Jamani nashauri kama kuna mtu yeyote ana ndugu yake amemaliza form 4 mwaka jana...asijisumbue kumtafutia shule eti kusoma advance(form 5 na 6)...hiyo level ni ya matesobna kupoteza muda tu...
Cheti cha form 6 hakina kazi popote zaidi ya kuombea chuo tu degree...yaani hiyo ni hata ukifaulu...ukikosa mkopo basi na elimu yako mpaka form 6 huwezi enda kampuni yoyote ukaomba kazi ukapewa...
Lakini aliyemaliza form akaunga college yoyote inayotambulika kwa ubora akajiunga akasoma zake miaka 3(ambayo imeongezeka just miez kadhaa tu ya ule muda unaopoteza form 5 na 6)...akitoka anakuwa na cheti ambacho kina umuhimu popote...kwanza anapata ujuzi...pili anaajiriwa popote na anasikilizwa ukilinganishwa na aliyesoma form 6...tatu kupitia cheti hicho hicho cha DIPLOMA anaombea nafasi za DEGREE bila shida yoyote kama aliyemaliza form 6...
Yaani alisoma mpaka advance...akizingua chuoni...basi ndo hana namna...
Ila aliyesoma diploma...akizingua chuoni degree basi anaweza kutumia cheti chake cha diploma kusurvive mjini...
KWANZA UKUBALI UKATAE...MWENYE ELIMU YA DIPLOMA NDIYE ANAYEPATA AJIRA KWA WINGI NA HARAKA ZAIDI KULIKO MWENYE DEGREE...KWA SABABU...
1. Wenye degree maofisini ni Ma Attendants... Wenyewe ndio wafanyaji kazi...ukilinganisha na MABACHELOR HOLDERS ambao ni MaDecision Makers...
Sasa huwezi kuwa na madecision makers wengi na watendaji ni wachache...
2. Maboss wanawapenda madiploma hawasumbui mishahara na kujiona classic alafu ni wachapakazi...alafu ndio wengi...ila mabachelor holders ni WASUMBUFU..
NIMEJIONEA...
Sent using
Jamii Forums mobile app