Nimepewe urithi wangu mapema, nimechanganyikiwa

Nimepewe urithi wangu mapema, nimechanganyikiwa

Nimepata nyumba chamazi kwa ml 15 sasa nawaza hiyo inayobaki
Mnaomba ushauri bila kutaja conditions mnatutia uvivu, ngoja nikupe in general. Chukua milioni 10 weka fixed account miezi sita. Unabaki na 8M

Milioni 3 agiza incubator ya mayai si zaidi ya 2000 hivi hela hiyo inatosha kununua, kusafirisha hadi Dar endapo uko jiji hili. Hapo inabaki 5M

After a month hapo ushafanya research na unasubiri incubator ifike kwani itachukua kama 50 days from ordering day mpaka kushushwa bandarini mpaka godown, panga chumba maeneo ya Kimara au eneo lolote lenye wafugaji wengi wa kuku, itategemea na research yako. Lipa kama 100k per month, ukilipa kodi ya 6months ni 600k plus hela ya kununua vitu 1.4M jumla ni 2M, hakikisha hapo kuna eneo la kutosha na sio mjini sana. Unabaki na 3M.

Wakati huo toa 1M ya kutumia kwenye vitu vya kijinga, hela inawasha siku zote. Unabaki na 2M hiyo ishi nayo tu kazi yako kutotoreshea watu vifaranga. Utaongeza mambo mengine kwenye huo ujasiriamali.

After 6 months ushaijua biashara toa 10M ikuze. Hiyo ni idea moja tu, zipo nyingi
 
Kwakua tayari kuna mtu anajiita mzee wa upako, we unatakiwa ujiite mzee wa kuwapaka alafu utenge 1M kila wikendi uwe unatafuta viwete wa mchongo wawili unawapa posho ya elf 10 unawaombea hadi wapone, hadi 1M iishe unakua umewaombea viwete wa mchongo 100 tayari Ni mtaji huo, unasubiri faida sasa huku ukijiita mzee wa kuwapaka

Kama zumaridi ana wenge kiasi kile lakin watu wamemuamini maana yake mchongo uko kule
 
Hiyo hela ni nyingi ukituliza akili yako vizuri, Ila ndogo sana endapo utakuwa na papara.

Chakufanya hapo, chukua milioni nane zitie fixed account kwa muda wa miezi sita.

Halafu kwenye kumi zinazobaki, chukua milioni nne tafuta kiwanja sehemu ya pembeni kidogo na mjini Ila iwe na miundombinu muhimu kama barabara bila kusahau huduma za umeme na maji, Kwanini pembeni na mji? Huko utapata kiwanja kikubwa.

Zimebaki sita, kwenye hizo sita chukua Milioni moja kwa ajiri ya kutunza eneo lako( kiwanja ) yaani nunua mabanzi au mbao kadhaa zungushia Kama fence kulinda mipaka ya kiwanja chako.

Hapo kwenye kiwanja Kama una hobby ya kilimo na ufugaji basi vuta maji au chimba kisima kwa ajiri ya bustani na vilevile tengeneza mabanda mazuri kwa ajiri ya ufugaji wa kuku, mbuzi nk, yaani hapo pafanye kuwa kambi yako ya kukimbilia siku ukipigika.

Hapo zitakuwa zimebaki Kama M4 hivi Basi hiyo unaweza toa M3 ukajaribu biashara unayoipenda.

M1 iliyobaki ni kwa ajiri ya dhalura mbalimbali, na kutatua changamoto ndogondogo.

Hakikisha hela yako inatumika ktk vitu vinavyoonekana siku hadi siku, na ambayo vinaweza kuongezewa thamani zaidi Kama ardhi, mifugo, nyumba nk.



Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
1. Ziweke fixed kwanza huku ukipunguza na kufikiria kwa umakini.

Ziweke fixed hata miezi 3 huku uki brain storm.

