Nimeshikwa na Taharuki

Nimeshikwa na Taharuki

Nilishangaa kidogo na sikuweka uzi sababu niliona ni mpenda mageuzi kwelikweli na kwenda kwake Chadema nilikuchukulia kuwapa support, ujuzi au siri ndogondogo zinazotumiwa an CCM ili washinde ukizingatia yeye alikuwa CCM miaka kadhaa na sikuhofia kama alifata maslahi maana kufikia kuwa na wadhifa wa Waziri Mkuu wa nchi una nafasi ya kupata vingi tuu.

Ila tangu waliohama CCM na kuhamia Chadema badala ya kufanya Chadema kisonge mbele badala yake kimerudi nyuma na kuvurugwa na kuchanyatika ukijumlisha na Zito bin kuhamia ACT bin Slaa kukimbia nchi na mapicha picha ya kila rangi....

Nashangaa sababu wakati huu ndo Chadema kinahitaji msaada ili walau nacho kisimame kifua mbele kupambana na uchaguzi, badala yake wanahama na kurejea walikotoka...
CDM Ina nguvu kubwa kuliko unavodhania wewe Dada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli kada yako mahaba,kitu tushasahaugi!! Mi mwenyewe nimetaharukika... unipe haba moja basi roho intulie kasinde

Mweeh, na wewe unataka kamojaa tuu...

Usijali ngoja mwezi wa kenda ufike na upite.
 
Chadema kwenye propaganda ni vilema, ila pia intelijensia yao ni kiwete kabisa mwisho tamaa yao ndiyo kabuli lao.

Sent using Jamii Forums mobile app

Aiseeeh sas kama ndivyo, si watulie wajifunze namna ya kuenenda, maana kwa mtizamo walikuwa na nguvu kubwa sana ya uma, ila kwa jinsi picha zinavyoendelea wanapoteza nguvu ya uma hatimaye watakufa kifo cha mende... ndembendembe japo siwaombei hivyo najikuta nawaza kwa maneno na siko upande wowote wa siasa.
 
Umesema urudi kwenye kada yako yamahaba af mwishoni unatuonya tusigusane. Are you serious? maha gani bila kugusana?

Aahahahahahaaa Mahaba ya kugusana kikorona yaani tunagusana umbali wa mita moja hivi, pata picha denda lake linakuwaje aahahahahahahahahahaaaa

Kuna jamaa mmoja aliweka picha ni mwendo wa kujifunika na ndoo na mikono inakuwa kwenye maji halafu huko kwingine hakusababishi maambukizo hivyo baiskeli inanyongwa kama kawaida eeheheheheheheee

K' Matata.
 
Aahahahahaa Kenzy banaa, maneno haya ulipaswa uniambie huku wamparua samaki kisha wamchoma taratiibu akiwiva wamkatia kachumberi halafu usikaribish nile, nikishiba nawezajikuta nimelainika na nyimbo zako maana looh ahhahahaaa

Ila naomba uniunganishe na babu yako kwanza nisemeshane nae halafu ndo tusemeshane nawe.
Mwe! Babu yangu shababi atanizidi kete huunganishwi hata kwa kamba ya buibui! Huko ni sawa na kukuuza malaika.. nami utayari huo niutolee wapi..?
Labda utayari wa kumtoa mtu chongo ama kumfanya TOINYO.
 



Basi asante, nimeelewa. Shukria babujii.

Demokrasia Chadema imeshindikana akatoka akisema hatojiunga na chama chochote, kweli tangu Disemba hadi mwezi huu wa tatu ndo anasema juhudi zake za kutaka kurudi CCM zimekubaliwa...je nia hiari yake au amelazimishwa?? Kapicha flani hivii kasiko na amsha amsha sanaa.

Alamsiki.
 
CDM Ina nguvu kubwa kuliko unavodhania wewe Dada

Sent using Jamii Forums mobile app

Niliiona hiyo nguvu kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2015 na kipindi cha kutaka kufanya maandamano ya UKUTA.... Ungozi uliokuwa madarakani ulipambana kisawasawa hadi tusiofatilia siasa tukaona kweli nguvu ya uvutano ni kubwa.
 
Mwe! Babu yangu shababi atanizidi kete huunganishwi hata kwa kamba ya buibui! Huko ni sawa na kukuuza malaika.. nami utayari huo niutolee wapi..?
Labda utayari wa kumtoa mtu chongo ama kumfanya TOINYO.

Sasa babu yako akielewana na bibi kigagula Kasie kuna madhara??!!1 huoni utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kudeka kwa bibi yako wa kambo bila hofu na kwa uhuru wotee?? aahahahahahahhaaaaaa!!!
 
Naona siasa n mchezo ambao ukiuingia unashindwa kuacha, hua nashindwa kuelewa kwann wazee kama wale ambao washakua na nyadhifa kubwa wanajidharirisha? Nawaza tu ukiona umezinguliwa chama chako kaa nyumban fanya mambo mengine pamoja na kulea wajukuu.
Alitumwa kuiokoa Chichiemu
 
Aahahahahahaaa Mahaba ya kugusana kikorona yaani tunagusana umbali wa mita moja hivi, pata picha denda lake linakuwaje aahahahahahahahahahaaaa

Kuna jamaa mmoja aliweka picha ni mwendo wa kujifunika na ndoo na mikono inakuwa kwenye maji halafu huko kwingine hakusababishi maambukizo hivyo baiskeli inanyongwa kama kawaida eeheheheheheheee

K' Matata.
Aysee... bt inakuwa haina amsha amsha. Utamu ni pale ushirikiano unapokuwa full! Kila kiungo kifanye kazi yake. Tujiachie tu, sisi blacks hatuna shida ni mafua km mafua mengine.
 
Sasa babu yako akielewana na bibi kigagula Kasie kuna madhara??!!1 huoni utakuwa kwenye nafasi nzuri ya kudeka kwa bibi yako wa kambo bila hofu na kwa uhuru wotee?? aahahahahahahhaaaaaa!!!
Haya majibu yako natamani hata kukuuma! Ombi lako ni batili ndugu mteja tazama vyema ombi lako kabla mhusika hajakutoa mapengo nakadharika!!.

Nakuambia babu yangu shababi nimekutajia tu wamng'ang'ania! Ukiongea nae utakuwa huna nafasi ya kusema no!! Huu mjadala naufunga utaniuzi nimeze simu bure..
 
Nilishangaa kidogo na sikuweka uzi sababu niliona ni mpenda mageuzi kwelikweli na kwenda kwake Chadema nilikuchukulia kuwapa support, ujuzi au siri ndogondogo zinazotumiwa an CCM ili washinde ukizingatia yeye alikuwa CCM miaka kadhaa na sikuhofia kama alifata maslahi maana kufikia kuwa na wadhifa wa Waziri Mkuu wa nchi una nafasi ya kupata vingi tuu.

Ila tangu waliohama CCM na kuhamia Chadema badala ya kufanya Chadema kisonge mbele badala yake kimerudi nyuma na kuvurugwa na kuchanyatika ukijumlisha na Zito bin kuhamia ACT bin Slaa kukimbia nchi na mapicha picha ya kila rangi....

Nashangaa sababu wakati huu ndo Chadema kinahitaji msaada ili walau nacho kisimame kifua mbele kupambana na uchaguzi, badala yake wanahama na kurejea walikotoka...
Kwa nini isiwe Chadema ndio waliwatumia hawa wazee kujijenga na kunufaika kisiasa na walipopata walichokitaka wakawaona ni "ganda la muwa la jana..."
 
Nilishangaa kidogo na sikuweka uzi sababu niliona ni mpenda mageuzi kwelikweli na kwenda kwake Chadema nilikuchukulia kuwapa support, ujuzi au siri ndogondogo zinazotumiwa an CCM ili washinde ukizingatia yeye alikuwa CCM miaka kadhaa na sikuhofia kama alifata maslahi maana kufikia kuwa na wadhifa wa Waziri Mkuu wa nchi una nafasi ya kupata vingi tuu.

Ila tangu waliohama CCM na kuhamia Chadema badala ya kufanya Chadema kisonge mbele badala yake kimerudi nyuma na kuvurugwa na kuchanyatika ukijumlisha na Zito bin kuhamia ACT bin Slaa kukimbia nchi na mapicha picha ya kila rangi....

Nashangaa sababu wakati huu ndo Chadema kinahitaji msaada ili walau nacho kisimame kifua mbele kupambana na uchaguzi, badala yake wanahama na kurejea walikotoka...
Chadema/ upinzani huwa ni mawazo yaliyo ndani ya mioyo ya wananchi juu ya kutoridhika hasa na mfumo wa utawala ktk nchi kwa mfano wanachi hawaitaki hii katiba ya sasa kwani inamapungufu mengi haiendani na hali ya sasa ya ulimwengu hivyo hata kama mbowe atajiunga ccm bado hakuta jibu la kitendawili cha mahitaji ya wananchi hakuna mamluki wa kuibomoa chadema au upinzani kwa sasa mda umewaacha
 
Aiseeeh, basi nimepitwa ni vile si mfatiliaji wa siasa, lakini hiyo inanifanya nijiulize tena... mwanzoni aliondoka CCM kwenda Chadema ili afanyaje? lengo lake lilikuwa ni nini?

Kama angefika Chadema na kuwapa mawaidha namna ya kuenenda kama back up wangemfukuza?

Na kama hawakumsikiliza badala yake walimtumia na kumkera si angeondoka mwenyewe kabla ya kufukuzwa? Dalili ya mvua si inaonekana?

Well kuna akili inaniambiaga iko siku tutakuja kusikia Mbowe amehamia CCM.....!! sijui kwanini.
Wote waliohama ccm na kwenda chadema mamvi na mr zero waliamua kwautashi wao tena kwa dhati nakuhakikishia kama tanzania ingeendelea kuwa na siasa za kistaarabu kidogo kama zamani hawa wazee wasingerudi ccm kamwe ila kilichowarudisha ccm ni siasa chafu za kukomoana kutekana kufungana yaani matumizi mabaya ya dola kwa upinzani hicho tu hakuna cjui cha kutumwa kukiboa chadema ni mawazo yangu tu
 
Wee kipindi cha uchaguzi 2015 kwa kiasi flani nilivutwa na sekeseke na ushabiki wa uchaguzi. Nilichoweza kujizuia ni kutokuwa kwenye chama chochote ili nisiumie moyo/roho yangu, nilikuwa ikishinda Chadema sawa ikishinda CCM sawa cha muhimu amani iwepo tuendelee kufanya kazi na usiku Mahaba kwama kawaida (kwa sie wazee mchana na asubuhi hatuwezi kumahabika).

Picha hilo la siku CCM ikifa wanachama kindakindaki itakuwaje niliiona ile siku ya kusomwa majina 5 bora ya kinyang'anyiro cha uraisi ndani ya CCM, joto lilikuwa kali aiseeh mle ukumbini baada ya mamvi kutokutajwa weeeh...... ukumbi mzima ulinyweaaaaaaaa nywiiiiiii na wakati wanaingia walikuwa wanaimba kwa nguvu zotee TUNA IMANIII NA LOWAASAAA OOYAAA OYAAA OYAAAA....aahahahahahaa walifurahishwa aiseeh na wengine walilazwa kwa presha wakati Lowasa mwenyewe alikuwa katulia tuliii.

Well siasa pia ina hatua na inakua kama mtia unavyomea, mipasuko na migawanyiko hutokea kwa sababu kadha wa kadha ila inapotokea uma kusapraiziwa ndo hapooo....

Taharuki ingine iliyonisababisha nizidi kuweka mbali siasa na moyo wangu ni siku ile Jiwe anatangazwa kuwa ndo Raisi..... jiji la Dar lilipoa utasema kulitangazwa msiba kila kaya hakukuwa an shamra shamra kuwa Jiwe katangazwa..... ile sadness mie ndo sitaki inikumbe ila kuna mahali najikuta tuu mambo nayafahamu na yananiumiza kichwa aaghh.

Kuhusu makala nasoma sanaa hata iwe ndefu kama reli mradi iwe na mtiririko na kuvutia kuendelea kusoma maana hata mie huwa naandika kinachonijia kichwani nisipoamua kuweka nukta naweza andika page hata tatu.
Nimeelewa kwa nini vijana wanapotezana juu yako.

Ni mtam...tam aisieee 'kasie'.

Nawaza tu simulizi hizi zipoje pale kitandani, si ndio komesha! Aaah, basi hayo tuyaache. Hapa ni siasa tuu, kama Kazi Tuu!
 
Kwa nini isiwe Chadema ndio waliwatumia hawa wazee kujijenga na kunufaika kisiasa na walipopata walichokitaka wakawaona ni "ganda la muwa la jana..."

Yawezekana pia....

Japo kupitia maelezo ya baba Sumaye yaonesha kuna changamoto CDM, labda baba Mbowe nae aweke neno.
 
Back
Top Bottom