nakata shurubati la kiwewe kwenye uno lakizee ila lakinyamwezi😋
Nakuapia utasahau hata ukiulizwa mwanasiasa hata mmoja hutamkumbuka ila utakumbuka kenzy ndie mtima wa nyongo,moyo na shina la huba lililojipandikiaza ktk viini vya kila mishipa yako😂
Wewe sio wa kufata nyuki ule asali,wewe ni wakufuata mzinga ule asali nyuki walishakuuma karne hizo now watakiwa kula hao nyuki na asali yake kipengo wewe😜
Nikiacha mimi atakuambia nani...? Mtaje kama yupo niitoe roho yake kwa jisu lenye makali kuwili..Hujaacha tuu makeke yako khaaa.... nimejikuta nacheka tuu eehehehheee.
Eeenh, nimefuatilia staili yako..., kama mzahamzaha hivi, na kumbe ujumbe mahsusi unauwasilisha.Wanakatisha tamaa wenye nia ya kuwa wanasiasa kweli na kulitumikia Taifa hili kwa utii.
Na Mzee Mangula naye aliambiwa hivyo hivyo pale Lumumba au?Aliambiwa sumu haionjwi kwa ulimi mkuu, wewe hapo ungebaki?
Na ukute alizoea kuonja vitu kadhaa kwa ulimi, mfano labda uviza kule.
Eeenh, nimefuatilia staili yako..., kama mzahamzaha hivi, na kumbe ujumbe mahsusi unauwasilisha.
Staili hiyo sijaona ikitumika sana katika jukwaa hili la JF.
Kuhusu hao wanaohamia CCM, wote, ikiwa ni pamoja na Ngoyai na wale wabunge wanaosemekana kununuliwa - hapa hapana shida ya kuelewa nia zao zilikuwa nini.
Lakini kwa huyu Sumaye, kusema kweli amewashangaza wengi. Mimi nadhani kalainishwa na mitikisiko aliyopata, yale mashamba n.k. Mwisho wa siku akaona hakuna namna, na hasa ukichukulia kuwa matumaini aliyokuwa nayo CHADEMA nayo ndiyo hivyo, yakawa matumaini hewa. Ikabidi amwage manyanga.
Najua husomi taarifa ndefu, nikiangalia aina ya uchangiaji wako, kwa hiyo nisikuchoshe, ila nikuache na hili wazo usiku huu:
Hivi walioko CCM huko leo hii, wakijikuta CCM imekwishapigwa chini (hata kwa miujiza)..., (nilitaka kufanya liwe swali, lakini naona linaelea).
Hebu wafikirie hawa wanachama kindaki ndaki wanaokula tunda la taifa leo hii kwa wao kuwepo huko CCM, hali itakuwaje wakifurumshwa?
Bado sipati njia bora..., acha na ibaki hivyo, nikitumaini utanielewa!
Nikiacha mimi atakuambia nani...? Mtaje kama yupo niitoe roho yake kwa jisu lenye makali kuwili..
Makeke nimerithi kwa babu! Tena alinifundisha na maneno matamu nikiyamwaga hapa kihoro kitakutoka bure!
Mi ntakapokukuta salamu yangu kwako busu bunifu,busu lenye husuda na kiherehere cha mahaba! Busu ambalo ni ama ukae au unyong'onyee kwa utamu wake!!
Mi ndio ile shekeli itafutwayo,shekeli iliyoshiba madini inayopendwa na vigoli bikira.. Kama uliwahi sikia ule usemi usemao usiache mbachao kwa msala upitao basi mimi ndimi hiyo mbachao!!
Mimi ndio reli yako ikitoka treni hutoenda kokote..
Nivike kidani chako cha huba nikupe utamu wako mahabuba😉