2. Kila biashara inalipa ukihadithiwa.

Nachokushauri kwenye biashara "FOLLOW UR PASSION""

Au kama vipi Tuagize biaaa

#YNWA
Kwa hela hiyo fixed account kwa mwezi atakua anaingiza sio zaidi ya laki na arobaini ,hamna kitu
 
Mnaomba ushauri bila kutaja conditions mnatutia uvivu, ngoja nikupe in general. Chukua milioni 10 weka fixed account miezi sita. Unabaki na 8M

Milioni 3 agiza incubator ya mayai si zaidi ya 2000 hivi hela hiyo inatosha kununua, kusafirisha hadi Dar endapo uko jiji hili. Hapo inabaki 5M

After a month hapo ushafanya research na unasubiri incubator ifike kwani itachukua kama 50 days from ordering day mpaka kushushwa bandarini mpaka godown, panga chumba maeneo ya Kimara au eneo lolote lenye wafugaji wengi wa kuku, itategemea na research yako. Lipa kama 100k per month, ukilipa kodi ya 6months ni 600k plus hela ya kununua vitu 1.4M jumla ni 2M, hakikisha hapo kuna eneo la kutosha na sio mjini sana. Unabaki na 3M.

Wakati huo toa 1M ya kutumia kwenye vitu vya kijinga, hela inawasha siku zote. Unabaki na 2M hiyo ishi nayo tu kazi yako kutotoreshea watu vifaranga. Utaongeza mambo mengine kwenye huo ujasiriamali.

After 6 months ushaijua biashara toa 10M ikuze. Hiyo ni idea moja tu, zipo nyingi
Mil 10 fixed account kwa miezi 6 haizidi 360000
 
Wakubwa Kwema?

Kama kichwa cha Habari kinavyoeleza hapo juu
Mimi ni kijana wa miaka 24, nimepewa Urithi wangu mapema kiasi cha milion 18 net.

Nimeambia hizo pesa nikizifanyia ujinga ndiyo basi tena nitakuwa sina kitu kwa mzee sasa nimewaza kununua hata kijumba cha milioni 14 nje ya Dar es salaam hata cha vyumba viwili.

Halafu 4 inayobaki nijaribu kuitia kwenye biashara yoyote itakayoweza kuizalisha sasa wakuu napagawa kwa sababu sikujipanga nisaidie kwa lolote hiyo kwangu ndo karata ya mwisho
UKinunua nyumba umepotea tayar..... tqfuta fani yeyote ya kusomea veta... halafu hiyo milioni 14 weka fixed deposit kwanza kichwa kitulie
 
Mimi mwenyewe Nina eneo la urithi pia lipo zaidi ya ekari moja kwa hiyo nakutolea 40* 40 kwa hiyo 7m Ni tambarare pazuri
 
kwahiyo unatak ubaki kuwa boss peke yako

Sasa kama madogo wanaweza pewa 18m na hajui mzaz kazipataje hawezi kuchanga akili yake akajiendeleza huoni tuna tatizo kubwa zaidi ya kulaumu serikali kua ajira hakuna mfano halisi ndio huyu mleta mada kabla hajapewa hizo 18 ukichunguza vizuri alikua anasubiri aajiriwe ndio maana kapata hicho kidogo hajui afanyeje huyu hata ukimuajiri kwenye kampuni hakuletei faida hata kidogo vijana hawana ushindani na malengo ndio ziro kabisa
 
Sasa kama madogo wanaweza pewa 18m na hajui mzaz kazipataje hawezi kuchanga akili yake akajiendeleza huoni tuna tatizo kubwa zaidi ya kulaumu serikali kua ajira hakuna mfano halisi ndio huyu mleta mada kabla hajapewa hizo 18 ukichunguza vizuri alikua anasubiri aajiriwe ndio maana kapata hicho kidogo hajui afanyeje huyu hata ukimuajiri kwenye kampuni hakuletei faida hata kidogo vijana hawana ushindani na malengo ndio ziro kabisa

Siyo wote wachche wao bhna tupo vijana smart sana ila no support
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom